TRA inakusanya kodi hadi kwa Maduka ya Mtaani wakati Madalali wapo Mitaani wanaingiza fedha ndefu bila makato yoyote

TRA inakusanya kodi hadi kwa Maduka ya Mtaani wakati Madalali wapo Mitaani wanaingiza fedha ndefu bila makato yoyote

Kayugumis

Senior Member
Joined
Jun 6, 2022
Posts
107
Reaction score
97
Juzi kati nilikuwa katika mishe zangu za harakati za kupambania mkate wa kila siku ambayo ilihusisha uuzaji wa nyumba. Biashara ikafanyika vizuri na mwisho wa siku dalali akaondoka na Shilingi 10.

Tangu siku hiyo nimekaa nikiwaza ni kiasi gani cha mapato Serikali inapoteza kama kodi kutoka katika sekta isiyo rasmi. Licha ya nchi yetu kuwa na watu zaidi ya milioni 60 ila walipa kodi hawazidi milioni 2 na wakati huohuo TRA imesajili walipa kodi wasiozidi milioni 5.

Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande akihutubia Bunge tarehe 6/9/2023 alidai sekta isiyo rasmi inakadiriwa kuajiri watu karibu milioni 27.7, Swali je, ni wangapi wanalipa kodi halali? na Serikali imechukua hatua zipi ili kuwawezesha watu hao kulipa kodi?

Sheria za kodi za Tanzania zina mtambua mtu mwenye kipato cha kuanzia Sh 270,000/= kulipa kodi ila wanaolipa kodi kwa sasa ni wale walio katika mfumo rasmi wa ajira, walio nje ya mfumo rasmi wa ajira hawalipi kodi hata kama kipato chao kinazidi kiwango cha laki mbili na sabini.

Sekta ya Udalali kwa miaka ya hivi karibuni imekua sana na imeingiliana na sekta kama kilimo, real estate, utalii, biashara nk ila mchango wake katika kuongeza mapato ya nchi kupitia kodi naweza kusema ni sawa na sifuri kabisa licha ya kwamba wanaingizi pesa nyingi.

Madalali wa nyumba, viwanja, magari wamekuea wakijipatia kipato kikubwa bila ya kulipa kodi kwa Serikali, kuna wakati wanachukua mpaka Asilimia 10 ya malipo ya walichodalalia.

Fikiria dalali anayeuza kiwanja/nyumba Kariakoo anaondoka na kiasi gani cha mapato? Kuna case madalali wanaondoka mpaka na Sh Milioni 50+ kwa kuuza jengo moja na wala hawalipi kodi sababu wapo kwenye sekta isiyo rasmi.

Kuna madalali wa mazao ambao wanafaidika kuliko Wakulima, ukirudi sekta ya uvuvi nayo wavuvi na walio kwenye mnyororo wa thamani wa uvuvi wengi wao hawalipi kodi, hivyo Serikali kukosa mapato.

Wito wangu kwa Serikali na hasa TRA watafute njia za kuingiza sekta isiyo rasmi katika ulipaji wa kodi maana uko ndipo hela nyingi ilipo.

Nchi kubwa kama hii yenye watu zaidi ya milioni 60 haiwezi kuendelea kwa kuwa na walipa kodi wasiozidi milioni 2 tena ambao hawalipi kodi kihalali, kila mtu anapaswa kuchangia maendeleo ya nchi yetu na maendeleo haya yanaletwa kwa kulipa kodi.

TRA wanatakiwa kuja na mbinu rafiki na madhubuti kuhakikisha watu wote wanaostahili kulipa kodi basi wanalipa kodi stahiki, kama TRA inaweza kukusanya kodi hadi kwenye maduka ya rejareja (kwa mangi) yalipo mitaani basi pia inaweza kukusanya kodi kwa madalali waliopo mitaani.

Mfano mosi, kuhakikisha kila mwenye nyumba / jengo / kiwanda / gari au mali yoyote inayouzwa kuwasilisha makato aliyomkata dalali la sivo basi yeye mnunuzi ndio atawajibika kulipa makato hayo.

