Top Ten footballers Tanzania ever produced

Naomba ujibu maswali yote fully. The most important is question number 1 in Red......do not dilly dally mate!! This is not politics, jibu swali kama lilivyoulizwa.

- Naona kila mahali unaweka hili neno hapa sio politics, hapo ninashindwa kukuelewa maana yako mkuu labda ufafanue kidogo! Mimi nipo hapa kujadili mpira, sasa hili la siasa linatokea wapi?

SIMPLE QUESTIONS:
1) How many games did the so greatest team of Tanzania play to qualify for the 1980 African Nations Cup?

- Kulikuwa na Raundi ya kwanza na ya pili, and then Robo finali, kisha nusu finali and then unakwenda kwenye final, Tanzania tumeliweza hili mwaka 1980 yaani tulienda final za African Cup kwa National teams, na since then hatujaweza tena, sasa labda mkuu utupe darasa why?
No one rembers losers, no one remembers third places........FOR A LONG TIME YOU OLDIES HAVE ALWAYS FILLED US WITH YOUR FANTASY...AMAZING 60s AND 70s FOOTBALL.........A CLOSE SCRUTINY PROVES

- But atleast everybody remembers who went to the final, I mean wote tunajua kuwa Tanzania iliwahi kufika finals za African Cup, mwaka 1980 na kila mwananchi anakumbuka kwamba since then hatujawahi kwenda popote.

- Yes kila mtu anakumbuka sana jinsi Dilunga na Mahadhi, walivyochaguliwa kuwakilisha Tanzania, kwenye all African Team, lakini since then hakuna anayekumbuka kuchaguliwa kwa mchezaji yoyote tena kutoka Tanzania! This are just facts huwezi kuzibadili wala kuongezea anything zinasimama kama zilivyo

- It has nothing to do na oldies or age, ila everything to do na the love of the game na knowing the history of anything you are interested in, I love soccer na michezo mingine yote, looking at the history vijana wa sasa wamefanikiwa sana kuliko wa zamani, kwenye Muziki na Ngumi tu, lakini wameshindwa vibaya sana kwenye soccer na Riadha.

Respect.


FMEs!
 
Swali limeulizwa top ten footballers ever wa bongoland?

Sasa hii miandering kazi kweli kweli. Anyway

Miaka ya 1970's rais wa Tanzania alialikwa kwenda kutazama mpira, wapambe wakamdhihirishia kwamba ngoma itakuwa mswano. Basi akaondoka na ving'ora vyake hadi uwanjani. Mechi ikaanza, sasa wale jamaa walipokuwa wanacheza mpira baada ya kuona rais wa nchi yupo pale badala ya kusakata kabumbu wakaanza kutwangana makonde. Ilikuwa ni aibu sana basi tangu siku ile rais alikataa kuhudhuria soka kwani aliona wengi wanaocheza huo mchezo nidhamu yao si ya kimichezo bali ya kuoneshana ubabe.

Miaka imepita lakini ukweli utabaki pale pale Tanzania tumeshindwa kuendeleza vipaji sio kwenye mpira tu hata kwenye riadha nk. Mtakumbuka miaka ile tulikuwa hata medali tunapata kwenye riadha nk. Siku hizi hazionekani kulikoni mafisadi wametuzidi ujanja.

Kumbukeni hata NHC waliweza kujenga nyumba za vyumba sita sita miaka hiyo kwa wananchi wa kawaida lakini leo hii wanajenga za kuuza kwa matajiri. Kazi tunayo.
 


NOPE - Swali langu nimekuuliza, na nilishalijibu ila umekwepa kwepa. How many games did Taifa Stars play to QUALIFY for the Finals....to "QUALIFY"........it cant be clearer than that...yaani before reaching Nigeria.

There was only about 22 teams playing in the African qualifications...and you only had to play 1 or 2 games to qualify for the Finals (ie kati ya timu 22 unabaki na timu 8 tu). I.e IT WAS EASIER TO QUALIFY BACK THEN...........YET, WE ONLY QUALIFIED ONCE!!

