Toaneni 'out' kwa uhai wa uhusiano wenu

Toaneni 'out' kwa uhai wa uhusiano wenu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Maisha ya mahusiano ni matamu sana, kama utapata mtu sahihi. Na utamu wake, muwe mnasikilizana; na sio kumfanya mtoto wa mwenzio kuwa mzazi wako, kwa kumbebesha majukumu ambayo hata wazazi wako waliyashindwa.

Kutoka toka 'out' kunanogesha sana uhusiano; hasa ile 'out' ya kulala huko muendako. Hotel, lodge n.k hizi zote zimejengwa kwa ajili yetu; na ukizitumia vizuri zinaboresha mahusiano mliyo nayo.

Si lazima, mpaka muwe mmefunga ndoa ndio mtoane 'out'; Itategemea na aina ya uhusiano mlio nao. kwa sababu, mahusiano ya kiutu uzima yapo ya aina nyingi; yapo ya kupeana kampani tu, yapo ya kuja kuoana baadaye, na pia yapo ya mume na mke.

Kwa hiyo jitahidini sana, kutoana 'out' hasa za mbali, iwe za kuvuka mikoa, wilaya, nchi n.k; kufanya hivyo kunanogesha uhusiano wenu; pia unakuwa umeipumzisha akili vizuri, na pia kuongeza uwezo mkubwa wa kufikiri namna ya kujiongezea kipato.

Utakuta katika mahusiano mnakuwa na mahasira hasira ya ajabu ajabu, yasiyokuwa na tija, muda wote mnanuniana, mara mwingine analalamika apelekewi moto, mara mwingine apikiwi n.k; hii inatokana na kutokutoana 'out'.

Toaneni 'out', kwa uhai wa mahusiano yenu.
 
Tuwatoe out hawa tulioowaoa tumesahau nini?


Halafu mpango wa kando watoto wabichi chuchu saa nne asubuhi awatoe nani?????

Hao wacha wajitoe wenyewe....


NB

Wananchi msinipopoe
 
Unaipangilia vizuri, angalau kwa mwezi mara moja

Kaka mimi nakubaliana na wewe kwenye hoja yako.
Mimi nachosema ili hoja yako itekelezwe basi lazima hela iwepo.
Umesema kuipangilia walau mara moja kwa mwezi,
Vipi hapo itageuka na kuwa siyo hela tena au!
 
Mahusiano kuwa hai lazima uwe na hela.
Bila hela mahusiano yanakuwa yanapumulia mipira.

Out hautoki na pumbu zako tu, lazima utoke na hela.
Ukiwa bahili sana mkuu, utashangaa bomu la nyuklia linakudondokea na kuziacha hizo salio
 
Mahusiano kuwa hai lazima uwe na hela.
Bila hela mahusiano yanakuwa yanapumulia mipira.

Out hautoki na pumbu zako tu, lazima utoke na hela.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]!Hatare sana
 
Back
Top Bottom