Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema maeneo yanayopata mvua za chini ya wastani hadi juu ya wastani yanatarajiwa kuwa na matukio ya hali mbaya ya hewa, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.
TMA imesema vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, yanayoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu, mazingira, mlipuko wa magonjwa pamoja na upotevu wa mali na maisha.
Mvua hizo zinatarajia kunyesha msimu wa masika Machi- Mei 2025 za chini ya wastani hadi wastani ni maeneo ya mikoa ya Pwani, Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Morogoro, Tanga, Dar es Salaam na visiwa vya Unguja na Pemba.
Mikoa inayopata mvua za wastani hadi juu ya wastani ni mashariki mwa mikoa ya Simiyu na Mara.
TMA imesema vipindi vya mvua kubwa vinatarajiwa kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, yanayoweza kusababisha uharibifu wa miundombinu, mazingira, mlipuko wa magonjwa pamoja na upotevu wa mali na maisha.
Mvua hizo zinatarajia kunyesha msimu wa masika Machi- Mei 2025 za chini ya wastani hadi wastani ni maeneo ya mikoa ya Pwani, Kigoma, Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Morogoro, Tanga, Dar es Salaam na visiwa vya Unguja na Pemba.
Mikoa inayopata mvua za wastani hadi juu ya wastani ni mashariki mwa mikoa ya Simiyu na Mara.