Ninaposema politics, ni jinsi unavyokwepa kujibu swali lilivyoulizwa.

Again you are wrong, there was NO QUARTER FINALS until after 1992. If there was, who did Tanzania Play IN THE QUARTER FINALS in 1980??

There were only 2 groups of 4 each at the finals in Nigeria. numbers 1 and 2 of each group went straight to the semifinals.

DO YOU SEE HOW EASY IT WAS??

Now taking all that into account, having only 8 teams in the finals, chances are each team can produce at least a player or two to make a squad of atleast 16 or more if to 21. Hence Dilunga etc. I cant knock him, i have said am sure he was good.

TOP list yako umewataja wachezaji wa 70s ndio wakali.......yet walioshinda makombe zaidi, be CECAFA etc ni wa 90s. Lakini hao hao wa 90s hawajafanikiwa Ulaya. having said that atleast China alicheza mechi 5 timu ya Walsall inaeleweka....kiasi.
 

Yes, true, swali ni kama ulivyouliza.
......we are measuring by what standards though? Kama by Tanzanian standards sawa. Sasa wanao measure by TZ standards ndio wanaanza ku-split pre 80s na 90s onwards.....
Mkuu, ishu mimi ninayoshindwa kuelewa, ni hawa watu wanaobebea bango timu ya 1980. Ila uki-scrutinise qualification system ya kipindi hicho na ya 90s kuendelea ni tofauti kabisa....in terms of quantity of teams n quantity of matches.

So on top of all that, I really wonder why we accept MEDIOCRITY. Yaani mentality yetu Tanzania, majority tunaridhika na minimum performance. Watu kwenye Jukwaa La Siasa wanailima majembe CCM kwa wizi na underperformance.....yet we accept it elsewhere? I mean, c'mon. If we crap we crap, n we need to raise the bar, simple.
 
mie nimejitoa kijana anapenda ligi.....hapa ni sawa na kumpigia gitaa mbuzi.na ukibishana na mjinga............
Haya wasasa(bongo flava) wanacheza sana mpira but hakuna hata kakijikombe ..tumebaki kufungwa na Rwanda/burundi.
halafu mie sina muda wa kuandika kama wewe na highlight nyekundu ili iweje???watu tupo busy bana na mishemishe za kusaka dollars au na ulaya utakuwa umepelekwa na ANKAL???
 

Poa, we niite mjinga maana ndo matusi yako. umekuwa ukinikashifu tangu mwanzo....ila I guarantee you kwa lugha yako hiyo, nilipopita darasani we utasoma tu kwenye net.
Mimi paundi zinanitafuta.....what is kutafuta dollars? lol.
 


- Since 1980, Tanzania tumefika finali hizo mara ngapi mkuu?


FMEs!
 

- Since 1980, Tanzania tumefika finali hizo mara ngapi mkuu?


FMEs!

Only that year mkuu. Ngoja nikusaidie majibu mengine pia. 1 or 2 matches qualification maximum to go to Nigeria. 3 matches in the finals itself as first round..straight to semifinals without quarterfinals. Since we didnt qualify for 1982, 1984, 1986 etc...then the players in 1980 were one year wonders....n werent consistent to call them greats. So in theory you only needed to play 6or 7 cup finals to win the African Nations Cup.

In 2010, Angola, 16 teams are at the Finals. They came from 48 teams that played qualification, split into 12 groups of 4. Only winners of the group went through and best runners 8 of them, played against each other to get 4 teams etc etc......This has been ongoing since 92. So just in the qualification you are playing atleast 6 matches plus another 2. hapo hujafika tu fainali.

You just can not compare the 2.......and still its no excuse for us not to do well. So we were crap in the 70s, 80s and 90s and now.......when we win something then lets re-vist the discussion.

