Tozo zinalemaza serikali kubuni miradi mipya

Tozo zinalemaza serikali kubuni miradi mipya

BARADIGE

Member
Joined
May 22, 2014
Posts
70
Reaction score
32
Habari za muda huu Wana Jamvi,
Kutokana na Hali hii inayo endelea ambapo Kila kunapo kuchwa serikali yetu inakuja na TOZO mpya za Kila kitu hii inapelekea serikali kuji sahau na kumuumiza mwananchi.

Kwa Sasa siyo Tena makato ya simu Hadi tulipo kimbilia benk Hali ni hiyo hiyo Serikali imeshindwa KUBUNI njia mbadala wa kuongeza kipato tofauti na Hali hii ya leo, Mwananchi maisha yamekuwa magumu lakini hii haitoshi ila serikali ijitathmini viongozi waliokuwepo wenye dhamana ya kutoa muongozo wa MIRADI itakayo ongeza kipato hawastahili kuwa sehemu hizo.

Wimbi la vijana wasio na kazi ni wengi huku wafanyabiashara wadogo (Machinga) wamekatazwa kujitafutia penye mzunguko wawatu lakini Kila kunapo kucha SERIKALI inatangaza kuweka TOZO hapa na pale.

Hii inasikitisha sana. Ni wazi Sasa
SERIKALI ikubali kuwa watu wake waneshindwa kujibu maswali magumu ya kupata pato la kuendesha nchi mwisho wamekuja kumuumiza mwananchi kwakuwa wao Wana upanga.
 
Naipa pole serekali yetu kwa mzigo mzito iliyopo ya umaliziaji wa miradi iliyopo, Inshaallah haya ni ya muda tu na yatapita,
Miradi ni lazima ikamilike
Nafahamu tumejifunga mkanda sote kwa pamoja kuimaliza miradi lukuki iliyopo.
Tutakapoimaliza tutapumua kwa pamoja.
#Kazi_iendelee.
 
Back
Top Bottom