Pili, kufatilia na kujiridhisha na miamala ya fedha ya kila mtu kama ni halali na imelipiwa kodi stahiki kuhakikisha kila kipato kinachoonekana katika miamala ya kibenki, simu nk imelipa kodi stahiki, maana leo hii Mtanzania anaweza kufanya miamala ya kibenki au simu bila kuulizwa chanzo cha kipato chake na kama kimelipiwa kodi.

TRA ikitaka kuongeza wigo wa kukusanya kodi basi sekta isiyo rasmi ndio mahali sahihi pa kuanzia kukusanya kodi ila kwa njia rafiki
 
Juzi nilikua katika mishe zangu za harakati za kupambania mkate wa kila siku ambayo iliuisisha uuzaji wa nyumba. Biashara ikafanyika vizuri na mwisho wa siku dalali akaondoka na 10 milion taslim.
Tangu siku hyo nimekaa nikiwaza ni kiasi gani cha mapato serikali inapoteza kama kodi kutoka katika sekta isiyo rasmi. Licha ya nchi yetu kua na watu zaidi ya milioni 6 ila walipa kodi hawazi milioni 2 na wakati huo huo TRA imesajili walipa kodi wasiozidi milioni 5.
View attachment 3175029
Naibu waziri wa fedha mh.Hamad chande akihutubia bunge tarehe 6/9/2023 alidai sekta isiyo rasmi inakadiriwa kuajiri watu karibu milioni 27.7 ,Swale je ni wangap wanalipa kodi?na serikali imechujua hatua zipi ili kuwawezesha watu hao kulipa kodi?sheria za kodi za tanzania zinamta mtu mwenye kipato cha kuanzia 270,000/= kulipa kodi ila wanaolipa kodi kwa sasa ni wale walio katika mfumo rasmi wa ajira, walio nje ya mfumo rasmi wa ajira hawalipi kodi hata kama kipato chao kinazidi kiwango cha laki mbili na sabini. Sekta ya udalali kwa miaka ya hivi karibuni imekua sana na imekua ikiingilia na sekta kama kilimo,real estate,utalii,biashara nk ila mchango wake katika kuongeza mapato ya nchi kupitia kodi naweza kusema ni sawa na sifuri kabisa licha ya kwamba wanaingizi pesa nyingi.madalali wa nyumba,viwanja,magari wamekua wakijipatia kipato kikubwa bila ya kulipa kodi kwa serikali,kuna wakati wanachukua mpaka asilimia 10 ya malipo ya walichodalalia.Fikiria dalali anayeuza kiwanja/nyumba kariakoo anaondoka na kiasi gani cha mapato?kuna case madalali wanaondoka mpaka na 50+milioni kwa kuuza jengo moja na wala hawalipi kodi sababu wapo kwenye sekta isiyo rasmi.Kuna madalali wa mazao ambao wanafaidika kuliko wakulima.Ukirudi sekta ya uvuvi nayo wavuvi na walio kwenye mnyororo wa thmani wa uvuvi wengi wao hawalipi kodi hvo serikali kukosa mapato.
Wito wangu kwa serikali na hasa TRA watafute njia za kuingiza sekta isiyo rasmi katika ulipaji wa kodi maana uko ndipo hela nyingi ilipo.Nchi kubwa kama hii yenye watu zaidi ya milioni 60 haiwezi kuendelea kwa kua na walipa kodi wasiozidi milioni 2,kila mtu anapaswa kuchangia maendeleo ya nchi yetu na maendeleo haya yanaletwa kwa kulipa kodi. Hivo TRA wanatakiwa kuja na mbinu rafiki na madhubuti kuhakikisha watu wote wanaostahili kulipa kodi basi wanalipa kodi stahiki.kama TRA inaweza kukusanya kodi hadi kwenye maduka ya rejareja (kwa mangi)yalipo mitaani basi pia inaweza kukusanya kodi kwa madalali waliopo mitaani.
Mfano mosi kuhakikisha kila mwenye nyumba/jengo/kiwanda/gari au mali yoyote inayouzwa kuwasilisha makato aliyomkata dalali,la sivo basi yeye mnunuzi ndio atawajibika kulipa makato hayo.
Pili kufatilia na kujiridhisha na miamala ya fedha ya kila mtu kama ni halali na imelipiwa kodi stahiki.kuhakikisha kila kipato kinachoonekana katika miamala ya kibenki,simu nk imelipa kodi stahiki.maana leo hii mtanzani anaweza kufanya miamala ya kibenki au simu bila kuulizwa chanzo cha kipato chake na kama kimelipiwa kodi.
TRA ikitaka kuongeza wigo wa kukusanya kodi basi sekta isiyo rasmi ndio mahali sahihi pa kuanzia kukusanya kodi ila kwa njia rafiki
Wamesajiliwa na qanalipia leseni.