Mkuu, nacheza na wapopo mpira, na huwa wanashangaa Mtanzania anajua kucheza mpira, lakini hatuonekani. Yaani siwezi mimi nikaongea na Mpopo halafu nimwambie tulicheza nusu fainali 1980. Aibu aibu. Mimi huwa na sema tu, we are s.h.it. Nawaambia all the wahala u guys get after reaching the finals, we get it on a a daily basis.
 

Kona za Kajole zilizokuwa zinatinga nyavuni zenyewe bila kuguswa na mtu, we acha tu. Unawasikia nguli wetu wa utangazaji wakiitana Miki au Sekin.k. Sasa watu kama hawa wangepatiwa ukwasishaji (financing) kama wa vijana wa Masikio Makisio lazima fainali za kombe la dunia wangetinga tu enzi zao. Jamani "chalukwa chasakahala", mtanisamehe kwa wale ambao hamtaelewa maana ya chalukwa cha sakahala kwani nimelazimika kuandika kiluga kwani nimekumbuka ile National 277 Dudu Proof ya Mzee Lubuva ilivyokuwa inatupa uhondo.
 
Timu ya vijana'vijeba' ya 1981 iliyokwenda Norway kwenye GOODWILL CUP if am correct...AHMED AMASHA,ZAMOYONI MOGELLA,ALI MAULID MTAWA et al..they played great football despite being overaged...but it ended there...as usual,no consistency...sijui huyu MTAWA aliishia wapi...a great defender of his time
 


- Mkulu Nzoka, soma tena my original answer to the question of this mada, maana naona umeenda mbali sana, labda ufungue thread mpya inayohusu techincalities za soccer Tanzania, soma tena my original answer hapa juu!

- Kama ni wapopo, wanatujua sana Tanzania, kuanzia National team na Yanga, maana ile gemu na Asante Kotoko kwenye robo finali ya kombe la Osagwefyo Kwame Nkurumah, ilikuwa ni mechi ya the ages mkuu, unless hawajui history ya kabumbu la nchi yao, waambie ilichezewa uwanja wa Kumasi, in the early 80s na kipa wao alikuwa Robert Mensah, jina ambalo baadaye alilirithi Jumapondamali.

Respect.


FMEs!
 

Hapa naona kuna Tom n Jerry!! By the way, 1980 African Nations cup haikuwa Accra. Umekuwa ukichanganya data tangu mwanzo. Mtu mwenye jicho zuri ata interpolate na ku-extrapolate na ku-doubt data zako zote hata kama unajaribu kusema ukweli.

Sijawahi kuona mpopo anaitwa Mensah.....last time I checked, Asante Kotoko was from Ghana.
What you described here is stupid pride, it is sarcasm by the Ghanians....Yaani, a team beats you, and it has the nerve to clown your keeper by baptising with a name that conquered you. We are sad indeed. And these are our proudest moments.
It would be an achievement if one day a European player has a Tanzanian nickname ie Ryan Babbel "Manara", or Steven Gerald "China"......John Terry "Kassanga".....Peter Crouch "FM ES"...Ryan Giggs "Nteze/Lungu".

We really are losers. Hope ujumbe unawafikia FAT.

Merry x-mas my friend and I wish you a great 2010 to you and your close ones mkuu. No love lost, its just a game. If we didnt have arguments/discussions like this, a forum wouldnt be a forum
 

Word is born!
 


ulianza vizuri sana, ili ujue A ni mbaya lazima iwepo B ambayo ni nzuri.

Nje ni nje tu sio lazima ucheze hizo ligi zako bora ndio uwe mchezaji wa kimataifa.
 
FMES,Nzoka,....

..naona mmeshikana mashati kama washabiki wa Jordan na Kobe.

..nadhani suala la yupi ni mchezaji bora all time linakuwa gumu kuamuliwa kutokana na era walizoshiriki wachezaji hao kupishana.

