Toka Azam TV ianze kuonesha ligi ya Tanzania, imepelekea kupunguza mashabiki wa ligi za Ulaya

0ozg Tz

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2016
Posts
4,155
Reaction score
11,168
Kwa jinsi hali ilivyo sasa ya kimpira hapa kwetu, hasa katika mazingira ya vibanda umiza, kwa kuangalia mashabiki wa hizi timu mbili kubwa hapa Bongo.

SIMBA
Kwa msimu huu wa 2021/22 hasa siku za hivi karibuni, mashabiki wa Simba wameanza kupungua kuhudhuria mechi za Simba, hasa hasa inapokuwa inacheza michezo ya Ligi Kuu na hata kutoa kiingilio wanakuwa wagumu.

Majibu yao ni kuwa "leo sina" au anatoa hela pungufu, wakati misimu mingine iliyopita mashabiki wa simba walikuwa wanafurika kwenye vibanda kwa idadi kubwa sana. kwa kila mechi haijalishi ni za kimataifa au za hapa nyumbani na walikuwa hawana usumbufu wa kutoa kiingilio.

YANGA
Kwa msimu huu wa 2021/22 mashabiki wa yanga wamekuwa wakitoa pesa ya kiingilio bila kuwa na usumbufu wowote.

Yanga ina mashabiki wavumilivu sana hata misimu ambayo walikuwa hawafanyi vizuri bado waliendelea kuhudhuria kwa wingi sana, ila kwa misimu ambayo Yanga walikuwa wanafanya vibaya mashabiki wake walikuwa wasumbufu kutoa kiingilio ingawaje walikuwa wanahudhuria wengi sana kwa kila mechi ambayo Yanga inacheza.

MASHABIKI WA JINSI YA "KE"
Takwimu zinaonesha Yanga wana mashabiki wengi zaidi ya mashabiki wa Simba,yaani mashabiki wa Yanga wa jinsi ya ke wapo 70% na simba 30% ya wanawake wote TZ.

LIGI ZA ULAYA
Toka Azam TV ianze kuonesha Ligi ya tz,imepelekea kupunguza mashabiki wa ligi za Ulaya.

Hii inapelekea kutumia faida tuliyoipata kwa kuonesha ligi ya TZ kulipia ving'amuzi vinavyoonesha ligi za ulaya,tunafanya hivi kutokana na kuwa sisi wamiliki ni wapenzi wa ligi hizi za ulaya lakini isingekuwa hivyo tusingekuwa tunalipia ving'amuzi vya Ulaya.

Niliwahi kuhisi labda zile bechi ambazo haziruhusu watu kuegema ndo zinasababisha watu wasipende kuangalia mechi za Ulaya maana wanakuwa wameshachoka baada ya mechi ya simba au yanga kuisha.

Niliamua kutafuta viti vya kuegama lakini bado watu walikuwa hawakai baada ya mechi ya simba na yanga kuisha.
 
Huu ndio ukweli, Ila usishangae Makolo watakuja kukupinga. Kama uongo check reply ya 2 hapo chini baada ya hii yangu😁😁
 
Ni kweli. Vipi takwimu kwa mechi za CAF.

Halafu kwenye wanawake sidhani hiyo ratio kama ni sahihi. Mashabiki wengi Wa kike wa Simba wamepatika kwenye hii misimu minne hasta wale ambao kabla walikuwa neutral . Hii pia imechagizwa na Azam. Baraka Mpenja ni maarufu kwao kuliko Gharib Mzinga mzee wa takwimu.

Yanga wako kwenye eda ya kukosea ubingwa kwa miaka 4 mfululizo. Sasa mzuka walionao kwa sasa vibandani si mchezo.
 
Kwa mechi za CAF hapo hawalembi wanahudhuria wengi sana na Yanga nao kwenye mechi hzo wanakuwepo wengi sana
 
Kubeti kumepunguza kwa kiasi kikubwa cha mahaba kwenye mpira halisi
 
Siku ya big match huwa sibet ili niinjoy kuchek game,maana mikeka inakufanya ushabikie hata litimu ambalo huwa hulipendi
Hapo sasa kama hawa mashabiki wa Arsenal wanabetia kuipa timu yao inachowafanyia wao wenyew wanachoka
Wakipatikana mashabiki wengi wa hivi anaachana na mahaba
 
Sijui niseme kweli au la, lakini nimepunguza sana kutazama game za ulaya eg Epl lakini pia hapa bongo pia naangalia game za Simba na Yanga tu.
 
Takwimu kuhusu ushabiki wa wanawake wewe ni mwongo,, anyway labda Kwenye banda umiza lako ndo umetolea hizo takwimu japo hujaonyesha source ya takwimu zako....
 
Kabisa
 
Ni bora Simba kuna mashabiki female wachache lakini wote pisi kali kuliko Utopolo kuwa na mashabiki weengi wa kike alafu sura za baba zao.
unamkuta mdada shabiki wa Yanga ana sura kama herufi za kichina,mmanina.
 
simba na yanga zipo Dar es salaam
mashabiki wa soka na wanaohudhuria vibanda umiza huko Daslam ni wanasimba na yanga hivyo mpira wa hizo timu mbili kwa Dar ndio kipaumbele

ukienda mikoani soka la ulaya hususani epl ndio habari yao, hizo takwimu za wanaume wa dar sio Tanzania nzima
 
Ni bora Simba kuna mashabiki female wachache lakini wote pisi kali kuliko Utopolo kuwa na mashabiki weengi wa kike alafu sura za baba zao.
unamkuta mdada shabiki wa Yanga ana sura kama herufi za kichina,mmanina.
Akili za kimalaya,hebu tuwekee picha ya dada zako kama wana sifa hizo!
 
Naweza kuwa shabiki wa Simba kindakindaki lkn kwenye mechi ya chelsea na simba. Samahani sana Simba itanisamehe... burudani ya pira la ulaya lina raha yake wew
Bora wee unaongea ukweli
 
Mimi na Litimu langu la Man U lilivyo Ndio baasi kabisa
Kwa Simba Sibanduki hata Icheze saa 8 usiku
ila Man U akicheza Wala Sina Hata wazo
Timu lenu ferguson hataki kocha mwengine awe na mafanikio hapo
 
Ni bora Simba kuna mashabiki female wachache lakini wote pisi kali kuliko Utopolo kuwa na mashabiki weengi wa kike alafu sura za baba zao.
unamkuta mdada shabiki wa Yanga ana sura kama herufi za kichina,mmanina.
Unajua sana kuchamba ila angalia usije vishwa khanga kama mudy
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…