Sema Kodi ya zuio kwenye mauziano wanayosimamia ndio haitozwi.
 
Juzi nilikua katika mishe zangu za harakati za kupambania mkate wa kila siku ambayo iliuisisha uuzaji wa nyumba. Biashara ikafanyika vizuri na mwisho wa siku dalali akaondoka na 10 milion taslim.
Tangu siku hyo nimekaa nikiwaza ni kiasi gani cha mapato serikali inapoteza kama kodi kutoka katika sekta isiyo rasmi. Licha ya nchi yetu kua na watu zaidi ya milioni 6 ila walipa kodi hawazi milioni 2 na wakati huo huo TRA imesajili walipa kodi wasiozidi milioni 5.
View attachment 3175029
Naibu waziri wa fedha mh.Hamad chande akihutubia bunge tarehe 6/9/2023 alidai sekta isiyo rasmi inakadiriwa kuajiri watu karibu milioni 27.7 ,Swale je ni wangap wanalipa kodi?na serikali imechujua hatua zipi ili kuwawezesha watu hao kulipa kodi?sheria za kodi za tanzania zinamta mtu mwenye kipato cha kuanzia 270,000/= kulipa kodi ila wanaolipa kodi kwa sasa ni wale walio katika mfumo rasmi wa ajira, walio nje ya mfumo rasmi wa ajira hawalipi kodi hata kama kipato chao kinazidi kiwango cha laki mbili na sabini. Sekta ya udalali kwa miaka ya hivi karibuni imekua sana na imekua ikiingilia na sekta kama kilimo,real estate,utalii,biashara nk ila mchango wake katika kuongeza mapato ya nchi kupitia kodi naweza kusema ni sawa na sifuri kabisa licha ya kwamba wanaingizi pesa nyingi.madalali wa nyumba,viwanja,magari wamekua wakijipatia kipato kikubwa bila ya kulipa kodi kwa serikali,kuna wakati wanachukua mpaka asilimia 10 ya malipo ya walichodalalia.Fikiria dalali anayeuza kiwanja/nyumba kariakoo anaondoka na kiasi gani cha mapato?kuna case madalali wanaondoka mpaka na 50+milioni kwa kuuza jengo moja na wala hawalipi kodi sababu wapo kwenye sekta isiyo rasmi.Kuna madalali wa mazao ambao wanafaidika kuliko wakulima.Ukirudi sekta ya uvuvi nayo wavuvi na walio kwenye mnyororo wa thmani wa uvuvi wengi wao hawalipi kodi hvo serikali kukosa mapato.
Wito wangu kwa serikali na hasa TRA watafute njia za kuingiza sekta isiyo rasmi katika ulipaji wa kodi maana uko ndipo hela nyingi ilipo.Nchi kubwa kama hii yenye watu zaidi ya milioni 60 haiwezi kuendelea kwa kua na walipa kodi wasiozidi milioni 2,kila mtu anapaswa kuchangia maendeleo ya nchi yetu na maendeleo haya yanaletwa kwa kulipa kodi. Hivo TRA wanatakiwa kuja na mbinu rafiki na madhubuti kuhakikisha watu wote wanaostahili kulipa kodi basi wanalipa kodi stahiki.kama TRA inaweza kukusanya kodi hadi kwenye maduka ya rejareja (kwa mangi)yalipo mitaani basi pia inaweza kukusanya kodi kwa madalali waliopo mitaani.
Mfano mosi kuhakikisha kila mwenye nyumba/jengo/kiwanda/gari au mali yoyote inayouzwa kuwasilisha makato aliyomkata dalali,la sivo basi yeye mnunuzi ndio atawajibika kulipa makato hayo.
Pili kufatilia na kujiridhisha na miamala ya fedha ya kila mtu kama ni halali na imelipiwa kodi stahiki.kuhakikisha kila kipato kinachoonekana katika miamala ya kibenki,simu nk imelipa kodi stahiki.maana leo hii mtanzani anaweza kufanya miamala ya kibenki au simu bila kuulizwa chanzo cha kipato chake na kama kimelipiwa kodi.
TRA ikitaka kuongeza wigo wa kukusanya kodi basi sekta isiyo rasmi ndio mahali sahihi pa kuanzia kukusanya kodi ila kwa njia rafiki

