TRC sikilizeni ushauri wa huyu Mkenya Ken Macharia kuhusu ucheleweshaji kukata tiketi na ukaguzi

TRC sikilizeni ushauri wa huyu Mkenya Ken Macharia kuhusu ucheleweshaji kukata tiketi na ukaguzi

Shotocan

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2023
Posts
6,650
Reaction score
12,711
Ken Macharia ni Mkenya anayezunguka nchi mbalimbali duniani kutalii yuko Tanzania na akaona apande train ya mwenfo kasi toka Dar hadi Morogoro Kwa mara ya kwanza. Kitu alicholalamika cha Kwanza ni ucheleweshaji kukata Tiketi pale dirishani inachukua karibu dakika 10 kukata Tiketi moja.

Pili ukishakata Tiketi kuna kuchekiwa Tiketi kabla kuingia kwenye train kunachukua muda pia anasema yawezekana system hazijakaa vizuri.

Ushauri wangu binafsi Kwa TRC najua mna mfumo WA kukata Tiketi Kwa simu utangazeni Sana huo mfumo watu waujue wekeni matangazo mengi hata humu Jamii Forums,Vipindi vya tV mfano ITV kabla ya taaria ya habari watu waujue kukata Kwa simu wakafie huko.

Pili chapisheni vipeperushi kwa lugha tatu wagawieni watu wanapoingia kuwa waweza kata Tiketi wenyewe kwenye simu au mtandaoni Kwa debit card au credit card.

Mjue sasa mnaingia kimataifa mtalii awe anaweza kata Tiketi online hukohuko aliko kama ifanyikavyo kwenye ndege akifika Tanzania anakuwa tayari ana Tiketi.

Matangazo ya muhimu mno kuna siku mtazidiwa kukata Tiketi hadi train itaanza kuchelewa kuondoka na kuleta maudhi Kwa abiria.

Pili muweke sehemu ya Mpesa, Tigo pesa nk MTU akishapata kipeperushi ajaze pesa kwenye simu yake hapo halafu ajikatie mwenyewe ili muanze kuwazoeza ila Kwa wale wasioweza wakaribisheni counter na mueleze hivyo asione kama hawezi kuwa kikwazo.

Watu kujaa kulundikana Tu counter kizamani mno

Tatu mfumo wa kucheki Tiketi Kwa wanaoingia kwenye train uwe wa haraka kama ilivyo Airports.

Video Yake huyo Mkenya hii hapa

View: https://youtu.be/886LVKcMQn4?si=YfaplUhptnWBxTLg
 
HUYO KAJA KUPONDA TU.MBONA AIRPORT KUBWA UNAKATA TIKETI NA BADO UNACHUKUA MDA KUONDOKA
Sikiliza kwanza wewe hajaongelea train kuchelewa kuondoka imeondoka on time kaongelea ucheleweshaji wakati wa kukata tiketi na kuchelewesha kwenye ukaguzi tiketi Usimlishe maneno ambayo hakuongea

Usiwe na mihemuko isiyo na tija
 
Hata huko online ticket napo Kuna shida, system inataka kabla ya kukata ticket ujisajili kama mgeni au mwenyeji, lakini Kuna kipengele kuwa namba ya simu lazima iwe verified ili uweze kuendelea na malipo, kuipata hiyo verification code via sms Kuna shida!! Binafsi nimeishia hapo toka juz si kufanikiwa kupata code, bila code huwezi kuendelea na malipo
 
Hata huko online ticket napo Kuna shida, system inataka kabla ya kukata ticket ujisajili kama mgeni au mwenyeji, lakini Kuna kipengele kuwa namba ya simu lazima iwe verified ili uweze kuendelea na malipo, kuipata hiyo verification code via sms Kuna shida!! Binafsi nimeishia hapo toka juz si kufanikiwa kupata code, bila code huwezi kuendelea na malipo
Inawezekana ni shida ya mtandao. Mimi ni mara ya pili jana sijapata tabu yoyote. Code inakuja kwa wakati.
 
Hata huko online ticket napo Kuna shida, system inataka kabla ya kukata ticket ujisajili kama mgeni au mwenyeji, lakini Kuna kipengele kuwa namba ya simu lazima iwe verified ili uweze kuendelea na malipo, kuipata hiyo verification code via sms Kuna shida!! Binafsi nimeishia hapo toka juz si kufanikiwa kupata code, bila code huwezi kuendelea na malipo
Feedback nzuri Kwa wahusika
 
Mie nipo nje ya nchi, najiandikisha kwa email inagoma!!!?
 
