Toyota IST vs Toyota Aqua katika biashara ya Taxi

Toyota IST vs Toyota Aqua katika biashara ya Taxi

Satoh Hirosh

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2021
Posts
6,432
Reaction score
25,646
Habari wakuu,

Kuna huyu mdogo wetu kitaani hapa amemaliza chuo miaka kadhaa iliyopita ila yupo home Hana mishe za kueleweka. Sasa Mzee kastaafu na ameshachukua kiinua mgongo. Dogo amemwomba Mzee anunue gari ili awe anapiga mishe za taxi mtandao(Uber,bolt nk).

Chaguo lake yeye lilikuwa ni Toyota IST,lakini Mimi nikamshauri achukue toyota Aqua maana ni hybrid car Ina ulaji mzuri wa mafuta inaenda hadi 30km/h hivyo kwa Biashara ya taxi itakuwa nzuri kuliko IST.

Hilo lilikuwa pendekezo langu Mimi.

Ila yeye akaja na hoja kadhaa ambazo ni kama amenichallenji nimeshindwa kutetea hoja yangu.

Hoja zake anasema;

1.Aqua imekaa kimayai haiwezi kuhimili shida na routes za off-road kulinganisha na IST. IST anazikalisha gari nyingi mdogo kwenye hili ikiwemo na hii gari yangu niliyoipendekeza. Anasema IST gari ngumu haiwahi kuchakaa hasa ukizingatia itakuwa inapiga kazi karibia Kila siku,hivyo akaikataa gari Aqua katika hili.

2. Ground clearance.

Anasema Aqua ipo chini sana kulinganisha na IST,hivyo anaiona ni gari ya kwenye lami pekee. Akaniuliza vipi nikipata wateja wa bonyokwa na maji matitu niwakatae?

Kwa kifupi dogo ameikataa kabisa aqua na kung’ang’ania IST ingawa kwa hoja zake bado Mimi nilikuwa napendekeza aqua maana ni latest kuliko hiyo IST ya 2001.

Nimeona niletee humu ili kupata maoni tofauti kutoka kwa wajuzi na wataalamu wa magari,maana Mimi siyo mjuzi wa hilo eneo,japo nimempa ushauri dogo.
 
Toyota Aqua
markup_1000211113.png
 
Sawa ni wazo zuri ila usiwaze in one dimension tu mpe mawazo mengi mengi mfano atafute location iliyochangamka aanze kuuza spare parts za pikipiki au afungue hardware, maana hiyo hela ya kununua gari Ist used isiyo na kipengele inabidi aandae budget ya kwanzia million 11 hiyo pesa anaweza kuanza biashara nyingi tu ambazo zina mzunguko mzuri wa pesa zaidi, ila kama kadhamiria Tax tu sawa pia.
 
Wakati hiyo kazi angeiwexa kuifanya ata angeishia darasa la saba what a wastage of time en money
Hapana,

Mimi nimemwelewa dogo kwa nini amechagua hii Biashara ya taxi. Lengo ni kutengeneza connections.

Kwenye hii kazi unakutana na watu mbalimbali wenye exposure tofauti,business owners,HR's,CEO's nk,hivyo akiitumia kama chance kuna uwezekano wa kumpeleka kwenye stage nyingine. alAnaweza kufanikiwa.
 
Sawa ni wazo zuri ila usiwaze in one dimension tu mpe mawazo mengi mengi mfano atafute location iliyochangamka aanze kuuza spare parts za pikipiki au afungue hardware, maana hiyo hela ya kununua gari Ist used isiyo na kipengele inabidi aandae budget ya kwanzia million 11 hiyo pesa anaweza kuanza biashara nyingi tu ambazo zina mzunguko mzuri wa pesa zaidi, ila kama kadhamiria Tax tu sawa pia.
Sawa sawa.

Hili nalo tutamshauri aliangalie.
 
Hapana,

Mimi nimemwelewa dogo kwa nini amechagua hii Biashara ya taxi. Lengo ni kutengeneza connections.

Kwenye hii kazi unakutana na watu mbalimbali wenye exposure tofauti,business owners,HR's,CEO's nk,hivyo akiitumia kama chance kuna uwezekano wa kumpeleka kwenye stage nyingine. alAnaweza kufanikiwa.
Watu wanazeekea kwenye kuendesha hizo tax mpaka miaka 40 anafanya hiyo kazi hizo connection hazipati ndogo ndo anazipata tu, hiyo ni assumptions mbovu sana, clients wengi hataki kusemeshwa wakiwa kwenye tax sasa huyu dogo wako atakua anawahoji tu kweli atawexa hiyo kazi bila kupata ajali?
 
PureView zeiss ,Mad Max na wataalamu wengine wa magari.
Hapo hakuna zaidi ya IST , huo utofauti wa ulaji wa mafuta usikuchanganye bado IST inafaa zaidi kumbuka biashara ya Uber ataenda sehemu mbalimbali na mazingira ya hovyo hasa kipindi cha mvua .
Ushauri wake yupo sawa kabisaa mwambie IST ndiyo mpango mzima
 
Back
Top Bottom