Tra na mtindo wa kufunga kufuli katika vibanda vya biashara ndogo ndogo:-

Tra na mtindo wa kufunga kufuli katika vibanda vya biashara ndogo ndogo:-

kamkoda

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2012
Posts
396
Reaction score
71
Wana JF,

Nimekuwa nikipata taabu kidogo na kadhia ya TRA wakati wanapokuja na mdali wao kufunga vibanda kwa ajili ya kukusanya Tzs.60,000/= za kodi na pamoja na faini ambayo ni Tzs. 35,000/= zote hulipiwa benki. Tatizo langu kiufundi ni kwamba biashara hizi ni ndogo ndogo na kimfumo kodi inatakiwa kulipwa mara baada ya kufunga hesabu za fedha kwa ufahamu wangu.

Kitendo kinachonishangaza ni kwamba hata kabla mwaka husika wa fedha haujaisha wao wameshakusanya kodi yao sijui hapa wanatumia vigezo gani hasa nazungumzia pia biashara za boda boda, bajaj ama taxi. Najaribu kufanya ulinganifu na makampuni makubwa ambayo sitapenda kuyataja hapa ambayo ukiondoa PAYE na NSSF wanaweza wasilipe kodi kabisa kwa sababu ya hasara katika biashara!!!! Kama wapo humu watuambie wanatumia fomula gani kupanga kodi ya vibanda bila kuangalia jiografia ya mji ama wilaya ama kitongoji pia.

Kitendo cha kufunga makufuli katika kibanda cha mtu mpaka kodi na faini ilipwe kabla ya mwaka wa fedha wa mfanyabiashara husika kuisha je ni halali ki sheria? kama wanasheria wamo humu watupe mawe ili turuke nao mahakamani tulambe fweza za madai wametufika kooni hawa, kufunga kibanda cha mtu si jinai? PASIPO AMRI YA MAHAKAMA....hapa ninaomba ushauri....!!!
 
Sikwepi kodi nalipa kodi kwa mapato ya shilingi ngapi kwa mwaka? Lazima ujue kanuni za kodi...
 
Sikwepi kodi nalipa kodi kwa mapato ya shilingi ngapi kwa mwaka? Lazima ujue kanuni za kodi...

Mkuu uwe unaenda tra kukadiriwa kodi kila mwaka, vinginevyo watakusumbua tu na huna pa kusikilizwa kwani wanafanya hivyo kwa mujibu wa sheria. Ukitaka amani ya biashara yako uwe na leseni na pia ulipe kodi tra
 
Wanafanya hivyo kwa sheria ipi? ufafanuzi tafadhali!!!
 
Wanafanya hivyo kwa sheria ipi? ufafanuzi tafadhali!!!

inaelekea rafiki umekuwa ukifanya biashara bila kulipa kodi, hakuna kodi inayolipwa baada ya kufunga hesabu! Kila mfanyabiashara lazima akadirie mapato yake kila mwanzo wa mwaka kabla ya siku ya mwisho ya kikazi ya mwezi wa tatu, na anapokadiria mapato yake kwa kishirikiana na maofisa wa tra anatakiwa alipe kodi ile kwa awamu nne(kila siku/kabla ya siku ya mwisho ya mwezi wa tatu)
kama wamefunga kofuli kibanda chako maana yake ni kwamba hujalipa kodi yako kwa mwaka 2013 awamu ya kwanza ambayo deadline ilikuwa tar 31/03/ au siku ya mwisho ya kazi ya mwezi machi.Maelezo yangu haya ni kwa mhtasari wa sheria ya kodi za ndani (income tax Act ya mwaka 2004) kuanzia sehemu ya 80-113 ambazo zinaelezea ukadiriaji, utaratibu na namna ya kulipa kodi za ndani pamoja na adhabu kwa wasiolipa/wanaokiuka sheria ya kodi za ndani.
Tulipe kodi tujitegemee!
 
Back
Top Bottom