..pia hapa bongo statistics haziko-compiled kama alivyoelekeza vizuri kabisa Nzoka. vilevile hatuna waandishi wa habari wa soka, football analists, and football historians, ambao wangeweza kusaidia katika kuchambua na kuweka kumbukumbu.

..kwa mtizamo wangu Taifa Stars iliyocheza fainali za Kombe la Afrika Lagos Nigeria nalazimika kuiweka juu kuliko timu nyingine za Taifa za Tz.

..si kweli kwamba timu zote za Afrika za wakati ule zilikuwa mbovu-mbovu. baadhi ya timu kama ya Zambia[KK 11] na Nigeria[Green Eagles] zilikuwa na wachezaji ambao mpaka leo wanakumbukwa nchini kwao kama one of the best.

..Nigeria kulikuwa na wachezaji kama Segun Odegbami, Mudashiru Lawal, Christian Chukwu,... hawa hata ukiuliza kwa ndugu zetu wa Nigeria watakwambia they came at a wrong time, na kwamba they were better than the likes of Amokachi,Okocha, Oliseh etc.

..huyu Segun Odegbami alikuwa ni kipande cha mtu kama Juma Mkambi au Sunday Oliseh, lakini alikuwa na mbio, ball control, na uwezo wa kutambaa na chaki, kama wa, au zaidi ya, Edibily Lunyamila.

..Mudashiru Lawal was just a ball of energy. jamaa alikuwa yupo kila mahali ambapo mpira ulikuwepo. huyu alikuwa ndiyo roho ya Green Eagles iliyokuwa chini ya kocha Mbrazili Otto Gloria.

..ukija kwenye KK 11 ya Zambia ilikuwa na wachezaji kama Dickson Chama, Peter Kaumba, Pele Kaimana, Alex Chola, etc. hii pia ilikuwa ni timu kali na kuna kipindi Kaumba na Chola walikuwa wanakubalika kama ma-winger hatari kabisa Afrika.

..naikubali ile timu ya 1981 kwasababu hakuna timu iliyoweza kufikia kiwango cha kucheza Africa Cup of Nations. pia vijana wale walikuwa na uwezo wa kuzi-challenge timu kali za Afrika kama hizi za Nigeria na Zambia. ulikuwa huwezi kusikia tunafungwa na timu za nchi ndogo-ndogo kama Burundi, Rwanda, au hata Kenya.

..nakumbuka vijana wetu walipotoka Nigeria, Harambee Stars walikuja DSM na tukawachabanga bao 5 -- 1 au 5 -- 0.

..Stars ya iliyongara kule Lagos -- Surulele stadium ilikuwa kama ifuatavyo:

1.Juma Pondamali/Athuman Mambosasa 2.Leopold Tasso Mukebezi/Daudi Salum 3.Mohamed Kajole Machela 4.Salim Amiri 5.Jella Mtagwa 6.Leodgar Tenga 7.Omari Hussein 8.Hussein Ngulungu 9.Peter Tino10.Mohamed Salum/Mohamed Adolf Rishard 11.Thuwein Ally.

..kwenye hii timu mchezaji ambaye aling'ara kwa muda mrefu kuliko wenzake ni JELLA MTAGWA. naamini huyu ni Captain wa Taifa Stars aliye-serve kwa muda mrefu kushinda wenzake. Jella Mtagwa ni mwanasoka pekee kuwa kwenye stempu za Tanzania. uwezo wake, pamoja na utulivu, alipokuwa uwanjani kama center back au "mkoba" hauna mfano mpaka leo.

..kuna wachezaji wengine ambao walikuwa very special wamepata kucheza hapa Tanzania. hapa nalazimika kumtaja SAIDI MWAMBA "KIZOTA." naamini Kizota ni mmoja kati ya wachezaji waliofunga mabao mengi ktk ligi zetu. pia huyu jamaa aliweza kucheza nafasi nyingi sana kama beki, kiuongo, mshambuliaji, na zote alizimudu vema.

