To You..

kwa vina hivo klorokwini lazima uopoe kimwana JF...afu wanajiletaga wenyewe... Nakuonea wiiiiivuuuuu
 


sema mwana sema,kati weka songa mbele,
nilizani wewe kihema,kosa ni langu milele,
samahani mwana nasema,kamwe si kihelehele,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,

Sante mwana kunirusha,hapo yote kumi juu,
nilianzia upusha,sione sa niko juu,
kamwe sijapata gusha,twende mambo juu,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,

Wanitajia asidi,kwa fani ndie kuwadi,
umemsahau judi,mwadada asi miadi,
mwanajamii kinadi,klorokwini sinadi,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,

mimi sie sharobaro,wala yule wake wema,
kwangu wale ni viharo,mwadui mpaka kahama,
kwa arumasi vinaro,dhahabu hadi kiama,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,

acha nirushe miaki,kwako mwana wa heri,
nipe stari mikiki,kloro rusha shairi,
pagawisha mpaka diki,afe asiye himiri,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,
 

Lizzy mama nakumisi,zawadi yako mezani,
watoto walopromisi,ya mama siku yajani,
kwangu mama una kesi,kutulizia tandani,
Babu kaachia ngazi,njoo uwanja ni wetu,

wino wake ni hafifu,kwishneli ninasema,
mwache awe mtiifu,kwa bibi mzaa mama,
kamwe hakuwa dhaifu,alishusha dinadama,
Babu kaachia ngazi,njoo uwanja ni wetu,
 

lizzy kamwaga mboga,aspirini ugari,
mimi nitamwaga chenga,tuone nani sukari,
klorokwini malenga,kwa vina na mistari,
Bongo flava ni wezi,waiselady tulia,

kamwe usije mdipu,babu lazima apige,
Tigo voda yeye kipu,ukome mpaka uringe,
salimia yule taripu,mwambie nipo samunge,
Bongo fleva ni wezi,waiselady tulia,
 
Klorokwini naona unafata nyayo za bujibuji sasa teh! Umejitahidi kwa mashairi, nimegonga tano hapo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…