TRA tafadhali angakieni upya huu utaratibu wa kitambulisho cha machinga

TRA tafadhali angakieni upya huu utaratibu wa kitambulisho cha machinga

EMMANUEL JASIRI

Senior Member
Joined
Feb 2, 2015
Posts
150
Reaction score
84
Mimi ni mjasiliamali mdogo mdogo,nayajua maumivu tunayo yapitia sisi wajasilia mali wadogo.Natambua uwepo wa wafanya biashara weye mitaji mikubwa ambao wamejigeuza kuwa machinga kwa lengo la kukwepa ulipaji kodi.

Hata hivyo wapo wengi ambo ni machinga halisi,pia wapo pia ambao hapo awali walikuwa na mitaji mikubwa lakini kwa sasa wamefilisika na kuamua kuchukua vitambulisho vya umachinga na kisha kuanza kudunduliza upya.

Nimesoma tangazo la TRA linalo sema,hatapewa kitambulisho cha umachinga mtu ambaye amekuwa na TIN Number,sasa kama mtu ameshuka mtaji toka milioni kadhaa na kuwa na mtaji wa elfu ishirini tu,japokuwa hapo awali amewahi miliki TIN na sasa kashuka,nasi tunajua maisha yana changamoto nyingi huyu anawekwa wapi?

Pia tangazo la vigezo vya kupata kitambulisho cha machinga linasema kuwa,machinga ni yule ambaye mauzo yake hayazidi 11,000 TTRA mauzo kwa kawaida yanaweza kushuka sana au kupanda sana,kuna siku ambapo inakuwa kama ni siku ya bahati kwa machinga maana anaweza akatokea mtu mmoja t akafanya manunuzi makubwa hata ya elfu hamsini,nanyi mnasema kigezo ni tshs 11,000 tu,je hamuoni mna watengeneza wajasilia mali mazingira ya kuwadanganya na kuanza kukimbizana.
Naamini nyie TRA mpo ofisini tunao itambua hali ya huku ni sisi,hivyo msiweke kanuni na sheria kwa mitazamo yenu,nacho kiona mimi kwa hivyo vigezo hamtusaidii ila mna tukwamisha.

Sasa niambie kuwa mnataka mauzo yawe 11000 tu,na je mmefikiria katika faida yake ni kiasi gani,maana hapo kuna mtaji na faida ,na bado,hivi kumtakia mtu kuuza tsh 11000 tu ili umpe kitambulisho mna maanisha nini,maana hicho ni kipato kidogo sana mnacho mkadiria mtu apate,ina maana akijiongeza akapata zaidi maana yake mnataka kumbana,hivi kweli ungekuwa ni wewe afisa ungeweza kumudu gharama za maisha kwa mauzo ya 11000 kwa siku?

Ushauri wangu mauzo tsh laki moja kushuka chini mngewatambua kama machinga,naamini katika laki moja kwa uzoefu wangu faida ni elfu kumi mpaka elfu ishirini,mtu wa kipato hicho bado yupo chini sana kiuchumi.

Mtu anaye uza tsh 11000 kwa siku ni mtu ambaye yuko hoi ,ana hitaji kusamehewa tu,maana hata mlo kwa siku inawezekana ni mmoja tu.

Kwa uzoefu wangu mtu anaye uza tshs 11000 kwa siku,maana anapata faida ya tshs 2000 hadi 3000
TRA Mpo ofisini,ugumu wa huku mtaani sisi ndio tunao ujue,tafadhali angalieni kwa makini taratibu zenu,vinginevyo mna tuumiza.
 
