Kama kuna mahali serikali hii imekosea ni kuhusu hii tozo ya miamala ya simu, madhara yake yatakuwa makubwa sana kwa biashara za watu wa chini. Wafanyabiashara wadogo wengi hawatumii bank kufanya manunuzi na malipo mbalimbali.
Tozo iliyowekwa ni kubwa kuliko faida tarajiwa katika muamala husika. Miamala mingi inafanyika kwa ajili ya kurahisisha tu kazi za watu lakini yenyewe haina faida hata iweze kumudu kulipa tozo kubwa namna hii. Wafanyabiashara wakubwa wanafanya biashara kupitia miamala ya kibenki, hawatumii miamala ya simu, kwa kiasi kikubwa huduma hii ni kwa ajili ya watu wa chini.
Ni kitu gani kimeifanya serikali ifikiri huku kutaleta mapato makubwa na kusahau athari zake. Huduma hii imekuwa kichocheo cha sekta zingine nyingi, kuifinyanga namna hii haiumii sekta hii peke yake bali unaathiri sekta nyingi za kiuchumi ambazo huduma hii imekuwa mwezeshi.
Hizi ni athari za hii tozo kwa mtazamo wangu;
1. Biashara ya fedha kwa simu itaathirika na ajira nyingi zitakufa kwa kukosa wateja
2. Wafanyabiashara wadogo ndio watakuwa waathirika wakubwa
3. Kasi ya mzunguko wa fedha kwenye uchumi itapungua sana
4. Watu wengi wataanza kutembea na cash na matumizi ya cash yatarudi kwa kiasi kikubwa.
5. Kampuni za simu zilizowekeza kwenye biashara hii zitaathirika sana
6. Kasi ya uchumi itapungua kufuatia kupungua kwa kasi ya shughuli za uzalishaji.
Ni vema serikali kama inataka mapato basi itambue ni kiasi gani cha tozo kinapaswa kutozwa pasipo kuathiri/kuua kabisa sekta nzima.
TOZO HII KUBWA MNO HAIBEBEKI NA HAINA UHALISIA NI MATESO MAKUBWA KWA WATU WA CHINI
Tozo iliyowekwa ni kubwa kuliko faida tarajiwa katika muamala husika. Miamala mingi inafanyika kwa ajili ya kurahisisha tu kazi za watu lakini yenyewe haina faida hata iweze kumudu kulipa tozo kubwa namna hii. Wafanyabiashara wakubwa wanafanya biashara kupitia miamala ya kibenki, hawatumii miamala ya simu, kwa kiasi kikubwa huduma hii ni kwa ajili ya watu wa chini.
Ni kitu gani kimeifanya serikali ifikiri huku kutaleta mapato makubwa na kusahau athari zake. Huduma hii imekuwa kichocheo cha sekta zingine nyingi, kuifinyanga namna hii haiumii sekta hii peke yake bali unaathiri sekta nyingi za kiuchumi ambazo huduma hii imekuwa mwezeshi.
Hizi ni athari za hii tozo kwa mtazamo wangu;
1. Biashara ya fedha kwa simu itaathirika na ajira nyingi zitakufa kwa kukosa wateja
2. Wafanyabiashara wadogo ndio watakuwa waathirika wakubwa
3. Kasi ya mzunguko wa fedha kwenye uchumi itapungua sana
4. Watu wengi wataanza kutembea na cash na matumizi ya cash yatarudi kwa kiasi kikubwa.
5. Kampuni za simu zilizowekeza kwenye biashara hii zitaathirika sana
6. Kasi ya uchumi itapungua kufuatia kupungua kwa kasi ya shughuli za uzalishaji.
Ni vema serikali kama inataka mapato basi itambue ni kiasi gani cha tozo kinapaswa kutozwa pasipo kuathiri/kuua kabisa sekta nzima.
TOZO HII KUBWA MNO HAIBEBEKI NA HAINA UHALISIA NI MATESO MAKUBWA KWA WATU WA CHINI