Uchaguzi 2020 Tofauti ya mikutano ya CCM na CHADEMA ni kuwa CCM inahudhuriwa na wanachama wengi wakiwa wamevaa nguo za CCM, CHADEMA hakuna

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Ukitaka kujua watu wana mapenzi gani na timu iwe Simba au yanga angalia uwingi wa uvaaji nguo za timu kwenye uwanja.

Tofauti ya mikutano ya CCM na CHADEMA ni kuwa CCM inahudhuriwa na wanachama wengi wakiwa wamevaa nguo za CCM, CHADEMA wanaohudhuria ni wasiojulikana ni chama gani.

Huoni zile tshirt za CHADEMA ushahidi kuwa wanaohudhuria ni wapita njia waliokuja tu kumshangaa Lissu.

Kwa mtizamo ukitizama picha zote za mikutano ya CHADEMA wavaa Tshirt za CHADEMA ni wa kumulika na tochi ni kama hawapo kabisa.

CCM mikutano yake unaona wazi kuwa waliofurika wengi ni wafia chama sio wapita njia.
 
Kwani si mnatumia kodi zetu, kununua mitishet na kuigawa bure??

Yaani kama ni mapenzi, Mapenzi walonayo wananchi kwa CHADEMA ndio Halisi.

Hamna cha hongo ya aina yoyote lakini nyomi lake sasa [emoji23][emoji23]
 
Utumbo mtupu
 
Tofauti zingine
1. CCM huwabebe maelfu kwa mamia kwa kutumia mabasi, bunda, ngamia, treni nk
2. CCM huwapa kwa upendo kabisa wahudhuriaji kuanzia 5,000/- na kuendelea.
3. CCM ndo chama kinachotumia Wanafunzi vzuri maana hakika wanavijaza viwanja,
4. CCM ndo chama pekee ambacho kila kinapoenda, shule , vyuo,vyote hufungwa . na kulazimishwa kuhudhuria.

NB: kinyume chake ni CHADEMA.
 
Wachawi nao wanaenda kanisani na misikitini
 
Hawa wa kusombelewa na malori..!?
 
Tuwaonee huruma chadema walikosea mgombea watanzania wanajua ni kuwadi wa mabeberu
Wanajifariji na uchache ule wa watu wanaona ndo ushindi,
Je wangepata wale watu wa Lowasa nadhani wangetangaza ushindi kaa ya kura.
 
Huwezi kujaza watu wa chama chako kwenye kampeni.

Kampeni inahitaji watu baki ili wasikilize sera zenu.

Hivyo Chadema inasikilizwa zaidi.
Sahihi kabisa ndugu...Tatizo sasa ukifika kwenye mkutano wa CCM,ukiwa umevaa T-shirt yenye nembo ya Chadema,utaacha utumbo pale.Sijui huwa ni nini hii.
 
Kwa hiyo hizo sare ndiyo zinazopiga kura!! By the way, hivi ilikuwaje Mgombea wenu siku ile alikubali kupigishwa magoti na Sholo Mwamba eti kwa kisingizio cha kumuombea marehemu?

Ninachofahamu mara nyingi tunasima walau kwa dakika moja tu hivi kumkumbika/kuwakumbuka marehemu!
Au alikuwa anatuomba msamaha kijanja? Maana nina imani kabisa kama kuna Jehanamu, basi mgombea siku ya hukumu atakua viti vya mbele mbele kule.
 
umenishitua ulipo sema ccm wamevaa nguo chadema hamna nikahisi labda umeona kwa jicho la tatu kama wako uchi.
 
Hawa ndio wahudhuriaji,kweli awamu ya 5 ni kichwa cha mwendawazimu
 
ni kwa vile mikutano ya CCM ina sura ya bonanza (wamo wapiga kura wa Lissu na wa Magufuli).

so CCM ina bajeti ya:

kununulia nguo wahudhuriaji wa mikutano yake
kuwasomba watu kuja kuhudhuria kwenye mikutano
kualika wasanii kwenye mikutano kwa malipo

Chadema haina bajeti hiyo - watu wanajileta wenyewe kwenye mikutano na nguo zao wenyewe, kwa usafiri wao wenyewe na bila ya kivutio chochote cha wasanii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…