Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Ladislaus Chang’a ametangaza mwelekeo wa msimu wa mvua za masika zinazoanza Machi mpaka Mei, 2023 ambazo zinatarajiwa kuwa za wastani huku baadhi ya mikoa kuwa wastani na juu ya wastani.
MWENENDO WA MVUA ZA MSIMU (NOVEMBA, 2022 HADI APRILI, 2023) NA MWELEKEO WA MVUA ZA MASIKA (MACHI – MEI), 2023
Mwenendo wa mvua za Msimu (Novemba, 2022 hadi Aprili, 2023)
Mvua za Msimu zilizoanza mwezi Novemba, 2022 katika maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka (mikoa ya Dodoma, Singida, Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Ruvuma, Lindi, Mtwara na kusini mwa mkoa wa Morogoro) zilinyesha kwa kiwango cha wastani katika kipindi cha Novemba, 2022 hadi Januari, 2023. Mvua hizi zilitawaliwa na vipindi virefu vya ukavu hususan mwezi Novemba, 2022 kwa maeneo ya pwani ya kusini, na kusini mwa mkoa wa Morogoro. Katika kipindi kilichosalia cha msimu (Februari, Machi na Aprili) mvua zinatarajiwa kuendelea kama ilivyotabiriwa mwezi Oktoba, 2022.
Mwelekeo wa mvua za Masika (Machi hadi Mei), 2023
Msimu wa mvua za Masika ni mahususi kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro), pwani ya kaskazini (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mikoa ya Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba), ukanda wa Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara) pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma.
Kutokana na mifumo ya hali ya hewa inayotarajiwa katika kipindi cha msimu (kama inavyoelezwa katika kipengele cha 2 cha taarifa hii), kwa ujumla mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga pamoja kisiwa cha Pemba katika msimu wa mvua za Masika, 2023. Hata hivyo, mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani (ikiwemo visiwa vya Mafia), kaskazini mwa mkoa wa Morogoro na kisiwa cha Unguja. Ongezeko la mvua linatarajiwa mwezi Mei, 2023 katika maeneo hayo. Maelezo ya kina juu ya mwelekeo wa mvua hizo za msimu ni kama ifuatavyo:
Kanda ya Ziwa Victoria: (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, na Mara) pamoja na kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma (wilaya za Kakonko na Kibondo):
Mvua za Masika zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani katika maeneo mengi ya ukanda wa Ziwa Victoria pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma. Mvua hizo zinatarajiwa kuanza wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Machi, 2023 na zinatarajiwa kuisha wiki ya nne ya mwezi Mei, 2023.
Ukanda wa Pwani ya Kaskazini: (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mkoa wa Pwani (ikijumuisha kisiwa cha Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba):
Mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani (ikiwemo visiwa vya Mafia), kaskazini mwa mkoa wa Morogoro na kisiwa cha Unguja.
Aidha, mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa kunyesha katika maeneo ya mkoa wa Tanga pamoja kisiwa cha Pemba. Mvua hizo zinatarajiwa kuanza wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Machi, 2023 na kuisha Juni, 2023.
Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki: (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro):
Mvua katika maeneo haya zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani na zinatarajiwa kuanza wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Machi, 2023. Mvua hizo zinatarajiwa kuisha wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Mei, 2023.
Mwenendo wa mvua za Msimu (Novemba, 2022 hadi Aprili, 2023)
Mvua za Msimu zilizoanza mwezi Novemba, 2022 katika maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka (mikoa ya Dodoma, Singida, Kigoma, Tabora, Katavi, Rukwa, Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Ruvuma, Lindi, Mtwara na kusini mwa mkoa wa Morogoro) zilinyesha kwa kiwango cha wastani katika kipindi cha Novemba, 2022 hadi Januari, 2023. Mvua hizi zilitawaliwa na vipindi virefu vya ukavu hususan mwezi Novemba, 2022 kwa maeneo ya pwani ya kusini, na kusini mwa mkoa wa Morogoro. Katika kipindi kilichosalia cha msimu (Februari, Machi na Aprili) mvua zinatarajiwa kuendelea kama ilivyotabiriwa mwezi Oktoba, 2022.
Mwelekeo wa mvua za Masika (Machi hadi Mei), 2023
Msimu wa mvua za Masika ni mahususi kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro), pwani ya kaskazini (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mikoa ya Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba), ukanda wa Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara) pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma.
Kutokana na mifumo ya hali ya hewa inayotarajiwa katika kipindi cha msimu (kama inavyoelezwa katika kipengele cha 2 cha taarifa hii), kwa ujumla mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga pamoja kisiwa cha Pemba katika msimu wa mvua za Masika, 2023. Hata hivyo, mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Dar es Salaam, Pwani (ikiwemo visiwa vya Mafia), kaskazini mwa mkoa wa Morogoro na kisiwa cha Unguja. Ongezeko la mvua linatarajiwa mwezi Mei, 2023 katika maeneo hayo. Maelezo ya kina juu ya mwelekeo wa mvua hizo za msimu ni kama ifuatavyo:
Kanda ya Ziwa Victoria: (Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, na Mara) pamoja na kaskazini mwa Mkoa wa Kigoma (wilaya za Kakonko na Kibondo):
Mvua za Masika zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani katika maeneo mengi ya ukanda wa Ziwa Victoria pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma. Mvua hizo zinatarajiwa kuanza wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Machi, 2023 na zinatarajiwa kuisha wiki ya nne ya mwezi Mei, 2023.
Ukanda wa Pwani ya Kaskazini: (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mkoa wa Pwani (ikijumuisha kisiwa cha Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba):
Mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani (ikiwemo visiwa vya Mafia), kaskazini mwa mkoa wa Morogoro na kisiwa cha Unguja.
Aidha, mvua za wastani hadi chini ya wastani zinatarajiwa kunyesha katika maeneo ya mkoa wa Tanga pamoja kisiwa cha Pemba. Mvua hizo zinatarajiwa kuanza wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Machi, 2023 na kuisha Juni, 2023.
Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki: (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro):
Mvua katika maeneo haya zinatarajiwa kuwa za wastani hadi chini ya wastani na zinatarajiwa kuanza wiki ya pili na ya tatu ya mwezi Machi, 2023. Mvua hizo zinatarajiwa kuisha wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Mei, 2023.