Vina bado vijaisha, Hakika nakuambia,
Vina ni yao maisha, Hawa naokutajia.
Klorokwini anatisha, Kunaye na lizzy pia,
Vina havijatuisha, majukumu yamebana.
Tunaye Magalumangu, Vina mejaa kichwani,
Kipaji kampa Mungu, Kamleta kwenye fani,
Ukija na hapa kwangu, Vimejaa ubongoni,
Vina havijatuisha, Majukumu yamebana
Mwanajamii wani, Acid nakutajia,
Ni magwiji kwenye fani, muda umewabania,
Mwanakijiji kundini, Teamo anafwatia,
Vina havijatuisha, Majukumu yamebana.
sema mwana sema,kati weka songa mbele,
nilizani wewe kihema,kosa ni langu milele,
samahani mwana nasema,kamwe si kihelehele,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,
Sante mwana kunirusha,hapo yote kumi juu,
nilianzia upusha,sione sa niko juu,
kamwe sijapata gusha,twende mambo juu,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,
Wanitajia asidi,kwa fani ndie kuwadi,
umemsahau judi,mwadada asi miadi,
mwanajamii kinadi,klorokwini sinadi,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,
mimi sie sharobaro,wala yule wake wema,
kwangu wale ni viharo,mwadui mpaka kahama,
kwa arumasi vinaro,dhahabu hadi kiama,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,
acha nirushe miaki,kwako mwana wa heri,
nipe stari mikiki,kloro rusha shairi,
pagawisha mpaka diki,afe asiye himiri,
Vina kwetu vikiisha,gamba na tutalivua,