Tozo za miamala zitasaidia ujenzi wa Shule zaidi ya 10,000; zahanati zaidi ya 4,500 na vituo vya afya 570 ifikapo 2025. Uzalendo zaidi unahitajika

Tozo za miamala zitasaidia ujenzi wa Shule zaidi ya 10,000; zahanati zaidi ya 4,500 na vituo vya afya 570 ifikapo 2025. Uzalendo zaidi unahitajika

CM 1774858

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2021
Posts
5,621
Reaction score
5,029

Tozo za miamala ya simu zitasaidia ujenzi wa Shule zaidi ya 10,000; Zahanati zaidi ya 4,500 na vituo vya afya 570 ifikapo 2025, Uzalendo zaidi unahitajika kwani vizuri vinamaumivu,​


Tupige moyo konde, nikweli pesa hakuna,nikweli mzunguko wa pesa si mzuri sana ila tuwaache wenye pesa walisaidie Taifa lao kwa faida ya watoto leo na faida ya watoto wao kesho.

Tuacheni harakati kwenye maendeleo ya watu, hayupo Mjomba wala shangazi wakutujengea hizi barabara, shule,Zahanati,Hospitali kwaajili yetu na kwaajili ya watoto wetu na watoto wao ila ni sisi wenyewe.

[Hebu angalia faida za tozo kwenye sekta mbili tu za Afya na Elimu]

1. UJENZI WA VYUMBA 8,000- 10,000 VYA MADARASA VIPYA

Tunaweza kujenga shule 2,000 za O'level au shule 2,500 za A'level au Shule 1,428 za kidato cha ( I-VI) au Shule 1,250 za Msingi hii ni sawa na katika kila kata 2 itajengwa shule mpya 1 kwenye kata zote 3,956 au nisawa nakusema katika kila jimbo la uchaguzi kwenye majimbo yote 264 zitajengwa shule mpya 8 za Mama Samia likiwemo Jimbo la kaka yangu, "Thadei Ole Mushi " anayezipatia kigugumizi hizi tozo ,Nakwarejea tu,Tanzania tuna shule 5,330 tu za sekondari,Shule mpya nikaribu nusu ya shule zote za sekondari zilizowahi kujengwa tangu Uhuru kwanini tuendelee kunung'unikia tozo Kila siku tozo,

Nakama tozo hii itaenda mpaka 2025 Mama Samia atajenga shule mpya zinazofikia 10,000 hii ni sawa na kusema karibu kila kijiji kitakuwa na shule mpya ama ya sekondari ama ya msingi kupitia tozo za e-money.

2. UJENZI WA ZAHANATI MPYA 900

Hyt Rais Magufuli kwa miaka mitano alijenga Zahanati 1,198.Leo Mama Samia kwa kutumia Tozo ya Uzalendo atajenga Zahanati mpya 900 kwa mwaka 1 wa fedha yaani FY 2021|22.Hii ni sawa na Zahanati mpya 4,500 kwa miaka 5 yaani kila Jimbo zitajengwa Zahati mpya 4 katika kila mwaka wa fedha ni sawa na Zahanati 20 kwa kila jimbo kwa miaka 5 ya kwanza ya Mhe Samia Suluhu na hii ni kwamajimbo yote 264,Kwa lugha rahisi ifikapo 2025 kila kata itakuwa na Zahanati Mpya 2 za Mama Samia Suluhu Hassan,

3. UJENZI WA VITUO 234 VYA AFYA

Hyt Rais Magufuli kwa miaka 5 alikarabati na kujenga jumla ya vituo vya afya 487,Leo Mhe Rais Samia Suluhu kwa kutumia Tozo ya e-money atajenga vituo vipya 234 kwa mwaka 1 huu na nusu sawa na vituo 570 kwa miaka 5 ya awamu ya kwanza,Kwa lugha rahisi mwaka 2025 kila Wilaya itakuwa na Vituo vipya 4 vya afya vya Mama Samia Suluhu Hassan vitakavyohudumia watoto wa masikini wa nchi hii,


Itaendelea, kazi iendelee...

photo_2021-10-07_12-10-20.jpg
 
Pia uzalengo huo uwahusu wao waanze kukatwa kodi kila mbunge akatwe kodi serikali itakusanya zaidi ya milion 500 kila mwezi ambazo zitasaidia maendeleo.

