KERO Tozo ya kimya kimya ya kununua umeme (LUKU) kupitia mitandao ya simu

KERO Tozo ya kimya kimya ya kununua umeme (LUKU) kupitia mitandao ya simu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Annonymous

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2013
Posts
688
Reaction score
1,126
Uzi uwe mfipi kabisa.

Nimefuatilia miamala yangu 6 ya kununua umeme ya mwishoni mwezi huu nimeona kuna tozo ya kununua umeme kwa njia ya simu (airtel money) ila haitajwi ni salio linakatwa tu kimya kimya.

Umeme wa elfu3 unakatwa TSH 90, Umeme wa elf 5 unakatwa TSH 100.

Umeme wa elf 1 unakatwa Tsh 80
Umeme wa 500 unakatwa Tsh 60.

Imenibidi kufuatilia hili baada ya kugundua mbona kila nikinunua umeme sms inakuja kuwa tokeni ni hii ila siambiwi baada ya kununua umeme salio limebakia Tsh ngap ni kimya kimya tu.

Kingine kwanini ukituma muamala, ule muamala badae ukikataa, pesa inarudishwa ila yale makato ya kutuma muamala huwa hayarudishwi wakati muamala haujafanikiwa.?

Tatu: kwanini muamala ukienda ukaurejesha haurejeshwi na makato yake inarudi elf 6 iliyotumwa bila 458 iliyokatwa kama makato
Screenshot_20240823-062139_Messages.jpg

Sample screenshot
 
hakuna tozo ya kimyakimya ndugu nafikiri elimu bado iko chini
 
Hiyo sio tozo gharama inayotozwa kwa kununua umeme kutoka kwa mtandao
 
Back
Top Bottom