Tofauti ya mishahara ya walimu Tanzania na Kenya

Lita moja ya maziwa ni around 100ksh, 2000 tsh
kilo moja ya sembe ni around 1500tsh
 
Mishahara minono kukarabati reli hadi mkopeshwe...priority zenu ni tumbo
Wacha serikali ijisort sekta ya reli. Mwananchi anafaa kulipwa vizuri pia yeye aweze kuenjoy maisha
 
acheni utani hawa hawa wakenya wangekuwa wanalipwa hiyo mishahara wasingehangaika kufurika Tz kila kukicha kutafuta ajira ...ninao jamaa zangu wakenya wanalipwa laki mbili na nusu tu na hawataki kurudi kwao kila uchao wanakimbizana na migration

Mkenya aje kulipwa madafu yenu laki mbili na nusu, hela ambayo tunalipa akina dada wa kutufulia nguo ambao wengi wametokea Tanzania.
Hao wafukuzeni sio Wakenya.
 
Mkenya aje kulipwa madafu yenu laki mbili na nusu, hela ambayo tunalipa akina dada wa kutufulia nguo ambao wengi wametokea Tanzania.
Hao wafukuzeni sio Wakenya.
we ni mpuuzi unadhani ninachoongea ni uongo ?!!! usitake kukataa ndg zako kwa sifa za kipuuzi asee !!!
 

Kaka, Kenya tungekua vilaza kwa nchi yetu ilivyo ndogo na kame aisei tungekua kwenye uchumi sawa na Rwanda. Halafu huwa tunajivunia nguvu kazi yetu iliyoelimika na ya kujituma, hatuna madini, ardhi yenyewe ndogo na kame, lakini tunaongoza ukanda wote huu kiuchumi, takwimu za hivi majuzi zinaonyesha pengo bana yetu na majirani limeongezeka pakubwa, Tanzania (ambayo tayari ni muungano wa nchi mbili) halafu uunganishe na Uganda ndio ukaribie uchumi wetu.

Siri yetu ni kujituma, hamna kingine, Mkenya popote alipo huwa anaweka utani pembeni likija suala la kujituma na ndio maana serikali yenu huzuia sana kuwapa Wakenya vibali maana wakija wataishia kuwafunika nyie, wamiliki wa makampuni ya Tanzania hujaribu sana kuwaajiri Wakenya lakini inashindikana kwenye vibali, wizara ya ajira na taasisi ya uhamiaji huwa wanakatalia mbali kabisa kwa vigezo kwamba kuna Watanzania wenye uwezo wa nafasi anayokuja kuajiriwa Mkenya, unakuta waajiri kwenu huko wanahangaika na mafaili kule uhamiaji wakijaribu kubembeleza.
 
Afadhali umebadili mada kwenye uduni wa wahitimu wa Tanzania hadi kwenye kujituma kwa wakenya.

Kwenye kujituma siongei neno.

Lakukuambia tu Kenya sio Kame ni moja ya nchi zenye aridhi nzuri saana..Ukame angeulaĺamikia Namibia na jirani zake sawa...

Maisha ya Tanzania na Kenya sijawahi kuona kama yanatofauti...Labda naona hazina tofauti kwasababu sijawahi kuona unafuu wa maisha ya binadamu wa kawaida baina ya nchi hizi mbili.
 
Pengo linapanuka, hamna uwezo ku fund hata mradi wa 40bln mpaka mkope,tumia akili bana.

Ona mwenzenu leo nayeye kaleta ulinganyifu wa mishahara ya waalimu,ameshasahau gharama za maisha kenya ni msumari.
 
Lazima mjue kubalance,lakini wazo lako ni zuri
In my opinion, ulilipa civil servants vizuri itaaffect economy positively. Ataweza kupromote mama mboga, hotel ndogo ndogo, salon, vinyozi, house maid etc na even the poorest of the poor watapata hizi pesa indirectly.
 

Tuletee other government jobs, Nice post. Gharama za maisha tz na ke ni almost the same at least kwa Nai na Dar ipo hivyo hasa kwa middle class. Bado sijajua though watu gani wana unafuu wa maisha, Maana Kenya pia wana challenge kubwa ya ardhi kujenga nyumba ni ndoto ambayo wakenya wengi hushindwa timiza tofauti na tz.
 
Sawa ntafanya research nipost
 

Wala sijabadili mada, mwisho wa siku elimu ni kujituma, ukiwa wa kujituma utakua bora kwenye idara zote, kaangalie kitaalam utaona Kenya inaizidi Tanzania kwa Global Human Capital Index kwenye country ranking ambayo hupima nguvu kazi ya raia kwenye
- Capacity
- Deployment
- Development
- Know-how

Fuata kwenye hii tovuti ya Benki Kuu https://www.worldbank.org/en/data/interactive/2018/10/18/human-capital-index-and-components-2018
 
Kujituma ni muhimu sana arif,
Nilikua nasoma hadi usiku mnene shule wanakusema unasomea kijiji ,nikatoboa
Baada ya kumaliza chuo serikali ikaniajiri sahivi nafurahia maisha na kazi kila nachopanga kinakua japo kuna muda kinachelewa...
Bidii ndio kila kitu,Mimi siwez kuimba, siwezi kazi ngumu nashindwaje kukaza shule?hii Ni kwa yoyote Yule anaejielewa
Lazima ujue unaweza wapi ukomae napo hadi kieleweke...
Wengi hubaki masikini kwa kujiendekeza na ujinga,uvivu na kupoteza muda kwenye mambo yasio na tija,Hakuna faida yoyote ya kua mkenya Au mtz usiezalisha chochote!!watu wabadilike
 
Wakenya wanafurika tz kutafuta ajira na biashara. Watanzania wanafurika Kenya kuomba omba..."maskini saidia" huku wamenyoosha vibakuli.
 
Nchi zote poor food is cheap,
Enda Uganda,burundi,congo,somalia ETC
 
Beautiful comment. Kenya hata usomee juu ya mparachichi utakaa miaka na mikaka bila kupata kazi. Inaonekana huko kwenu mnapata kazi punde tu mnapohitimu chuo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…