''tragedic comedy'' wako watakaocheka wako watakaolia

''tragedic comedy'' wako watakaocheka wako watakaolia

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
''TRAGIC COMEDY'' WAKO WATAKAOCHEKA WAKO WATAKAOLIA

Kwa umri wangu huu baada ya kula chakula cha mchana kitanda kinaniita kujipumzisha kidogo.

Lakini kama kawaida kutakuwa na hiki au kile mtu unataka uchungulie katika simu na ikibidi nifungue mtambo ikibidi kwani huko ndiko Maktaba ilipo.

Nasikia, ‘’Hodi, hodi, hodi.’’

Nafungua nawaona watu wa stesheni moja maarufu sana wako mlangoni pangu wananiambia wamekuja kunihoji kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka wa 1964.

Nikawakaribisha ndani.

Si wageni hawa vijana wameshafika kwangu mara kadhaa kwa kunihoji.

Wananiambia kuwa wangependa wanihoji kuhusu sherehe za mapinduzi.
Akili yangu inajisemeza yenyewe kuhusu hili neno, ‘’sherehe.’’

Sherehe ndani ya msiba.

Mimi kwa haraka sana nikawaambia kuwa suala la mapinduzi ya Zanzibar ni historia inayotakiwa ichukuliwe kwa tahadhari kubwa sana kwani kwangu mimi na kwa wengine si suala la kuchukuliwa kwa sherehe kama wanavyotaka kunihoji.

Nikawaambia kuwa mapinduzi kwa baadhi ya watu huwakumbusha vifo vya ndugu zao siku ya mapinduzi na baada ya mapinduzi.

Historia ya mapinduzi si jambo jepesi kama wanavyolichukulia.

Wale vijana hawakutegemea maneno yale kutoka kwangu.
Nikaona sura zao zina mchanganyiko wa kushangaa na mashtuko.

Nikawaambia, ‘’Mimi baba yangu alikuwa na rafiki zake wawili, Jaha Ubwa na Abdulaziz Twala wanamapinduzi na wana ASP kindakindaki.

Hawa waliuliwa baada ya mapinduzi na baba yangu alikuwa na picha walipiga wote watatu picha hii baba alikuwa ameitundika ukutani nyumbani kwetu.

Baada ya kuuliwa hawa rafiki zake wawili picha ile aliitungua pale pengine kwa uchungu kuwa hakuweza kuitazama ile picha kwa majonzi yaliyokuwa moyoni kwake na pia pengine kwa hofu ya yeye kuogopa asije kuhusishwa na wale watu ‘’wabaya,’’ ambao kwa ubaya wao hukumu yao ilikuwa ni kuuliwa.’’

Niliwaonyesha hawa vijana kitabu cha Dr. Haritht Ghassany, ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,’’ nikawauliza kama wamepata kusoma kitabu hiki.

Hata kukiona au kukisikia ilikuwa bado.

Niliwaeleza kuwa kitabu kile kina maneno ya yale yaliyotokea Zanzibar wakati wa mapinduzi kutoka kwenye vinywa vya wahusika wenyewe na wengi wao wametangulia mbele ya haki wakiwa na majuto kwa yale ambayo mikono yao imetanguliza.

Nikawaambia wao kama waandishi wajitahidi sana kusoma.

Juu ya haya yote tulifanya kipindi kifupi kuliko kawaida cha mapinduzi lakini yale maswali ambayo naamini walikusudia kuniuliza hawakuniuliza.

Hawakuweza tena kuwa na moyo wa kuniuliza nilikuwa nimewafanulia pazia kuona upande mwingine wa jukwaa.

Picha ya kwanza ni Mohamed Omari Mkwawa, John Okello na picha ya mwisho askari wa mapinduzi akiwa katika ulinzi wakati wa mapinduzi.
 
Hata ukijificha vipi na uongo mwingi, kila mtu anajuwa wewe ni nani. Ila ungekuwa mkweli ungeonyesha pande zote za shillingi. Upande mzuri na upande mbaya.

Ni kweli mapinduzi ya Zanzibar au mapinduzi ya nchi yoyote yana mazuri na mabaya. Mabaya ni yale ya watu wengi kupoteza uhai. Kama ingewezekana ingekuwa jambo jema mapinduzi kutokea bila vifo kwa upande wowote.

Kwa upande mwingine mapinduzi huleta uhuru kwa wale ambao hutawaliwa kwa maguvu, kama vile sultani alivyokuwa anatawala Zanzibar na kuwafanya weusi kuwa watumwa nyumbani kwao.

