TRA KUANZA KUWATOZA KODI WANAOFANYA BIASHARA MTANDAONI

Pastory Kimaryo

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2018
Posts
967
Reaction score
668
> Mamlaka hiyo imesema inatambua uwepo wa Watanzania wanaofanya biashara kupitia Mitandao ya Kijamii hivyo wote watakiwa kujitokeza ili wapewe namba ya mlipa kodi(TIN)
 


Chanzo: Ukurasa wa Twitter - Swahili Times

My Take
- Je ni vigezo vipi hivyo?
- Kwa anayejua atusaidie
 
Mbona kama jamaa wanaacha tena maswali mengine.

Biashara za mtandaoni zipo za aina nyingi lakini pia kuna ambao wanafanya biashara ya kuuza physical product lakini pia ni walipa kodi ila mitandao ni kwa ajili ya kujitangaza.

Na hiyo pia inakaaje?

Na pia sifa za mlipa kodi ni zipi maana kuna biashara ambazo zinahusisha digital products(eg ebooks) ambazo unaweza kuanza na zero capital.

Kwa huyo kwa mtu ambaye hatokuwa na uwezo wa kulipa kodi mwanzoni(hasa digital product) hatoruhusiwa kufanya biashara mtandaoni au akifanya atakuwa amekiuka sheria?

Dah hii nchi bhana. Niliona mtandao kama mbadala wa kusaidia watu wasiokuwa na mtaji ila sasa naona wavurugaji wameingia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…