Kampuni ya Uwakala wa Forodha ili ipate leseni ya kufanya kazi nchini Tanzania ni lazima ifanye mtihani wa Uwakala wa Forodha Tanzania unaotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kitengo cha Ushuru na Forodha ( Custom and Excise). Tarehe ya mtihani itatangazwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania, kwa watu na makampuni yote yaliyopatiwa usajili wa awali, baada ya kufaulu mtihani wa Uwakala wa Forodha, kampuni husika itapatiwa leseni ya uwakala wa forodha, ila Kabla ya kupatiwa Leseni ya uwakala wa forodha kampuni zote zinatakiwa kuwa na mtaji (Capital) isiyopungua milion 50 /= na pia kuwa na Banki guarantee isiyopungua milioni 100 /=. hivyo vyote ni muhimu hasa kwa mizigo ya Transit inayotakiwa kuwa na Bond ili kuzuia upotevu wa mizigo kunakoweza kusababishwa na wakala wa forodha husika.
Pia kuna vitu vingine ambavyo muombaji wa leseni ya uwakala wa forodha atatakiwa kuwa navyo kama Cheti kutoka Sumatra, Barua ya uthibitisho wa usajili kutoka Brela, wafanyakazi kusajiliwa mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Kuwa na Ofisi inayotambulika na mamlaka husika.
Hayo ndio mambo ya Msingi ya kuzingatia