Tofauti kati ya uzuri na urembo na mvuto

Tofauti kati ya uzuri na urembo na mvuto

my-eyes

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2015
Posts
551
Reaction score
133
Amani iwe nanyi wakuu., nimekutana sana na maongezi hayo .mfano wapo wanaosema inawezekana mtu kuwa ni mzuri lakini akawa hana mvuto., pia kuna warembo ila si wazuri na wapo wazuri kisha warembo halafu wana mvuto.! Hili limenitanza naomba kujuzwa na wajuzi wa hili au niseme ni upi mtizamo wako kwa hili.karibuni.....
 
Kwa mtazamo wangu hayo ni maneno tofauti japo hapo kwenye mvuto nadhani ndo huwa inatajwa kuwa ni haiba.

Ni wasichana/wanawake wachache waliojaliwa kuwa na vitu vyote hivyo vitatu.

Mmoja wapo aliyejaliwa kuwa na vitu vyote hivyo vitatu ni Wema Sepetu.
 
Nakubaliana na mdau hapo juu, hata hivyo niongezee kidogo kwa uelewa wangu.

Uzuri- muonekano wa mtu ambao hautegemei hali ya maisha au hadhi fulani ya maisha. Nadhani ushawahi sikia watu wakisema "Yule binti ni.mzuri sana sema tu kakosa matunzo". Uzuri kila mtu anao kwakuwa hakuna aloumbwambaya. Ila tu kivumishi "Sana" kinaweza tumika kuonesha tu kiwango cha uzuri.

Urembo- Muonekano wa binti ambao unategemea zaidi hadhi ya mtu. Hapa kiwango cha pesa na umaarufu wa mtu vinahusika. Hapa ni swala la pesa kuogezea kwenye uzuri. Inahusisha matumizi ya vipodozi, vyakula, mazoezi ya kuweka shape vizuri nk. Hapa hakutegemii uasili wa mtu bali kipato cha mtu. Kuna watu(mabinti) ambao ni warembo lakini sio wazuri.

Mvuto- hii tofauti na hizo hapo juu hutegemea zaidi watu wengine na sio muhusika. Ni namna watu wanavyoutazama uzuri na urembo wa mtu. Hata hivyo mvuto unakwenda mbali zaidi kwakuwa unahusisha vile jamii inotizama vitu kama akili,uelewa utendaji kazi wa mtu nk. Kuna watu wanamvuto wa kuwasikiliza tu yani hutamani wamalize kuongea hata kama hivo viwili hapo juu vimepungua. Mfano kwa mtizamo wangu Obama anamvuto zaidi kuliko maraisi wengi hasa katika swala la kuongea.
 
Nakubaliana na mdau hapo juu, hata hivyo niongezee kidogo kwa uelewa wangu.

Uzuri- muonekano wa mtu ambao hautegemei hali ya maisha au hadhi fulani ya maisha. Nadhani ushawahi sikia watu wakisema "Yule binti ni.mzuri sana sema tu kakosa matunzo". Uzuri kila mtu anao kwakuwa hakuna aloumbwambaya. Ila tu kivumishi "Sana" kinaweza tumika kuonesha tu kiwango cha uzuri.

Urembo- Muonekano wa binti ambao unategemea zaidi hadhi ya mtu. Hapa kiwango cha pesa na umaarufu wa mtu vinahusika. Hapa ni swala la pesa kuogezea kwenye uzuri. Inahusisha matumizi ya vipodozi, vyakula, mazoezi ya kuweka shape vizuri nk. Hapa hakutegemii uasili wa mtu bali kipato cha mtu. Kuna watu(mabinti) ambao ni warembo lakini sio wazuri.

Mvuto- hii tofauti na hizo hapo juu hutegemea zaidi watu wengine na sio muhusika. Ni namna watu wanavyoutazama uzuri na urembo wa mtu. Hata hivyo mvuto unakwenda mbali zaidi kwakuwa unahusisha vile jamii inotizama vitu kama akili,uelewa utendaji kazi wa mtu nk. Kuna watu wanamvuto wa kuwasikiliza tu yani hutamani wamalize kuongea hata kama hivo viwili hapo juu vimepungua. Mfano kwa mtizamo wangu Obama anamvuto zaidi kuliko maraisi wengi hasa katika swala la kuongea.
Sina zaidi
 
Back
Top Bottom