TMA yatabiri uwepo wa mvua kubwa kubwa kwenye mikoa 11 kuanzia leo

TMA yatabiri uwepo wa mvua kubwa kubwa kwenye mikoa 11 kuanzia leo

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza utabiri wa mvua kubwa katika mikoa 11, itakayoanza leo, Novemba 30, hadi Desemba 1, 2024.

Maeneo yatakayoni mikoa ya Nyanda za Juu Kusini (Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, na Rukwa), ukanda wa Pwani ya Kusini mwa Bahari ya Hindi (Lindi na Mtwara), Kanda ya Kati (Dodoma na Singida), Kanda ya Kusini (Ruvuma), pamoja na Mkoa wa Morogoro.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA leo, Novemba 29, 2024, hali mbaya ya hewa inatarajiwa kuendelea kwa siku tano kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 3, 2024.

Mamlaka imewataka wakazi wa maeneo husika kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa zaidi kuhusu hali ya hewa.

TMA Mvua.png


Source: Mwananchi
 
Kwa leo wamepatia utabiri wao mvua kubwa imenyesha mkoa nilipo. Kwa sisi watu wa asili huwa tupo mbele kusoma hali ya hewa kwa siku nzima, wiki, mwezi na hata mwaka, hatusubiri utabiri wao wa kubahatisha, ila tuwasikilize maana ndio wenye mamlaka ya kutangaza hali ya hewa
 
TMA nawafatilia sana tuwape maua yao asilimia 80 wakiongea uwa ni kweli.
 
Back
Top Bottom