Deus F Mallya
JF-Expert Member
- Jul 28, 2011
- 705
- 441
TRA kama taasisi ya serikali ya kukusanya mapato inapaswa kujua kuwa kupandisha kodi hovyo ni kuchelewesha maendeleo ya Taifa.
Pamoja na hayo, wafanyabiashara ndio watu walio Kwenye hatari kubwa zaidi ya kuanguka kibiashara (kupata hasara ) au kuingia kwenye migogoro ya kimkataba na wateja.
Kitengo cha kukusanya kodi Bandarini kwa maksudi jana kimetoa orodha mpya ya makadirio ya kodi za kulipwa kwa Magari yanayoingia nchini kutoka Japan. Mnafanya hivyo bila alert yoyote (japo hii si mara ya kwanza ) bila kujua mikataba yetu na Wateja ikoje. Ni ajabu kuongeza kodi kutoka 3.6 hadi 6.3 karibu 90%!.
Inawezekana mnafanya haya mkijua kuwa mna lengo zuri la kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam au kuongeza pato la Taifa, lakini kumbukeni bila serikali kuhakikisha kuwa inauza zaidi nje kuliko kuingiza bidhaa ndani hata mkipandisha kodi kwa lengo la kuzuia bidhaa kuingia ni bure Kiuchumi.
Nimeandika logic ya kiuchumi leo na kuikabidhi kwa TRA. Naamini mtazingatia mapendekezo yangu.
Deus.
Pamoja na hayo, wafanyabiashara ndio watu walio Kwenye hatari kubwa zaidi ya kuanguka kibiashara (kupata hasara ) au kuingia kwenye migogoro ya kimkataba na wateja.
Kitengo cha kukusanya kodi Bandarini kwa maksudi jana kimetoa orodha mpya ya makadirio ya kodi za kulipwa kwa Magari yanayoingia nchini kutoka Japan. Mnafanya hivyo bila alert yoyote (japo hii si mara ya kwanza ) bila kujua mikataba yetu na Wateja ikoje. Ni ajabu kuongeza kodi kutoka 3.6 hadi 6.3 karibu 90%!.
Inawezekana mnafanya haya mkijua kuwa mna lengo zuri la kupunguza msongamano jijini Dar es Salaam au kuongeza pato la Taifa, lakini kumbukeni bila serikali kuhakikisha kuwa inauza zaidi nje kuliko kuingiza bidhaa ndani hata mkipandisha kodi kwa lengo la kuzuia bidhaa kuingia ni bure Kiuchumi.
Nimeandika logic ya kiuchumi leo na kuikabidhi kwa TRA. Naamini mtazingatia mapendekezo yangu.
Deus.