Torra Siabba
JF-Expert Member
- Jul 24, 2016
- 243
- 287
Ndugu Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani hapa Tabora, Mh Magayane sisi wakazi wa hapa tunakuomba udhibiti suala la msongamano wa magari eneo la Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani hususan jioni maana hakuna utaratibu maalumu kila basi linashusha njia kuu jambo linalisababisha msongamano.
Ikifika Saa 2 Usiku na kuendelea, tunashuhudia Mabasi yanashusha abiria barabarani, hali hiyo inachangia msongamano kama vile kuna msafara unapishwa, kumbe wapi.
Mabasi mengi yanaziba njia na kusababisha usumbufu kwa wapita njia wa kawaida maana msongamano unakuwa mkubwa bila sababu, hivyo hii changamoto kusema ukweli itatuliwe kwa uharaka maana haijaanza leo wala kesho.
Tusaidieni maana muda huo askari wanakuwa maeneo mengine kwanini pale stendi wale waliomo ndani wasisaidie kwenye hili?
Ikifika Saa 2 Usiku na kuendelea, tunashuhudia Mabasi yanashusha abiria barabarani, hali hiyo inachangia msongamano kama vile kuna msafara unapishwa, kumbe wapi.
Mabasi mengi yanaziba njia na kusababisha usumbufu kwa wapita njia wa kawaida maana msongamano unakuwa mkubwa bila sababu, hivyo hii changamoto kusema ukweli itatuliwe kwa uharaka maana haijaanza leo wala kesho.
Tusaidieni maana muda huo askari wanakuwa maeneo mengine kwanini pale stendi wale waliomo ndani wasisaidie kwenye hili?