Samedi Amba
JF-Expert Member
- Nov 13, 2018
- 227
- 178
Habari za muda wadau na wanajamvi,
Tony Elumelu ni mwana wa afrika, mjasiriamali, mpambanaji na mkarimu pia. Alianzisha foundation ya Tony Elumelu, mnamo mwaka 2010. Nia ilikuwa ni
Mnamo mwaka 2015, mlango ulifunguliwa kwa ajili ya kuwafadhili wajasiriamali barani Afrika, kupitia kampuni ya Tony yenye jina "Heirs Holdings". Aliunda programu maalum yenye jina "The Tony Elumelu Foundation (TEF)". Aliwekeza dau la $100,000,000 (dola milioni mia moja za kimarekani) kwa ajili ya kuwafadhili wajasiriamali 10,000 ndani ya muda wa miaka kumi.
TEF imewezeshwa na kutiwa shime na mashirika kama vile United Nations Development Program (UNDP), the African Development Bank na United Bank of Afrika.
Kila mwaka (tangu 2015), kila mshindi hupewa $5000 (dola elfu tano za kimarekani, au milioni Kumi za kitanzania), kwa ajili ya kuanza au kukuza biashara.
Ikumbukwe kuwa sio lazima uwe na biashara inayotembea tayari. Hata idea tu inatosha. Wakiipenda, dau unalo.
Nilifanikiwa kuongea na wajisiriamali wachache wa kitanzania ambao wamepokea hizo pesa tangu 2018 (sijapata wa 2017 kwenda nyuma), na wana shuhuda nzuri.
Kwa ufupi, ni hivi:
Milango imefunguliwa kwa wajasiriamali wote ambao wanaamini wana idea itakayoifanya bara la Afrika kupiga hatua nyingine mbele. Tarehe ya mwisho ya kujiandikisha ni Jumapili, Januari 31, 2021.
Kwa habari zaidi, tembelea
Tony Elumelu ni mwana wa afrika, mjasiriamali, mpambanaji na mkarimu pia. Alianzisha foundation ya Tony Elumelu, mnamo mwaka 2010. Nia ilikuwa ni
kuwawezesha wanaume na wanawake katika bara letu (la Afrika), kutia chachu ukuaji wa kiuchumi, kuondoa umaskini na kutengeneza fursa za ajira. Tunaamini kuwa sekta binafsi ina sehemu nyeti katika kuzalisha mali na rasilmali watu.
Mnamo mwaka 2015, mlango ulifunguliwa kwa ajili ya kuwafadhili wajasiriamali barani Afrika, kupitia kampuni ya Tony yenye jina "Heirs Holdings". Aliunda programu maalum yenye jina "The Tony Elumelu Foundation (TEF)". Aliwekeza dau la $100,000,000 (dola milioni mia moja za kimarekani) kwa ajili ya kuwafadhili wajasiriamali 10,000 ndani ya muda wa miaka kumi.
TEF imewezeshwa na kutiwa shime na mashirika kama vile United Nations Development Program (UNDP), the African Development Bank na United Bank of Afrika.
Kila mwaka (tangu 2015), kila mshindi hupewa $5000 (dola elfu tano za kimarekani, au milioni Kumi za kitanzania), kwa ajili ya kuanza au kukuza biashara.
Ikumbukwe kuwa sio lazima uwe na biashara inayotembea tayari. Hata idea tu inatosha. Wakiipenda, dau unalo.
Nilifanikiwa kuongea na wajisiriamali wachache wa kitanzania ambao wamepokea hizo pesa tangu 2018 (sijapata wa 2017 kwenda nyuma), na wana shuhuda nzuri.
Kwa ufupi, ni hivi:
- Wewe una idea yako, ambayo ikiwezeshwa itazalisha mali. Au una biashara ambayo haina zaidi ya miaka 3 tangu kusajiliwa.
- Wewe ni mtanzania (automatically mwafrika)
- Unaweza kujielezea vizuri, na kuwashawishi hawa wafadhili kwamba ukipewa pesa, utafanyia kitu
- Idea au biashara yako iwe na uwezo wa kuscale (yaani kukua kwa mapana na marefu, ikipewa muda na "mbolea"). Kumbuka kuwa milioni 10 sio hela ndogo. Kwa hiyo, lazima uwe na kitu ambacho kina uwezo wa kukua.
Milango imefunguliwa kwa wajasiriamali wote ambao wanaamini wana idea itakayoifanya bara la Afrika kupiga hatua nyingine mbele. Tarehe ya mwisho ya kujiandikisha ni Jumapili, Januari 31, 2021.
Kwa habari zaidi, tembelea