Uzalendo gani ambao una mipaka kwa hao wanawahamasisha wenzao wakatwe kodi kwanini wao hawataki kukatwa.
 
Pia uzalengo huo uwahusu wao waanze kukatwa kodi kila mbunge akatwe kodi serikali itakusanya zaidi ya milion 500 kila mwezi ambazo zitasaidia maendeleo.
Uzalendo gani ambao una mipaka kwa hao wanawahamasisha wenzao wakatwe kodi kwanini wao hawataki kukatwa
Naunga mkono hoja, Wabunge wakatwe kodi,Wengine wanalala bungeni eti baadae wanampigia rais apunguze makato stupid

MAMA KATA KODI WABUNGE WOTE
 
Naunga mkono hoja, Wabunge wakatwe kodi,Wengine wanalala bungeni eti baadae wanampigia rais apunguze makato stupid

MAMA KATA KODI WABUNGE WOTE
Huu ni ujinga wa hali ya juu, hii sisheria wameipitisha wao bungeni juzijuzi tu, sasa yini kutufanyia maagizo
 
Kama MO, BAKRESA na GSM watalalamika namimi nitalalamika ila nashanga mtu anakatwa 4,200 analialia hajua hawa matajiri kwa siku wanakatwa mamilioni na hawana kelele, Masikini hana jema.

Shida sio makato shida Magufuli alitupiga kiuchimi balaaaaa, elfu 4,200 inaumaa
 
Tulipe kodi, mbona sio hela nyingi, tena ukilinganisha na nchi za wenzetu, kodi yetu ya miamala iko chini nitaweka data hapa, watanzania hawana utamaduni wa kutaka kulipa kodi, watumishi wa umma na sector binafsi ndio walipaji wakubwa wa kodi.

Ila wafanya biashara huwa hawataki hata kusikia 1% ya kodi imeongezeka. Watumishi wa umma hulipa hadi 30% ya makato yote ya mshahara. Ila mfanyabiashara akisikia hata 3% ya kodi imeongezeka, ni kelele na hawataki kusikia. Tulipe kodi plz
 
Tulipe kodi, mbona sio hela nyingi, tena ukilinganisha na nchi za wenzetu, kodi yetu ya miamala iko chini nitaweka data hapa, watanzania hawana utamaduni wa kutaka kulipa kodi, watumishi wa umma na sector binafsi ndio walipaji wakubwa wa kodi. Ila wafanya biashara huwa hawataki hata kusikia 1% ya kodi imeongezeka. Watumishi wa umma hulipa hadi 30% ya makato yote ya mshahara. Ila mfanyabiashara akisikia hata 3% ya kodi imeongezeka, ni kelele na hawataki kusikia. Tulipe kodi plz
Watanzania hawaeleweki juzi walisema tuwapunguzie kodi wawekezaji wanakimbia Leo wao nao wanalalamikia kodi sijui wao watakimbilia nchi gani

Hakuna cha bure, No pain no gain

Shida ya Mwigulu hatoi ufafanuzi mzuri kwa wananchi waelewe kwanini makato sasa.
 
Pia uzalengo huo uwahusu wao waanze kukatwa kodi kila mbunge akatwe kodi serikali itakusanya zaidi ya milion 500 kila mwezi ambazo zitasaidia maendeleo.
Uzalendo gani ambao una mipaka kwa hao wanawahamasisha wenzao wakatwe kodi kwanini wao hawataki kukatwa.
Ati kwa nini wao hawataki kukatwa kodi lakini wanatuhamasisha sisi tulipe kodi? Au wao ni wananchi zaidi ya sisi?
 
HIZI HAPA FAIDA ZA TOZO MPYA KWA WATOTO WA MASIKINI WA NCHI

Tupige moyo konde, najua pesa hakuna,najua mzunguko wa pesa hakuna ila tuwaache wenye pesa wasaidie Taifa lao kwa faida ya watoto wetu kesho.