..MOHAMED "ADOLF" RISHARD naye alikuwa special ingawa maumivu ya goti yalikatisha career yake. huyu namkubali kuwa kati wachezaji wenye IQ kubwa waliopata kucheza hapa Tanzania. alikuwa na uwezo wa kucheza nafasi zote za kiungo na ulinzi.
 
 

- Mkuu Joka, ahsante sana kwa kusisitiza uzito wa hoja zangu, maana all you did ni kuzikubali hoja zangu kwa kutumia maneno tofauti, ingawa naomba kusema tena kwamba wachezaji wa mchezo wowote dunaini wanahukumiwa uwezo wao wa kucheza kutokana na ushindi hasa internationally, kutokana na kukubalika kwao internationally,

- Sasa kwa dhana hiyo, wachezaji wa zamani wa soccer Tanzania bado wame-accomplish more kuliko wa sasa, ndio point yangu ya msingi na unaonekana kukubaliana nayo kutokana na hoja zako hapa.

Respect.


FMEs!
 


Swadakta Mkulu,

Haya uliyo yasema na mengi mengineyo huko nyuma ni kweli kabisa,umetuongezea wengi ufahamu wa soka letu tulipoanzia mpaka tulipofikia.
Ni ukweli usio fichika kwamba wachezaji wa zamani ndio,na bado wataendelea kua icons wa soko la letu,kwani wachezaji wetu wa kipindi hichi hawawezi kufikia mafanikio hayo,labda wenyewe kwa maamuzi yao binafsi waamue kubadirika katika mifumo mizima ya maisha yao na wawekezi nguvu na hari zao kwenye hiyo kazi yao ya mpira kama wachezaji hao wazamani tunao wasema walikua na mafanikio walivyokua wakifanya.
Sasa hivi kutokana na maendeleo ya utandawazi tunaweza kuona wachezaji wa ulaya wanapofanya mazoezi binafsi ukiachia yale ya pamoja ya kitimu,wachezaji wa kibongo wanatakiwa waache starehe na kufanya kazi kweli ili kufikia mafanikio kama hao wachezaji wa ulaya na waache kujibweteka kwenye ma-bar na starehe za kipumbavu kutokana na umaarufu kidogo waupatao.
Mfano,sio ajabu mchezaji wa sasa kutafuta waandishi wa habari jamaa zake wamuaandike vizuri kwenye magazeti yao ili apate umaarufu,mpira umekua kama kucheza sinema za kibongo,auzi mpaka uandikwe kwenye magazeti!scouting inafanya na watu wanye mapenzi binafsi na wachezaji au club wanazochezea.
wachezaji wazamani hawakua hivyo,walikua wanafanya mazoezi kweli kweli,na mafanikio yao yalikua yakionekana uwanjani viwango vya uchezaji na uwezo ulia mkubwa na wao ndio walio tamba kwa kipindi kilefu mpaka leo tunawakumbuka.
Nina mfano wa mchezaji mmoja ambaye alipata mafanikio,alikua na uwezo wa kukumbia kutoka alipokua akiishi 8-10 km mpka oesterbay beach na akifika hapumziki anaanza mwanzo wa beach mpaka mwisho mara kumi na zaidi anazunguka na anrudi kwa mbio hizo hizo mpaka nyumbani kwao,at last mchezaji huyu alipata mafanikio.Lakini wachezaji wetu wa kipindi hichi hawawezi kufanya hayo wao ni bora wende Mawela Bar (FM hiyo mawela bar ni bar moja ipo hapo sinza opposite na Vatican Hotel kwenye kiwanja kilipokua kiwanja cha wazi nadhani umeondoka siku nyingi huku wachezaji wengi wa kibongo ndio sehemu yao ya kula raha)
Namna hii,kamwe hatuta pata wachezaji wa kukumbukwa kama akina Dilunga,Manara,Gaga,Kibadeni,Pondamali,Mtawa,China,Lunyamila Masha,Method,Issa,Masatu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…