TRA chukueni ushauri huu (kulipa kwa installments) juu ya kodi kwenye imported goods

TRA chukueni ushauri huu (kulipa kwa installments) juu ya kodi kwenye imported goods

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Kwema Wakuu?

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Tanzania ni nchi ambayo inaingiza au kuagiza bidhaa nyingi kutoka nje. Bidhaa hizi zinaweza kua za mahitaji au matumizi binafsi, bidhaa za biashara, bidhaa kwa ajili ya kutoa huduma, etc.

Ukiacha bidhaa hizi zinazoagizwa sasa, wapo pia wengine wangependa kuagiza lakin wanashindwa kwa kuogopa ushuru ulivyo mkubwa. Kwamba wanaweza kagiza kisha mizigo ikafika kwa wakati ambao mambo ya fedha yameyumba mizigo ikaishia kupigwa mnada bandarini ikawa hasara kwao.

Ushauri wangu ni kwa mamlaka ya mapato kuruhusu waagiza bidhaa KULIPA KWA AWAMU (INSTALLMENTS). Yaani mfano nimenunua gari ushuru ukaja labda 9Mil basi kuwe na maximum miezi 6 labda ya kulipa kwa awamu. Naweza nikawa natoa japo 1.5Mil kia mwezi kulipa TRA ili after 6months niwe nimemaliza deni la 9Mil.

Hii itawawezesha wengi kuagiza bidhaa hizi kutoka nje ya nchi wakijua kua mzigo utakapofika bandarini basi watakua wnaalipa kidogo kidogo mpaka kodi ikiisha. Mteja hatoruhusiwa kuchukua bidhaa zake mpaka atakapomaliza deni la kodi yake kwa hiyo miezi 6. Na ikitokea hapo kati mambo yakakaa vizuri basi amalizie tu deni lilobaki.

TRA inaweza kujenga "ma-godown" ya kuhifadhi hizo bidhaa (bonded warehouse) na ikawa inalipisha kodi ya kuhifdhi mizigo kwa gharama rafiki tu. Inaweza ikaonekana kama inachelewesha mapato kwenye mamlaka lakini kwenye uhasibu kuna kitu kinaitwa "acrrual", ambapo kwa muktadha huu ni kua mapato yatahesabiwa pale tu mzigo utakapoingia, na sio mpaka malipo yake yawe yamefanywa yote.

Hili likifanyika, litawashawishi wengi zaidi kuagiza bidhaa nje, walipa kodi wataongezeka na hata kwenye hizo bonded warehouse mapato pia yataongezeka. Ingawa Ki uchumi kuagiza bidhaa nje ni hasara zaidi kuliko kutumia bidhaa zako za ndani, lakini sababu ni swala ambalo haliepukiki basi serikali haina budi kuweka mazingira mazuri ya uagizaji huo.
 
Umefikiria mustakabali wa bidhaa zinazo zalishwa ndani. Kodi haipo kwa ajili ya kupata mapato tu. Kodi ipo pia kwa ajili ya kulinda soko la ndani. Hizo changamoto za kikodi zinazotokana na kuagiza bidhaa nje ndio zitakupelekea kununua bidhaa za ndani.

Lakini pia inabidi ufikirie kuhusu Value Chain. Wafanya biashara wa ndani wanapoagiza bidhaa na kuziuza kwa soko la ndani kunakua impact kwenye uchumi wa ndani sasa kukiwa na unafuu wa kikodi kuagiza bidhaa nje unategemea biashara za ndani zitakua?
 
Umefikiria mustakabali wa bidhaa zinazo zalishwa ndani. Kodi haipo kwa ajili ya kupata mapato tu. Kodi ipo pia kwa ajili ya kulinda soko la ndani. Hizo changamoto za kikodi zinazotokana na kuagiza bidhaa nje ndio zitakupelekea kununua bidhaa za ndani.

Lakini pia inabidi ufikirie kuhusu Value Chain. Wafanya biashara wa ndani wanapoagiza bidhaa na kuziuza kwa soko la ndani kunakua impact kwenye uchumi wa ndani sasa kukiwa na unafuu wa kikodi kuagiza bidhaa nje unategemea biashara za ndani zitakua?
Viwanda vya ndani inabidi vilindwe. Lakin umeshajiuliza Kwanini bidhaa zinazotoka nje ambako zimelipiwa kodi na usafiri ziwe na unafuu wa bei kuliko za ndani?

Unafuu naouzungumzia mimi huko kwenye kiwango cha kodi, bali mechanisms za kuilipa hiyo kodi.
 
Wazo zuri japo linahitaji mipango mizuri asee
Sahihi kabisa,
Ikiwekwa mipango mizuri basi swala hili litakua na tija pamoja na ufanisi. Hakuna kodi itakayokwepwa au kupotea sababu kutakua na ukomo (deadline) wa awamu za kuilipa.
 
Umefikiria mustakabali wa bidhaa zinazo zalishwa ndani. Kodi haipo kwa ajili ya kupata mapato tu. Kodi ipo pia kwa ajili ya kulinda soko la ndani. Hizo changamoto za kikodi zinazotokana na kuagiza bidhaa nje ndio zitakupelekea kununua bidhaa za ndani.

