Tofauti ya kufuga mbwa kama mlinzi au kama rafiki ni gharama za matunzo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mbwa akiwa mlinzi kuna wanaokumbuka kumjengea kennel lakini mbwa wengine wanalala barazani au chini ya mti kwenye kivuli. Mvua ikinyesha anaachwa apambane na hali yake. Kuna wanaokumbuka kununua mifupa butcher au dagaa na kumpikia mbwa chakula. Wengine wanaachwa tu wajiokotezee, unamkuta mbwa jalalani anagombania ukoko wa ugali na kuku.

Mbwa rafiki hukaa ndani na rafiki yake, anaogeshwa mara moja kwa wiki, ana shampoo, taulo, ana chanjo za magonjwa na huonwa na vet kila baada ya miezi sita kwa check up. Mbwa huyu chakula chake ni cha makopo na kila rafiki yake akinunua chakula huangalia stock ya mbwa. Mbwa huyu anakaa kwenye makochi wanaangalia movie na rafiki zake. Mvua ikinyesha kukiwa na baridi hujisogeza kitandani na rafiki yake wakajifunika blanket.

Ukitokea na mlipuko wa kichaa cha mbwa unafikiri ni mbwa yupi atapata chanjo kati ya hawa mbwa wawili?
 
Mh! Ili fumbo, ila labda wa ndani acha yule wa jalalani.
 
Huyu wa ndani kwasababu rafiki yake anamuona ana thamani sana, anaweza kukopa pesa ili mbwa apate chanjo. Hatataka kumpoteza.
Ofcourse Huu mtego nilishauona,as kuna kitu unarelate if I’m not mistaken🤣🤣
 
Mke wangu mara nyingi akikasirika huniita "mbwa wee". Sasa akinuita Tena hivyo, kudadadeki atanikuta majalalani kwenye kugombania ukoko na rafiki zangu KUKU WA KIENYEJI
 
Mi nitakuja kuanza kufuga mbwa nawaokota wale wa mtaani nawafuga. Mbwa na kitten.

Jana jogging nilikutana na kitten jaman dah. Kadogo sidhani kama kana mwezi 1. I wish ningekachukua ila ndio ivo ghetto katakula nini, mikate na chips?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…