Tuache harakati kwenye maendeleo ya watu, hayupo Mjomba wala shangazi wakutujengea barabara, shule,Zahanati,Hospitali kwaajili yetu na kwaajili ya watoto wetu na watoto wao ila ni sisi wenyewe.

[Hebu angalia faida za tozo kwenye sekta mbili tu za Afya na Elimu]

1. UJENZI WA VYUMBA 10,000 VYA MADARASA

Tunaweza kujenga shule 2,000 za O'level au shule 2,500 za A'level au Shule 1,428 za kidato cha ( I-VI) au Shule 1,250 za Msingi hii ni sawa na katika kila kata 2 itajengwa shule mpya 1 kwenye kata zote 3,956 au nisawa nakusema katika kila jimbo la uchaguzi kwenye majimbo yote 264 zitajengwa shule mpya 8 za Mama Samia likiwemo Jimbo la kaka yangu, "Thadei Ole Mushi " Nakwarejea tu,Tanzania tuna shule 5,330 tu za sekondari,Shule mpya nikaribu nusu ya shule zote za sekondari zilizowahi kujengwa tangu Uhuru,

Nakama tozo hii itaenda mpaka 2025 Mama Samia atajenga shule mpya zinazofikia 10,000 hii ni sawa na kusema karibu kila kijiji kitakuwa na shule mpya ama ya sekondari ama ya msingi kupitia tozo za e-money.

2. UJENZI WA ZAHANATI MPYA 900

Hyt Rais Magufuli kwa miaka mitano alijenga Zahanati 1,198.Leo Mama Samia kwa kutumia Tozo ya Uzalendo atajenga Zahanati mpya 900 kwa mwaka 1 wa fedha|FY 2021/22.Hii ni sawa na Zahanati mpya 4,500 kwa miaka 5 yaani kila Jimbo zitajengwa Zahati mpya 4 katika kila mwaka wa fedha ni sawa na Zahanati 20 kwa miaka 5 ya kwanza ya Mhe Samia Suluhu na hii ni kwamajimbo yote 264,Kwa lugha rahisi ifikapo 2025 kila kata itakuwa na Zahanati Mpya 2 za Mama Samia,

3. UJENZI WA VITUO 114 VYA AFYA

Hyt Rais Magufuli kwa miaka 5 alikarabati na kujenga jumla ya vituo vya afya 487,Leo Mhe Rais Samia Suluhu kwa kutumia Tozo ya e-money atajenga vituo vipya 114 kwa mwaka 1 sawa na vituo 570 kwa miaka 5 ya awamu ya kwanza,Kwa lugha rahisi mwaka 2025 kila Wilaya itakuwa na Vituo vipya 4 vya afya vya Mama Samia vitakavyohudumia watoto wa masikini

Itaendelea, kazi iendelee...

C&P
Hayo yote yanaweza kufanyika bila kuumiza wananchi,Mama aanze na kupunguza wizi wa pesa na matumizi mabaya,Kuna watu walijilipa millioni 500 kwa siku kwenye vikao vya bord,pale TASAC,mama akawapa vyeo,Kuna njemba za hazina nazo ziliupiga mwingi zikajilipa ,300 millioni kama posho za may day,wakati may day ilifanyika Mwanza,,!waziri mkuu alienda pale akademka demka,mambo yakaishia hapo.
Uliyotaja sio mapya yanaweza kujengwa kwa pesa yoyote,sio rocket science kujenga hivyo vitu
 
Watanzania hawaeleweki juzi walisema tuwapunguzie kodi wawekezaji wanakimbia Leo wao nao wanalalamikia kodi sijui wao watakimbilia nchi gani

Hakuna cha bure, No pain no gain

Shida ya Mwigulu hatoi ufafanuzi mzuri kwa wananchi waelewe kwanini makato sasa.
Swala la ufafanuzi ni kwa sababu ni mjivuni anadharau kwa wananchi
 
Back
Top Bottom