kelvin patrick
Member
- Feb 20, 2017
- 62
- 72
Naombeni maelekezo ya kina juu ya torque, lakini pia juu ya Power,namna zinavofanya kazi katika gari,kipi kinamtegemea mwenzie zaidi na vinamaana gani katika kuelezea uwezo wa injini katika gari husika?
Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
Hii ni figure ya piki piki kati ya cc 125 to 150Kweli hakuna mwenye lugha rahisi ya kuelezea hizi mambo
Max. Power 8.0 kW/8,250 rpm Max. Torque 10.4 Nm/6,500 rpm
Je nikilinganisha na hii nasema ipi ina nguvu
Bora wangeniwekea namba zote ziwe kubwa au ndogo zote ningebabia sasa wamenikomesha hapa wanaweka kadogo kule wanaweka kubwa wanapishanisha😥. Nikifanikiwa majibu ntakuja kumjibu mleta mada na kujijibu hapa ila mtaalamu angeturahisishia fasta basi
- Max Power: 8.8 kW (8000r/min)
- Max Torque: 11.6 Nm (6000r/min)
Mhhh hhh mhh.. Aisee hatari..!maelezo yako sio ya Uhakika kama jina lako..!Jibu la Behaviourist
Jibu ni rahisi sana.Horsepower ni kwa ajili ya speed wakati torque ni kwa ajili ya nguvu.
Assume kuwa wewe unapanda mlima mrefu ukiwa umebeba mzigo mkubwa begani.Hapa maana yake unahitaji nguvu nyingi.Ili uweze kumaliza kupanda mlima wako salama inabidi utembee taratibu sana(low rpm).Kwa hiyo unakuwa na nguvu nzuri ya kuupanda mlima kama utatembea taratibu(low rpm).Kama utakosea ukapanda mlima wako kwa haraka au ukiwa unakimbia(high rpm) lazima utaishiwa nguvu(torgue) haraka sana na hutafanikiwa kumaliza kupanda huo mlima.Lakini ili umalize kupanda mlima wako lazima utahitaji kutembea kutoka speed ya zero kwenda speed fulani na hapa ndipo unaona kuwa torque inaongezeka kadri rpm inavyoongezeka hapo mwanzo.
Hii maana yake ni kwamba unakuwa na nguvu nyingi(high torque) kama utapanda mlima wako taratibu(low rpm).Torque na horsepower ni ndugu ambao hawapatani.Ili uweze kukimbia bila shida(high horsepower) inabidi usiwe na mzigo mkubwa na ili uweze kubeba mzigo mkubwa(high torque) inabidi usikimbie.
The higher the rpm the high the speed(horsepower) while the low the rpm the high the torque.Kwenye graph yako hapo unaweza kuona kuwa torque inaongezeka tu hapo mwanzoni jinsi rpm inavyoongezeka lakini inapungua kadri rpm inavyozidi kuwa kubwa wakati horsepower inaongezeka kadri rpm inavyoongezeka.
Hahahahaaah sio jibu langu bro, ni jibu la behaviourist nimemkopy sehemu.Mhhh hhh mhh.. Aisee hatari..!maelezo yako sio ya Uhakika kama jina lako..!
Umeshawahi kuiona 1vd-ftv au 1hd-fte inakosa spidi kwenye mlima sababu ya mzigo..!!?
Torque na Horsepower sio kuwa hawapatani.. Ni ndugu wa karibu sana na wanashirikiana sana tuu..!huwezi kupata Horsepower bila Torque..!
Torque ni nguvu yenyewe ya gari..
Horsepower ni spidi ya gari kutumia hiyo nguvu kufanya kazi..!
Rpms zikiongezeka sio kwamba Torque inapungua au Horsepower inaongezeka..!
Kila engine ina horsepower na Torque curves.. Kwahiyo kupanda au kushuka kunategemea na curve.. Hata Horsepower inashuka rpms zikipanda zaidi ya peak..!
Diesel engines Horsepower na Torque figures zake zinapishana sana.. Petrol engines figures zinakaribiana..!
Maana yake ukitaka gari ya kufanya kazi ngumu na kubwa chukua diesel..!
Sawa kabisa ndivyo ilivyo tupatie maelezoHii ni figure ya piki piki kati ya cc 125 to 150
Diesel hiyo..😀😀 naomba kujua tofauti pia , huwa naona kwenye games wakati wa kununua magari