Ila sihangai mleta maada kuangalia hili kwa upande mmoja. Huyu ni kinara wa malalamiko mengi ambapo huwa anatetea uarabu, mara uislamu, mara Nyerere kawasahau waleta uhuru halisia na mambo chungu mbovu. Sasa hapa kaja kwa kujificha ili tusimbaini ni nani.
 
Negative perception, mpk inashangaza… atleast ungenarrate hta gettysburg address ya Abraham Lyncoln
 
Hata ukijificha vipi na uongo mwingi, kila mtu anajuwa wewe ni nani. Ila ungekuwa mkweli ungeonyesha pande zote za shillingi. Upande mzuri na upande mbaya. Ni kweli mapinduzi ya Zanzibar au mapinduzi ya nchi yoyote yana mazuri na mabaya. Mabaya ni yale ya watu wengi kupoteza uhai. Kama ingewezekana ingekuwa jambo jema mapinduzi kutokea bila vifo kwa upande wowote. Kwa upande mwingine mapinduzi huleta uhuru kwa wale ambao hutawaliwa kwa maguvu, kama vile sultani alivyokuwa anatawala Zanzibar na kuwafanya weusi kuwa watumwa nyumbani kwao.

Ila sihangai mleta maada kuangalia hili kwa upande mmoja. Huyu ni kinara wa malalamiko mengi ambapo huwa anatetea uarabu, mara uislamu, mara Nyerere kawasahau waleta uhuru halisia na mambo chungu mbovu. Sasa hapa kaja kwa kujificha ili tusimbaini ni nani.
Ksk,
Sijapata kujificha.

Nyote hapa barzani mnanijua kwa jina, sura na sauti.

Sijapata kusema uongo.
Naandika lile ninalolijua.

Ikiwa unaona mimi nimeeleza ya upande mmoja hii ni nafasi yako nawe kueleza upande ule mwingine.

Kuhusu kuwa natetea Uarabu na Uislam labda nikuulize kwani hairuhusiwi?

Kuhusu Nyerere kuwasahau wapigania uhuru je Mwalimu amepata kuwaenzi wale waliompokea Dar es Salaam na kumtia katika siasa za TAA na kumjulisha kwa watu wa mjini?

Ulipata kujua kabla sijaeleza mimi kuwa kadi ya Ally Sykes ya TANU ni no. 2 na ya kaka yake Abdul Sykes ni no. 3 na kadi ya Nyerere ni no. 1 na aliandikiwa na Ally Sykes?

Je ulikuwa unajua kuwa kadi 1000 za kwanza za TANU alinunua Ally Sykes?

Historia hii ulipatapo kuisikia ikifundishwa popote?
 
Hivi kuna watu bado wanafuatiria huu upupu wa huyu mzee ambaye mawazo yake zote yapo kwa bwana zake waaarabu..kwa mgongo wa dini.

Huyu mzee wa kupuuzwa kama wapuuzi wengine wanayopaswa kupuuzwa.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee Mohamed yale yalikuwa mapinduzi maana serikali ya Shamte iling'olewa....kuna wanaoita ule ulikuwa 'uvamizi' kutoka Tanganyika wakishirikiana na kina Hanga...hii historia ina utata mwingi na watawala hawataki kuiweka wazi.
 
Negative perception, mpk inashangaza… atleast ungenarrate hta gettysburg address ya Abraham Lyncoln
Lam...
Ni ''Lincoln'' si ''Lyncoln.''

1641963226423.png

Lincoln Memorial, Washington DC.
 
Mzee Mohamed yale yalikuwa mapinduzi maana serikali ya Shamte iling'olewa....kuna wanaoita ule ulikuwa 'uvamizi' kutoka Tanganyika wakishirikiana na kina Hanga...hii historia ina utata mwingi na watawala hawataki kuiweka wazi.
Pro...
Nilikuwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiiti kitabu chake, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

Katika kipindi kile nimejifunza mengi katika historia ya Zanzibar.
Watawala wala hawajui ila wasome kwanza kwa wale waliotafiti na kuandika.

Hapo ndipo watafahamu.

1641963814310.png

Hassan Nassor Moyo akisoma kitabu, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' 2012.
 
Mapinduzi ya Zanzibar yana mengi yaliyojiri ambayo hayawekwi wazi
 
Hivi kuna watu bado wanafuatiria huu upupu wa huyu mzee ambaye mawazo yake zote yapo kwa bwana zake waaarabu..kwa mgongo wa dini.

