TMA yatabiri mafuriko, maporomoko mikoa 14, Dar ipo. Tahadhari yaathari kubwa kwa miundombinu na maisha

TMA yatabiri mafuriko, maporomoko mikoa 14, Dar ipo. Tahadhari yaathari kubwa kwa miundombinu na maisha

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema maeneo yanayopata mvua za chini ya wastani hadi juu ya wastani yanatarajiwa kuwa na matukio ya hali mbaya ya hewa, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
IMG_2708.jpeg

TMA imesema vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, yanayoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu, mazingira, mlipuko wa magonjwa pamoja na upotevu wa mali na maisha.

Mvua hizo zinatarajia kunyesha msimu wa masika Machi- Mei 2025 za chini ya wastani hadi wastani ni maeneo ya mikoa ya Pwani, Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Morogoro, Tanga, Dar es Salaam na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mikoa inayopata mvua za wastani hadi juu ya wastani ni mashariki mwa mikoa ya Simiyu na Mara.
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema maeneo yanayopata mvua za chini ya wastani hadi juu ya wastani yanatarajiwa kuwa na matukio ya hali mbaya ya hewa, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
View attachment 3211672
TMA imesema vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, yanayoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu, mazingira, mlipuko wa magonjwa pamoja na upotevu wa mali na maisha.

Maeneo yanayotarajiwa kunyesha mvua za chini ya wastani hadi wastani ni mikoa ya Pwani, Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Morogoro, Tanga, Dar es Salaam na visiwa vya Unguja na Pemba.

Mikoa inayopata mvua za wastani hadi juu ya wastani ni mashariki mwa mikoa ya Simiyu na Mara.

Hata hivyo, Mwananchi imemtafuta Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali, Hosea Ndagala kujua walivyojipanga iwapo hali hiyo itajitokeza.
Taarifa ya TMA haina tarehe wala nini, ama ni mvua za miaka kumi ijayo?
 
TMA wanatumika kupoza hali ya kisiasa inayoipa CHADEMA airtime kubwa


Matarajio :​

UPEPO MKALI NA MAWIMBI MAKUBWA​

ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi, Mtwara, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba..

SOMA KWA KINA :

TMA YATOA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA 2025 KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA MARA MBILI KWA MWAKA.​

TMA YATOA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA 2025 KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA MARA MBILI KWA MWAKA.


Dar es Salaam; Tarehe 23 Januari 2025;
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi Utabiri wa Msimu wa Mvua za Masika 2025 kwa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka.

Akizungumza wakati wa mkutano na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa Ubungo Plaza, Tarehe 23 Januari 2025, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Mwakilishi wa Kudumu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Changa alisema mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki pamoja na Mashariki mwa mikoa ya Mara na Simiyu huku mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zikitarajiwa katika maeneo ya Pwani ya Kaskazini, Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma na Ukanda wa Ziwa Victoria.


“Mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki pamoja na Mashariki mwa Mikoa ya Mara na Simiyu. Aidha, mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo ya Pwani ya Kaskazini, Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma na Ukanda wa Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga na magharibi mwa mikoa ya Simiyu na Mara) katika kipindi cha Msimu wa Masika, 2025.”

Alisema Dkt. Chang’a
Vilevile, taarifa hiyo imeelezea pia ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha mwezi Aprili sambamba na kutoa angalizo la matukio ya hali mbaya ya hewa ikiwemo vipindi vya mvua kubwa kujitokeza hata katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani.


Akizungumzia athari zinazoweza kujitokeza, Dkt. Chang’a alisema Mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika baadhi ya maeneo zinaweza kupelekea upungufu wa upatikanaji wa maji kwa matumizi ya majumbani, kilimo na ufugaji.