Halafu mtu unatoka airport na mabegi 3, je utaweza kusafiri nazo na SGR?
 
Halafu umeme ulikatika watu wakaanza kushtuka. Walishighulikie Hilo suala la umeme ipo siku litaleta matatizo.
 
Yuko sahihi, kukata tiketi pale dirishani ni inachukua muda sijui wanafanya kusudi ili wakukatia ndani ya treni wawe wengi, maana muda treni kuondoka ukifika utaambiwa wasio na tiketi wapande wanaenda kukatiwa tiketi ndani ya treni.

Lakini pia watanzania tuache mambo ya kizamani, tukate tiketi mtandaoni, ni rahisi ni inaokoa muda.
 
Sikiliza kwanza wewe hajaongelea train kuchelewa kuondoka imeondoka on time kaongelea ucheleweshaji wakati wa kukata tiketi na kuchelewesha kwenye ukaguzi tiketi Usimlishe maneno ambayo hakuongea

Usiwe na mihemuko isiyo na tija
Kamanda wala husihangaike na huyu jamaa. Nilishasema kwenye andiko langu kwamba Watanzania wengi hatujui kumake a case na nikasema nitakuwa natoa mifano jinsi tulivyo poor kwa kuangalia urgument zetu humu kwenye jamii forum

Huu ndio mfano mwingine wa uwezo mdogo wa watanzania kujenga hoja, ku-make a case, ku appropriately respond to the issue under discussion. Sisi sijui elimu yetu imetuziba fikra kwa sababu ya kukalilishwa. Mtu anasoma hoja juujuu na kukurupuka kupinga . Sasa anavyopinga ndio kituko anatumia scernario tofauti kabisa na ya kwenye hoja. Yaani ni utopoo wa hali ya juu. Kibaya anajifanya yuko very much exposed kumbe anaonyesha umbumbumbu wake na mifano anayotoa tena inaongezea kuonyesha kumbe hata huko hajui kitu.

Huyu Mkenya ameongelea suala la ucheleweshaji wa tiketi , hakuona haja ya kutumia hizo dakika kama wangekuwa wamealtomate mfumo wao.halafu kaona suala la ukaguzi linafanyika locally wakati wangeweza kufastrastrack zoezi hilo. Hajaongelea suala la kuchelewa kwa treni kuondoka au masuala ya kuchelewa kufika wala ubora au uzuri au hajalinganisha na treni yao ya Kenya.

Mimi nafikiri ifike mahali sisi watanzania tunaojifanya tunajua saaaana tukubali sometimes "FEEDBACK IS A GIFT", we should start embracing feedback to improve our way of working and doing things
 
Airport sio kama treni, hii treni inabeba watu wenye haraka zao, kuna watu wanaeza kuishi pugu na Kuja kufanya kazi mjini, system ya ticket inatakiwa pia iwe ya haraka.
Unapachukuliaje Pugu!?
 
Kamanda wala husihangaike na huyu jamaa. Nilishasema kwenye andiko langu kwamba Watanzania wengi hatujui kumake a case na nikasema nitakuwa natoa mifano jinsi tulivyo poor kwa kuangalia urgument zetu humu kwenye jamii forum

Huu ndio mfano mwingine wa uwezo mdogo wa watanzania kujenga hoja, ku-make a case, ku appropriately respond to the issue under discussion. Sisi sijui elimu yetu imetuziba fikra kwa sababu ya kukalilishwa. Mtu anasoma hoja juujuu na kukurupuka kupinga . Sasa anavyopinga ndio kituko anatumia scernario tofauti kabisa na ya kwenye hoja. Yaani ni utopoo wa hali ya juu. Kibaya anajifanya yuko very much exposed kumbe anaonyesha umbumbumbu wake na mifano anayotoa tena inaongezea kuonyesha kumbe hata huko hajui kitu.

Huyu Mkenya ameongelea suala la ucheleweshaji wa tiketi , hakuona haja ya kutumia hizo dakika kama wangekuwa wamealtomate mfumo wao.halafu kaona suala la ukaguzi linafanyika locally wakati wangeweza kufastrastrack zoezi hilo. Hajaongelea suala la kuchelewa kwa treni kuondoka au masuala ya kuchelewa kufika wala ubora au uzuri au hajalinganisha na treni yao ya Kenya.

Mimi nafikiri ifike mahali sisi watanzania tunaojifanya tunajua saaaana tukubali sometimes "FEEDBACK IS A GIFT", we should start embracing feedback to improve our way of working and doing things
Kiufupi Mtanzania anauelewa mdogo sana.
 
Back
Top Bottom