Pesa nyingi zinapotea huko huko serikalini hakuna sababu ya kuwakuda madalali nyumba moja madalali watano utawaonea tu bure
 
Kuna machinga,wauza chakula(chips,wali,choma choma ),ma-MC n.k
In short Kuna Kodi kubwa sana wanabebeshwa watu wachache kama Wafanyakzi wa serikali/taasisi rasmi pamoja na wenye kurasimisha biashara/frame.
Utitiri WA Kodi nchi hii ukijidai kufungua kiji-frame/biashara utajuta mazimaaaaa wakati hii Kodi ingetawanywa kwa serikali kuanzisha vyanzo vipya vya makusanyo.

Kariakoo nimeshuhudia watu wana meza na wanauza vibaya mno,ajabu anabanwa zaid mwenye frame tena juu ya gorofa sometimes..

Nchi hii ina safari ndefu sana
 
Juzi nilikua katika mishe zangu za harakati za kupambania mkate wa kila siku ambayo iliuisisha uuzaji wa nyumba. Biashara ikafanyika vizuri na mwisho wa siku dalali akaondoka na 10 milion taslim.
Tangu siku hyo nimekaa nikiwaza ni kiasi gani cha mapato serikali inapoteza kama kodi kutoka katika sekta isiyo rasmi. Licha ya nchi yetu kua na watu zaidi ya milioni 6 ila walipa kodi hawazi milioni 2 na wakati huo huo TRA imesajili walipa kodi wasiozidi milioni 5.
View attachment 3175029
Naibu waziri wa fedha mh.Hamad chande akihutubia bunge tarehe 6/9/2023 alidai sekta isiyo rasmi inakadiriwa kuajiri watu karibu milioni 27.7 ,Swale je ni wangap wanalipa kodi?na serikali imechujua hatua zipi ili kuwawezesha watu hao kulipa kodi?sheria za kodi za tanzania zinamta mtu mwenye kipato cha kuanzia 270,000/= kulipa kodi ila wanaolipa kodi kwa sasa ni wale walio katika mfumo rasmi wa ajira, walio nje ya mfumo rasmi wa ajira hawalipi kodi hata kama kipato chao kinazidi kiwango cha laki mbili na sabini. Sekta ya udalali kwa miaka ya hivi karibuni imekua sana na imekua ikiingilia na sekta kama kilimo,real estate,utalii,biashara nk ila mchango wake katika kuongeza mapato ya nchi kupitia kodi naweza kusema ni sawa na sifuri kabisa licha ya kwamba wanaingizi pesa nyingi.madalali wa nyumba,viwanja,magari wamekua wakijipatia kipato kikubwa bila ya kulipa kodi kwa serikali,kuna wakati wanachukua mpaka asilimia 10 ya malipo ya walichodalalia.Fikiria dalali anayeuza kiwanja/nyumba kariakoo anaondoka na kiasi gani cha mapato?kuna case madalali wanaondoka mpaka na 50+milioni kwa kuuza jengo moja na wala hawalipi kodi sababu wapo kwenye sekta isiyo rasmi.Kuna madalali wa mazao ambao wanafaidika kuliko wakulima.Ukirudi sekta ya uvuvi nayo wavuvi na walio kwenye mnyororo wa thmani wa uvuvi wengi wao hawalipi kodi hvo serikali kukosa mapato.
Wito wangu kwa serikali na hasa TRA watafute njia za kuingiza sekta isiyo rasmi katika ulipaji wa kodi maana uko ndipo hela nyingi ilipo.Nchi kubwa kama hii yenye watu zaidi ya milioni 60 haiwezi kuendelea kwa kua na walipa kodi wasiozidi milioni 2,kila mtu anapaswa kuchangia maendeleo ya nchi yetu na maendeleo haya yanaletwa kwa kulipa kodi. Hivo TRA wanatakiwa kuja na mbinu rafiki na madhubuti kuhakikisha watu wote wanaostahili kulipa kodi basi wanalipa kodi stahiki.kama TRA inaweza kukusanya kodi hadi kwenye maduka ya rejareja (kwa mangi)yalipo mitaani basi pia inaweza kukusanya kodi kwa madalali waliopo mitaani.
Mfano mosi kuhakikisha kila mwenye nyumba/jengo/kiwanda/gari au mali yoyote inayouzwa kuwasilisha makato aliyomkata dalali,la sivo basi yeye mnunuzi ndio atawajibika kulipa makato hayo.
Pili kufatilia na kujiridhisha na miamala ya fedha ya kila mtu kama ni halali na imelipiwa kodi stahiki.kuhakikisha kila kipato kinachoonekana katika miamala ya kibenki,simu nk imelipa kodi stahiki.maana leo hii mtanzani anaweza kufanya miamala ya kibenki au simu bila kuulizwa chanzo cha kipato chake na kama kimelipiwa kodi.
TRA ikitaka kuongeza wigo wa kukusanya kodi basi sekta isiyo rasmi ndio mahali sahihi pa kuanzia kukusanya kodi ila kwa njia rafiki
Hongera kwa andiko zuri la ushauri nini kifanyike hakika umeonekana una nia njema na mzalendo kweli. Ila jambo moja tu naomba nikurekebishe picha uliyoweka siyo ya Mh Naibu Waziri .
chande.jpg
 