Mimi ni mjasiliamali mdogo
mdogo,nayajua maumivu tunayo yapitia sisi wajasilia mali wadogo.Natambua uwepo wa wafanya biashara weye mitaji mikubwa ambao wamejigeuza kuwa machinga kwa lengo la kukwepa ulipaji kodi.
Hata hivyo wapo wengi ambo ni machinga halisi,pia wapo pia ambao hapo awali walikuwa na mitaji mikubwa lakini kwa sasa wamefilisika na kuamua kuchukua vitambulisho vya umachinga na kisha kuanza kudunduliza upya.
Nimesoma tangazo la TRA linalo sema,hatapewa kitambulisho cha umachinga mtu ambaye amekuwa na TIN Number,sasa kama mtu ameshuka mtaji toka milioni kadhaa na kuwa na mtaji wa elfu ishirini tu,japokuwa hapo awali amewahi miliki TIN na sasa kashuka,nasi tunajua maisha yana changamoto nyingi huyu anawekwa wapi?
Pia tangazo la vigezo vya kupata kitambulisho cha machinga linasema kuwa,machinga ni yule ambaye mauzo yake hayazidi 11,000 TTRA mauzo kwa kawaida yanaweza kushuka sana au kupanda sana,kuna siku ambapo inakuwa kama ni siku ya bahati kwa machinga maana anaweza akatokea mtu mmoja t akafanya manunuzi makubwa hata ya elfu hamsini,nanyi mnasema kigezo ni tshs 11,000 tu,je hamuoni mna watengeneza wajasilia mali mazingira ya kuwadanganya na kuanza kukimbizana.
Naamini nyie TRA mpo ofisini tunao itambua hali ya huku ni sisi,hivyo msiweke kanuni na sheria kwa mitazamo yenu,nacho kiona mimi kwa hivyo vigezo hamtusaidii ila mna tukwamisha.
Sasa niambie kuwa mnataka mauzo yawe 11000 tu,na je mmefikiria katika faida yake ni kiasi gani,maana hapo kuna mtaji na faida ,na bado,hivi kumtakia mtu kuuza tsh 11000 tu ili umpe kitambulisho mna maanisha nini,maana hicho ni kipato kidogo sana mnacho mkadiria mtu apate,ina maana akijiongeza akapata zaidi maana yake mnataka kumbana,hivi kweli ungekuwa ni wewe afisa ungeweza kumudu gharama za maisha kwa mauzo ya 11000 kwa siku?
Ushauri wangu mauzo tsh laki moja kushuka chini mngewatambua kama machinga,naamini katika laki moja kwa uzoefu wangu faida ni elfu kumi mpaka elfu ishirini,mtu wa kipato hicho bado yupo chini sana kiuchumi.
Mtu anaye uza tsh 11000 kwa siku ni mtu ambaye yuko hoi ,ana hitaji kusamehewa tu,maana hata mlo kwa siku inawezekana ni mmoja tu.
Kwa uzoefu wangu mtu anaye uza tshs 11000 kwa siku,maana anapata faida ya tshs 2000 hadi 3000
TRA Mpo ofisini,ugumu wa huku mtaani sisi ndio tunao ujue,tafadhali angalieni kwa makini taratibu zenu,vinginevyo mna tuumiza.
TRA wanapandisha mabega naona hawaelewi hawa jamaa mama anataka nini?
 
Hiv utaratibu wa kupata upoje

Yaan unaanzia ofisi gani na unamalizia wapi..?
 
Wamachinga lipeni kodi kwa maendeleo ya nchi. Acheni kukimbilia kwenye hivyo vitambulisho vya elfu 20!

Hiyo ni kodi ndogo sana kwa mwaka ukilinganisha na makundi mengine ya walipa kodi, mfano wafanyakazi.
 
Kumbe machinga mauzo yake hayazidi elfu 11 kwa siku? Basi Bongo hamna machinga.
 
Kumbe machinga mauzo yake hayazidi elfu 11 kwa siku? Basi Bongo hamna machinga.
Si ndio hapo. Hiyo biashara ya 11,000 kwa siku si biashara kichaa? Tena nadhani hiyo 11 ni mauzo ghafi...ukitoa cost hapo inabaki faida gani? Hebu TRA wawe serious aisee
 
Mimi naona tufute kabisa kundi la wamachinga. Itambulike tu kuwa ukiamua kufanya biashara lazima utoe risiti na ulipe kodi. Kodi ilipwe kwa kuzingatia faida anayopata mfanyabiashara na kodi hiyo iwe fair.

Kwa hiyo machinga na Bakhresa wote wasajiliwe kama wafanyabiashara period.
 
Mimi naona tufute kabisa kundi la wamachinga. Itambulike tu kuwa ukiamua kufanya biashara lazima utoe risiti na ulipe kodi. Kodi ilipwe kwa kuzingatia faida anayopata mfanyabiashara na kodi hiyo iwe fair.

Kwa hiyo machinga na Bakhresa wote wasajiliwe kama wafanyabiashara period.
Watu wanaotembeza biashara yao barabarani...au wachoma mahindi ambao wanahama na majimo yao kila siku TRA wanawapata wapi? EFD machine ananunuaje kwanza?
 
Pale Kariakoo wanaoitwa machinga wanapata mpaka faida ya 40000 kwa siku sasa wataondolewa?
 
Back
Top Bottom