Huyu mzee wa kupuuzwa kama wapuuzi wengine wanayopaswa kupuuzwa.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Jiwe...
''Wanafuatilia,'' si ''Wanafuatiria.''
''Waarabu,'' si ''waaarabu,'' na unaanza na herufi kubwa, ''Waarabu.''

Nukta zinakuwa tatu, ''...''

Uniwie radhi lakini ni vyema hapa tukachukua fursa kama hizi kufunzana lugha za kistaarabu katika kuandika.

Ukishaandika ipitie kazi yako uangalie makosa ili ufanye masahihisho.

Tukitoka hapa tunaweza tukaingia katika adabu za uandishi ikiwa utapenda nikufundishe.
 
Mzee tunashukuru kwa Historia, je hao rafiki wa baba yako waliouawa waliuawa kwa sababu gani wakati wao walikuwa ni ASP? au walikuwa na asili ya kiarabu au chotara?
 
Wacha tufanye kile tunachoaminishwa sasa na hata baadae ....Kufurahi na kushangilia
 
Jiwe...
''Wanafuatilia,'' si ''Wanafuatiria.''
''Waarabu,'' si ''waaarabu,'' na unaanza na herufi kubwa, ''Waarabu.''

Nukta zinakuwa tatu, ''...''

Uniwie radhi lakini ni vyema hapa tukachukua fursa kama hizi kufunzana lugha za kistaarabu katika kuandika.

Ukishaandika ipitie kazi yako uangalie makosa ili ufanye masahihisho.
Tukitoka hapa tunaweza tukaingia katika adabu za uandishi ikiwa utapenda nikufundishe.

Na tunafanyaje kuhamasisha jamii ipende kusoma au kujisomea vitabu ili kuongeza maarifa na uelewa mzee wangu?

Kama ulivyoshuhudia mwenyewe kwenye maelezo yako vijana waandishi waliokufuata, sio tu hawajawahi kukisoma au kukishika kitabu, hawajawahi kukisikia kabisa, hiyo ni hatari.

Sishangai leo kusikia kiongozi, tena wakati mwingine wa mhimili wenye dhamana ya kutunga sheria au kusimamia sheria anafanya jambo hadharani, ambalo haliko sawa kikanuni na lipo wazi kabisa kwenye katiba ( hayo kwangu ni madhara ya kutokupenda kujisomea) haiwezekani ikawa ni ulevi wa madaraka au jeuri kwa sababu hua wanajitahidi iwezekanavyo kwa nje waonekane wanafuata taratibu. Hata kama ndani wanazivunja.
 
Huwa na tofautiana (kwenye baaddhi ya maeneo) na Mzee Mohamed Said namna anavyowasilisha historia ya Tanzania na Uislam!
Nikiamini kuwa Huwa ana viashiria vya Udini!
Nafikiri Historia ya Zanzibar na Mapinduzi Matukufu' ndio eneo ameshindwa kuonesha au kuchomekea " Udini !
Hakika Histori ya Zanzibar na Mapinduzi haijakaa sawa .Kuna mengi Yamefichwa!
Miaka ya hivi karibuni,Kuna Waandishi akiwemo.Mzee Mohaamed na Joseph Mihangwa,wameandika upande wa pili wa Mapinduzi ya Zanzibar!
Cha kushangaza Serikali haijawahi kukanusha ....Kwa maana hiyo yanayoandikwa ni kweli!
Zanzibar inahitaji maridhiano na Ukweli,la sivyo makovu haya yatendelea kudumu mioyoni mwa watu!
Bahati nzuri Wazanzibar 99%ni Waislam ,hii ni fursa kwao ya kuponya makovu hayo!
Acheni Unafiki!
 
Hivi huyu Mzee Ni muarabu?
Mcq...
"Hivi Mohamed ni Muarabu?"
"Hivi huyu mzee ni Muarabu?"

(Kwa kawaida Muarabu inaanza na herufi kubwa).

Sentensi ya kwanza imeandikwa na moyo uliotulia.

Sentensi ya pili imeandikwa na mtu moyo umejaa hasira.

Hili neno, "huyu," linaashiria shari, kejeli, kebehi na dharau.

Kipi kibaya nilichoandika?
 
Mzee tunashukuru kwa Historia, je hao rafiki wa baba yako waliouawa waliuawa kwa sababu gani wakati wao walikuwa ni ASP? au walikuwa na asili ya kiarabu au chotara?
Chinch...
Sijui kosa lao lilikuwa nini kwa kuwa hapakuwa na mahakama.
 
Back
Top Bottom