TRA, kufungia biashara endelevu ni mbinu ya kizamani

TRA, kufungia biashara endelevu ni mbinu ya kizamani

Congo

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2008
Posts
2,081
Reaction score
2,325
Nawaasa TRA kuwa kufungia biashara endelevu kwa kisa cha kukusanya malimbikizo yakodi ni mbinu ya kizamani. Badilikeni. Mna wahasibu wengi tu. Kama mnaidai kampuni na bado inaendelea na biashara pelekeni mhasibu wenu aisimamie ili fedha zinazoingia zitumike kulipa kodi inayodaiwa. Wakati huohuo kamouni itakuwa inaendelea na shughuli zake. Mbinu hii hutumiwa pia na mabenki yanapokuwa yanadai marejesho ya mikopo kwa makampuni ambayo hayajafilisika. Itumieni.
 
Ni mbinu nzuri..changamoto zipo kwa pande mbili (Kwa haraka haraka) aidha wadaiwa wamezoea kuwapa kitu kidogo watumishi na baadhi yao hawaambiliki..lakini mbinu ya kufungia biashara hua ni suluhisho la mwisho baada ya maonyo kadhaa!
Deni ni kama usingizi..usipolala utaulipa tu!

Niliwahi shuhudia wakifungia mahali na nilikua sehemu ya wanahabari ilikua scenario mbaya sana hasa kwa wafanyakazi ambao walikua hawana taarifa na baadhi yao wakikosa hata nauli ya kurejea majumbani!
 
Back
Top Bottom