Lakini pia inabidi ufikirie kuhusu Value Chain. Wafanya biashara wa ndani wanapoagiza bidhaa na kuziuza kwa soko la ndani kunakua impact kwenye uchumi wa ndani sasa kukiwa na unafuu wa kikodi kuagiza bidhaa nje unategemea biashara za ndani zitakua?
Tengenezeni magari pia tununue hapahapa ndani
 
Kwema Wakuu?

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Tanzania ni nchi ambayo inaingiza au kuagiza bidhaa nyingi kutoka nje. Bidhaa hizi zinaweza kua za mahitaji au matumizi binafsi, bidhaa za biashara, bidhaa kwa ajili ya kutoa huduma, etc.

Ukiacha bidhaa hizi zinazoagizwa sasa, wapo pia wengine wangependa kuagiza lakin wanashindwa kwa kuogopa ushuru ulivyo mkubwa. Kwamba wanaweza kagiza kisha mizigo ikafika kwa wakati ambao mambo ya fedha yameyumba mizigo ikaishia kupigwa mnada bandarini ikawa hasara kwao.

Ushauri wangu ni kwa mamlaka ya mapato kuruhusu waagiza bidhaa KULIPA KWA AWAMU (INSTALLMENTS). Yaani mfano nimenunua gari ushuru ukaja labda 9Mil basi kuwe na maximum miezi 6 labda ya kulipa kwa awamu. Naweza nikawa natoa japo 1.5Mil kia mwezi kulipa TRA ili after 6months niwe nimemaliza deni la 9Mil.

Hii itawawezesha wengi kuagiza bidhaa hizi kutoka nje ya nchi wakijua kua mzigo utakapofika bandarini basi watakua wnaalipa kidogo kidogo mpaka kodi ikiisha. Mteja hatoruhusiwa kuchukua bidhaa zake mpaka atakapomaliza deni la kodi yake kwa hiyo miezi 6. Na ikitokea hapo kati mambo yakakaa vizuri basi amalizie tu deni lilobaki.

TRA inaweza kujenga "ma-godown" ya kuhifadhi hizo bidhaa (bonded warehouse) na ikawa inalipisha kodi ya kuhifdhi mizigo kwa gharama rafiki tu. Inaweza ikaonekana kama inachelewesha mapato kwenye mamlaka lakini kwenye uhasibu kuna kitu kinaitwa "acrrual", ambapo kwa muktadha huu ni kua mapato yatahesabiwa pale tu mzigo utakapoingia, na sio mpaka malipo yake yawe yamefanywa yote.

Hili likifanyika, litawashawishi wengi zaidi kuagiza bidhaa nje, walipa kodi wataongezeka na hata kwenye hizo bonded warehouse mapato pia yataongezeka. Ingawa Ki uchumi kuagiza bidhaa nje ni hasara zaidi kuliko kutumia bidhaa zako za ndani, lakini sababu ni swala ambalo haliepukiki basi serikali haina budi kuweka mazingira mazuri ya uagizaji huo.
Hizo installments unalipia mzigo ukiwa umekufikia au unauacha mpaka umalize deni? Kodi za ndani tu watu wanakwepa na wana installments 4 kwa mwaka.

Yaani mbongo umkabidhi gari mkononi hajamaliza ushuru? Vilio kutoka TRA vitakuwa sio vya mchezo
 
Hizo installments unalipia mzigo ukiwa umekufikia au unauacha mpaka umalize deni? Kodi za ndani tu watu wanakwepa na wana installments 4 kwa mwaka.

Yaani mbongo umkabidhi gari mkononi hajamaliza ushuru? Vilio kutoka TRA vitakuwa sio vya mchezo
Hapana Mkuu,
Nimeandika pale kua mzigo utachukua ukimaliza deni lako lote. Kuhusu kulipia nadhan mzigo ukifika wakafanya assessment na kujua value (then kodi yake) ndio uanze kulipa.
 
Hapana Mkuu,
Nimeandika pale kua mzigo utachukua ukimaliza deni lako lote. Kuhusu kulipia nadhan mzigo ukifika wakafanya assessment na kujua value (then kodi yake) ndio uanze kulipa.
Hapo sawa mkuu, wazo zuri sana
 
Umefikiria mustakabali wa bidhaa zinazo zalishwa ndani. Kodi haipo kwa ajili ya kupata mapato tu. Kodi ipo pia kwa ajili ya kulinda soko la ndani. Hizo changamoto za kikodi zinazotokana na kuagiza bidhaa nje ndio zitakupelekea kununua bidhaa za ndani.

Lakini pia inabidi ufikirie kuhusu Value Chain. Wafanya biashara wa ndani wanapoagiza bidhaa na kuziuza kwa soko la ndani kunakua impact kwenye uchumi wa ndani sasa kukiwa na unafuu wa kikodi kuagiza bidhaa nje unategemea biashara za ndani zitakua?
Bidhaa za ndani ni zipi mkuu?
 
Back
Top Bottom