Ili kupata taarifa zaidi za utabiri huu, tembelea: https://www.meteo.go.tz/
 
Kimbilieni mbeya wajameni kabla room hazijajaa mje mbebe kipindupindu 🥴
 
Mwelekeo wa hali ya hewa kwa mwaka 2025

TAARIFA MPYA KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA KUHUSU MVUA ZA MASIKA KWA MWAKA 2025

Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Tanzania kizungumza wakati wa mkutano na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa Ubungo Plaza,

View: https://m.youtube.com/watch?v=xU_kwtW-dAo
..Tarehe 23 Januari 2025, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Mwakilishi wa Kudumu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Changa

Dr. LaLadislaus ubobezi kitaaluma

Dr. Ladislaus Chang’a has participated in the preparation of National Communication to the United Nation Framework Convention on Climate Change (UNFCCC), preparation of the National Climate Change Strategies and National Climate Change Communication Strategies, and review of the IPCC reports (AR4 and AR5, AR6).

He has computer skills and knowledge including programming language and statistical software such as FORTRAN and R.

He has participated in a number of climate change projects and consultancy. His particular strength includes good leadership skills and experience in climate change negotiation, and in chairing climate change negotiation meetings at UNFCCC and IPCC.

Dr. Chang’a is also working as a Part-time Lecturer at the University of Dar Es Salaam, teaching Climatology, Climate Monitoring and Prediction for BSc students, and the Science of Climate Change for MSc students. He is actively involved in supervision and mentoring of BSc, MSc and PhD students
 
TMA wanatumika kupoza hali ya kisiasa inayoipa CHADEMA airtime kubwa


Matarajio :​

UPEPO MKALI NA MAWIMBI MAKUBWA​

ANGALIZO la upepo mkali unaofikia kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayofikia mita 2 limetolewa kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wote wa pwani ya bahari ya Hindi (mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi, Mtwara, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba..

SOMA KWA KINA :

TMA YATOA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA 2025 KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA MARA MBILI KWA MWAKA.​

TMA YATOA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA MASIKA 2025 KWA MAENEO YANAYOPATA MVUA MARA MBILI KWA MWAKA.


Dar es Salaam; Tarehe 23 Januari 2025;
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa rasmi Utabiri wa Msimu wa Mvua za Masika 2025 kwa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka.

Akizungumza wakati wa mkutano na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa Ubungo Plaza, Tarehe 23 Januari 2025, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Mwakilishi wa Kudumu wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Changa alisema mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki pamoja na Mashariki mwa mikoa ya Mara na Simiyu huku mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zikitarajiwa katika maeneo ya Pwani ya Kaskazini, Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma na Ukanda wa Ziwa Victoria.


“Mvua za Wastani hadi Juu ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki pamoja na Mashariki mwa Mikoa ya Mara na Simiyu. Aidha, mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinatarajiwa katika maeneo ya Pwani ya Kaskazini, Kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma na Ukanda wa Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga na magharibi mwa mikoa ya Simiyu na Mara) katika kipindi cha Msimu wa Masika, 2025.”

Alisema Dkt. Chang’a
Vilevile, taarifa hiyo imeelezea pia ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha mwezi Aprili sambamba na kutoa angalizo la matukio ya hali mbaya ya hewa ikiwemo vipindi vya mvua kubwa kujitokeza hata katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani.


Akizungumzia athari zinazoweza kujitokeza, Dkt. Chang’a alisema Mvua za Wastani hadi Chini ya Wastani zinazotarajiwa katika baadhi ya maeneo zinaweza kupelekea upungufu wa upatikanaji wa maji kwa matumizi ya majumbani, kilimo na ufugaji.


Ili kupata taarifa zaidi za utabiri huu, tembelea: https://www.meteo.go.tz/
Habari ya wastani, juu au chini bila data au namba haitoshi. Lazima watu wajue huo wastani ni mm ngapi?
 
Taarifa ya TMA haina tarehe wala nini, ama ni mvua za miaka kumi ijayo?
soma vizuri, Tindo mbona uko hivi.... ndiyo maana unamshabikia mropokaji Lisu!
wameandika hivi......Mvua hizo zinatarajia kunyesha msimu wa masika Machi- Mei 2025
 
Back
Top Bottom