TRA: Kutumia "plate number" ambazo hazijatolewa na mamlaka za Serikali au TRA ni kosa kisheria

TRA: Kutumia "plate number" ambazo hazijatolewa na mamlaka za Serikali au TRA ni kosa kisheria

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema imebaini uwepo wa magari barabarani yaliyobandikwa na kutumia namba ambazo hazijatolewa na TRA ama Taasisi nyingine za Serikali ambazo zimepewa jukumu hilo kisheria.

“Aidha, kumekuwepo na matumizi ya vibati vya namba vyenye rangi zisizotambulika kisheria vinavyowekwa mbele na nyuma ya vyombo vya moto (Plate number)”

“Hivyo, Wamiliki wa vyombo vya moto na umma kwa jumla wanatangaziwa kwamba, utengenezaji na matumizi ya vibati hivyo ni kosa kisheria kama inavyoelezwa kwenye Kifungu cha 8 cha Sheria ya Usalama Barabarani (The Road Traffic Act, 1973)”

“Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote anayekiuka sheria hii ikiwa ni pamoja na kutaifisha chombo cha moto husika”

1665058675923.png

 
Wazee wa kuuza gari namba E. Gari inatembelewa na chasis number kwa miezi na miezi. Akipatikana mteja ndio inasajiliwa.

Trend hii ilianza rasmi kuelekea mwishoni mwa namba D.
 
Naona Hata plate no. Za Gauteng Kwny Audi,bimmer zinatamba sana hapa mjini.

Na zina Muda mrefu kuliko Muda wa Kwny kibali Cha temporary import.
Hao wazee wa kununua ma file. Utashangaa gari lina namba za Gauteng na Kwazulunatal kwa miezi halafu ghafla unalikuta lina namba C.
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema imebaini uwepo wa magari barabarani yaliyobandikwa na kutumia namba ambazo hazijatolewa na TRA ama Taasisi nyingine za Serikali ambazo zimepewa jukumu hilo kisheria.

“Aidha, kumekuwepo na matumizi ya vibati vya namba vyenye rangi zisizotambulika kisheria vinavyowekwa mbele na nyuma ya vyombo vya moto (Plate number)”

“Hivyo, Wamiliki wa vyombo vya moto na umma kwa jumla wanatangaziwa kwamba, utengenezaji na matumizi ya vibati hivyo ni kosa kisheria kama inavyoelezwa kwenye Kifungu cha 8 cha Sheria ya Usalama Barabarani (The Road Traffic Act, 1973)”

“Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote anayekiuka sheria hii ikiwa ni pamoja na kutaifisha chombo cha moto husika”

Wapo wengine wenzao na hawa
1666881117873.png

Namba zao zinaanza na JU
 
Back
Top Bottom