TRA kitengo cha elimu kwa mlipa kodi kijitathmini

TRA kitengo cha elimu kwa mlipa kodi kijitathmini

pombe kali

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2014
Posts
282
Reaction score
561
Suala la kulipa kodi ni suala la kizalendo hii elimu inatakiwa iwe inawekwa kwenye mitaala ya shule zetu, mifumo yetu ya elimu imejikita zaidi kwenye kuajiriwa hivi majuzi imekuwa kama kauli mbiu ya serikali Kwamba watu wajiajiri kwani serikali haina ajira za kuwapa..inasikitisha sana inapotokea mmoja mbunifu anaamua kubuni Jambo lake kisha anajiajiri Anafikia mpaka hatua ya Kutoa ajira kwa watanzania wengine kitu ambacho serikali imeshindwa halafu Hawa watoza ushuru wanakuja kwa kuvizia kuvizia Mara wamfungie biashara yake au wamkamate na kumfungulia mashtaka ambayo ni Makubwa huwa najiuliza lengo ni kukatishana tamaa au kukwamishana kwani elimu hii ya mlipa kodi ingekuwa bure na inapatikana kiurahisi kungekuwa na haja gani ya kukimbizana na wafanyabiashara? Ukienda ofisi ya mapato kuna foleni na Huduma zisizoridhisha unaweza kushinda kutwa hapo utakuta unataka kuuliza nikitaka kufungua Duka natakiwa kuwa na vitu gani utaambiwa nenda kwa Huyu Mara Huyu, mamlaka ya mapato Mnakosa ubunifu na kututukanisha na serikali… wenzenu takukuru wameanzisha vilabu vya elimu kuanzia shule ya msingi nyie mnasubiri Mtu abuni biashara yake kisha mumvizie na kumfungulia mashtaka lengo ni nini?
 
Hawa watu Ni Kama wanajiona Miungu watu..
Ukihitaji huduma zao wanakuwa na mbuli Sana.

Wanapenda rushwa ndiyo maana wanafanya mambo ya hovyo, kwenye makadirio Ni Kama vile kukomoana.

Wajitafakari Hawa Viumbe
 
Mambo ya elimu ni mwalimu sasa hapo TRA kitengo cha elimu kwa mlipa kodi yupo mhasibu ndio anatoa elimu hawataki mchukua mwalimu wa polical science atoe elimu ya kodi kwa mlipa kodi
 
Nimeona Jana kwenye Facebook page Yao wameanza kutoa elimu ya aina za kodi kwa mizigo inayo ingizwa toka nje ya nchi
 
Kuna wengine hawajui kata mapato yanalipwa namna gani
Wao wenyewe wanahitaji elimu
Pia waweke vipeperushi kuelimisha watu kila ofisi

Bado watu hawana elimu ya kodi kabisa na wakiuliza wanaambia Lipa tu
 
Back
Top Bottom