Punguza roho mbaya mkuu acha watu wapige pesa ,hata akilipa kodi nothing changes if nothing changes


#Wajinga ndo waliwao.
 
Tatizo mapato yakiongezeka na mikopo hewa inaongezeka, WB na IMF wanatulazimisha tuchukue mikopo kwa ajili ya ‘kukuza uwezeshwaji wa watumishi katika kutoa huduma bora’ , sasa imagine mnasainishwa mkataba wa mkopo wa trillion 2 kwa ajili ya mradi kama huo, pesa haziji ila mkopo tunalipa na riba juu. Ukiuliza imekuwaje unaambiwa watumishi wameshapewa mafunzo tayari, mradi umeisha.
 
Tatizo mapato yakiongezeka na mikopo hewa inaongezeka, WB na IMF wanatulazimisha tuchukue mikopo kwa ajili ya ‘kukuza uwezeshwaji wa watumishi katika kutoa huduma bora’ , sasa imagine mnasainishwa mkataba wa mkopo wa trillion 2 kwa ajili ya mradi kama huo, pesa haziji ila mkopo tunalipa na riba juu. Ukiuliza imekuwaje unaambiwa watumishi wameshapewa mafunzo tayari, mradi umeisha.
uko sahihi mkuu eti mapato ya kodi na makusanyo yakiongezeka basi viongozi wa juu watajiongezea posho na mishahara si uliona juzi kati baada ya kunogewa na pesa za tozo za miamala chap wakapeleka sheria bungeni na wakapitisha sheria ya wake wa viongozi kupokea asilimia 60 ya mshahara wa aliye madarakani kwa ile nafasi aliyokuwa mwenza wake na mume mstaafu akilamba 80% yaani wanampita hadi aliye madarakani sahivi kwenye hicho cheo..vp nchi ikiwa na wastaafu kumi kila nafasi kuanzia Urais na makamu,CDF,IGP,PM,Spika hadi ujaji mkuu uwalipe pamoja na wenza wao jumla asilimia 140 kila mmoja na nyingine 100% aliye ofisini.! mnasemaje nchi haina hela..kwa hali hii ndio mtoa mada anataka tuwaongezee zaidi na sisi huku tukiongezwa kulipa kodi zaidi na wao huko juu watapanua goli zaidi kwa kuanzisha ulaji mpya wa vyeo na mafao..mtoa mada hana hoja apuuzwe.!
 
Serikali imejikita kwenye kuomba omba misaada na hivi karibuni kukopa zaidi sana kuhudumia anasa na miradi yenye harufu ya ubadhirifu.

Kitu kimoja Serikali haikifanyi kikamilifu tena haikifanyi kwa makusudi ni kutokusanya maduhuri au kuyachepusha ili kuwanufaisha watendaji ambao wako kuhujumu zoezi zima la ukusanyaji mapato ya Serikali.
 
Back
Top Bottom