Tozo za miamala zitasaidia ujenzi wa Shule zaidi ya 10,000; zahanati zaidi ya 4,500 na vituo vya afya 570 ifikapo 2025. Uzalendo zaidi unahitajika

Tanzania tuna viongozi wabinafsi kupindukia!!

Hebu pata picha:
Wabunge wanalipwa kiasi gani bila kodi. Wanapokea marupurupu kibao, na hata fedha zao za bima wanapewa zote kwa mkupuo mwisho wa miaka mitano bila kucheleweshewa.
Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Idara, Wakuu wa Taasisi za Serikali wanaendesha magari ya kifahari ya serikali, yakihudumiwa kwa kodi za wananchi...NK. NK.

Leo hii wako mstari wa mbele wanamwambia mtanzania "afunge mkanda tujenge nchi!" Hawana hata soni yakuonyesha uzalendo kwa kupunguza matumizi au hata kuchangia kodi!

LOH! Inatia hasira na kinyaa!! Hata shetani anachukua somo kwetu!
 
Hebu tueleweshane mkuu...Ni CCM ndio inajenga shule, miundo mbinu na huduma za umma, au ni SERIKALI kupitia KODI ZA WANANCHI, FEDHA ZA MAENDELEO na MIKOPO?
 
kwani umesikia hatulipi kodi?
 


Shida sio namna gani pesa hiyo itatumika, shida ni namna pesa hiyo inavyopatikana kiharamu.

Njia mbovu inatumika (wizi) kutekeleza jambo zuri, mojakwamoja jambo hilo litakuwa halina baraka kwasababu litakuwa limepatikana kwa njia haranu.

Hiyo ndio point.
 
Uhuni mtupu
 
ni sawa na mavi kuyapaka asali ili kudanganishia walaji



Sisi tunaokaa vijijini ndio tunaelewa maana ya Zahati ya kijiji, Shule ya kijiji au kata, Sisi ndio tunajua adha ya maisha,

Mnaopinga ni nyie mnaoishi mjini na ndio maana mnamiliki hata simu,

Njooni mtuhoji hukuvijiji nasisi,

Sisi tunataka shule, zahati na barabara mengine ya tozo tutavumilia
 
Kwa CCm hii akuna wanachowez kutekeleza hz ni siasa miaka 60 uhuru wameshindwa kufanya hayo zaidi waTz wamekuwa masikin zaidi
 
Yote hayo yanaweza kufanyika kupitia madini.Miaka 60 ya Uhuru bado unajenga shule na zahanati kupitia tozo za raia maskini ni upumbavu.waziri tengeneza chanzo kipya Cha mapato,chukua Kodi kwenye mishahara ya wabunge,tumia bahari kuyageuza maji kuwa pesa,geuza Simba was Serengeti kuwa pesa.ukifanya hayo utakuwa waziri mwena.
 
Watz bado hatuko serious na mambo yetu. Watu wanacheza na uhai wetu halafu wengine wanaona poa tu wa miaka yote hiyo walikuwa wapi kujenga hiyo miundombinu mpaka tukamuliwe kwenye miamala tunayoifanya.
Tunaona bora tumalize hili suala ujenzi haushi sasa wananchi tuungane pamoja kwenye kodi ya uzalendo tunamaliza ujenzi wa shule na vituo vya afya nchi nzima tunafunga kazi halafu tunahamia kwenye barabara zilizobaki za vumbi nchi nzima tunatandaza lami sio kila siku ni kujenga tuu wenzetu nchi zilizo endelea haya mambo walimaliza kitambo sana na hawana mgodi wa mbuga ya wanyama ni kodi tu kutoka kwa wananchi wake kwanini na sisi tushindwe.
 
Ebu taja ni nchi gan iliyoendelea kwa kutegemea kodi kutoka kwa wananchi tu
 
Amekuuliza pesa za uwanja wa ndege chato, pesa wanazotembea nazo mifukoni wanagawa. Sasa hivi mnataka kujenga sanamu tu kwa hela inayolingana na mikopo ya wanafunzi. Ukiwa nacho mfukoni wala hufikirii wasiokuwa nacho. Kama wengine waliweza bila tozo kwa nn huyu asiweze. Wakiisha pata hela na kujenga sifa na kujidai maemdeleo yanaletwa na CCM.
 
Pumbavu zenu wakati mnashangilia watu kuporwa pesa zao wakiitwa mafisadi mlijua ni raha? Sasa hii ni zamu ya wote hakuna cha mwenyenacho au asiyenacho.
 
Hata hiyo hela yenyewe ya kufanya hiyo miamala tunayo basii..ni kelele tu tunapiga mwisho wa siku hata hayo malengo hamtoyafika sababu hiyo elfu 30 ya kumtumia mjomba kijijini hata hatuna
 
umeongea kizalendo Sana Jay
 
Cheap propaganda......
Tanzania tatizo sio kukusanya Kodi ndugu yangu, watanzania hawajakataa kulipa Kodi, watanzania hawajakataa maendeleo ila tujiulize, je hizo pesa tunazokusanya kidogo zinatumikaje? Maana tuanzie hapo inawezekana tukaelewana kwa mfano bajeti ya mwaka huu pesa itakayokusanywa asilimia kubwa inaenda kwenye matumizi ya kawaida badala ya maendeleo, yaani wamepanga matumizi yatakua zaidi ya 33trillion lakini zaidi ya 20trillion zinaenda kwenye matumizi ya kawaida ie mishahara,posho, usafiri alafu zinazobaki zaidi ya 13trillion ndio ziende kwenye maendeleo ie afya,maji,elimu nk. Sasa kwa namna hiyo hata kama tutakabana mpaka tutoke damu kukusanya pesa nyingi kiasi gani bado suala la maendeleo litabaki ni hadithi tu kwa sababu viongozi hawako serious kwenye maendeleo zaidi ya kuteneza mazingira ya kujinufaisha wao ndio maana hata hizo shule au hospitali zilizopo hazina huduma bora na wao na familia zao hawaendi huko.
 
Kwa nini tusisimamie Natural resources zotee tukapata hela tujenge hizo classes na zahanati.

Hayati alisema tusimamie kodi kubwakubwa za madini, bandari etc...

Achana na hizi za kumuumiza mwananchi .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…