TRA punguzeni hekaheka zisizo na msingi kwa wafanya biashara, fanyeni integration ya mfumo wenu na wa NIDA ili mteja apate nambari ya NIDA papohapo

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
TRA sijui niseme wamekosa ubunifu ktk kutoa huduma zao au wapowapo tu kutumia nguvu ktk kutimiza majukumu yao?

Ili uweze kupata nambari ya mlipa kodi TIN nilazima uwe na na kitambulisho cha NIDA,ambao nao wapowapo tu kama msumari nilazima wagongwe ndio waendee,mtu akienda kuomba TIN na hana NIDA anaambiwa akatafute NIDA ambayo inaweza mchukua mpaka miezi 7 hajapatiwa na kwa wakati huo huo wanaendelea kumfuatilia ktk biashara yake kiasi kwamba anaamua kufunga biashara,je hamuoni kama mna athiri biashara Za watu.

TRA fanyeni integration ya mifumo yenu ya usajiri wawalipa kodi na mfumo wa NIDA,na katika kila ofisi ya TRA awepo afisa wa NIDA au mtumishi wenu aliyepewa mafunzo na NIDA namna ya kufanya usajiri,ili Mtulo akija kuomba TIN na hana kitambulisho asajiriwe hapo hapo na apate namba ya NIDA hapo hapo siku hiyohiyo pamoja na TIN yake NIDA aende kufuata kitambulisho tu.

Sambamba na hilo mfumo wa NIDA ufanyiwe marekebisho use na uwezo Wakutengeneza nambari Za utambulisha online kupitia TRA.

TRA kitengo chenu cha IT kiwe na ubunifu basi kuna mambo ni mepesi tu
 
Acha uongo TIN namba sio lazima kuwa na NIDA unaweza kuwa na kitambulisho cha mpiga kura au barua ya serikali za mitaa au pasport ya kusafiria ukapata TIN, huna namba ya kitambulisho cha Taifa chukua barua ya utambulisho serikali za mitaa unapata TIN shida mmejaa uongo uongo
 
Acha upimbi paka wewe ,kati ya hivyo ulivyo taja kipi ni upatikanaji wake ni rafiki zaidi ,hukujifunza faida za ufupisho wa maneno?,
 
Acha upimbi paka wewe ,kati ya hivyo ulivyo taja kipi ni upatikanaji wake ni rafiki zaidi ,hukujifunza faida za ufupisho wa maneno?,
wewe ndio pimbi kuleta uongo kwamba kama huna namba ya nida hupati TIN namba, wakati ukichukua barua ya utambulisho kutoka serikali za mtaa tu unapata TIN, iyo namba ya nida unaifiatilia miezi saba yote ya nini lete visingizio vingne we kachukue barua ya serikali za mitaa tena haraka tu chap unapata TIN, ukadiriwe ulipe kodi acha longo longo sisizo na maana lipa kodi kwa maendeleo ya Taifa

Toka lini mtu anaenda TRA hana nida anaambiwa akatafute namba ya NIDA kama sio uongo na kuchafua tasisi ya watu, huna nida chukua barua ya utambulisho serikali za mitaa
 
Nchi yetu hii bado sana. Upo uwezekano wa kitambulisho cha uraia kuwa na taarifa zote ikiwemo kitambulisho cha kura, leseni yz udereva, cheti cha kuzaliwa, kadi za benki etc. Hakuna tatizo lolote kwa sababu taarifa husika zitasomwa kwenye kompyuta au POS
 
mbona siyo lazima kuwa na NIDA kama nida wamekusajili na namba unayo ingia mtandao wa hawa jamaa zetu wa mapato tra unajisajili mwenyewe siyo lazima mpaka uwe na kadi ile. Ulizia namba yako ya nida inatosha . tena wajanja wasije wakakupiga hiyo tin ni bure unajisajili mwenyewe kwenye tovuti yao tra ukishindwa nistue nikuelekeze maana nami nilipewa elimu wakati nasajili cha dogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…