TRC: Treni za SGR zilisimama maeneo matatu tofauti kutokana na hitilafu ya umeme katika Gridi ya Taifa

TRC: Treni za SGR zilisimama maeneo matatu tofauti kutokana na hitilafu ya umeme katika Gridi ya Taifa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Majira ya Asubuhi ya leo Desemba 4, 2024, iliripotiwa kuwa Treni ya Abiria ya Kisasa (SGR) iliyokuwa ikitokea Dar kuelekea Dodoma imekwama katika Stesheni ya Kilosa Mkoani Morogoro kwa kilichoelezwa kuwa ni hitilafu ya Umeme na hivyo kusababisha safari hiyo kushindwa kuendelea.

JamiiForums imezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano TRC, Fredy Mwanjala ambaye anafafanua kilichotokea:

“Treni zetu zilisimama katika maeneo matatu tofati kutokana na hitilafu ya umeme katika gridi ya Taifa, hivyo mikoa inayopata umeme kutoka katika gridi ya Taifa yote haikupata umeme ikiwemo Dar es Salaam na Morogoro.

“TANESCO wameshatoa taarifa yao kuhusu changamoto hiyo, kutokana na kuwa Treni yetu ni ya umeme na tunalishwa umeme na TANESCO ndio maana ikatokea changamoto hiyo.

“Hivyo sio shida ya Treni, kichwa wala reli, shida ni kukatika kwa umeme katika Gridi ya Taifa, tayari umeme umerejea na ilipofika Saa tano na nusu Asubuhi hii safari zimeanza zote rasmi.”
WhatsApp Image 2024-12-04 at 12.34.03_59c07fb1.jpg
Pia soma
~
Treni ya SGR kutoka Dar kwenda Dodoma yadaiwa kukwama tena baada ya Umeme kukatika Stesheni ya Kilosa
~ Shirika la Reli Tanzania (TRC) laomba radhi kutokana na kuchelewa kwa safari kulikosababishwa na changamoto zilizo nje ya uwezo wao
~ Treni ya SGR Dodoma kwenda Dar imekwama kituoni Mkata SGR station toka saa 1 jioni
 
Majira ya Asubuhi ya leo Desemba 4, 2024, iliripotiwa kuwa Treni ya Abiria ya Kisasa (SGR) iliyokuwa ikitokea Dar kuelekea Dodoma imekwama katika Stesheni ya Kilosa Mkoani Morogoro kwa kilichoelezwa kuwa ni hitilafu ya Umeme na hivyo kusababisha safari hiyo kushindwa kuendelea.

JamiiForums imezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano TRC, Fredy Mwanjala ambaye anafafanua kilichotokea:

“Treni zetu zilisimama katika maeneo matatu tofati kutokana na hitilafu ya umeme katika gridi ya Taifa, hivyo mikoa inayopata umeme kutoka katika gridi ya Taifa yote haikupata umeme ikiwemo Dar es Salaam na Morogoro.

“TANESCO wameshatoa taarifa yao kuhusu changamoto hiyo, kutokana na kuwa Treni yetu ni ya umeme na tunalishwa umeme na TANESCO ndio maana ikatokea changamoto hiyo.

“Hivyo sio shida ya Treni, kichwa wala reli, shida ni kukatika kwa umeme katika Gridi ya Taifa, tayari umeme umerejea na ilipofika Saa tano na nusu Asubuhi hii safari zimeanza zote rasmi.”

Pia soma
~
Treni ya SGR kutoka Dar kwenda Dodoma yadaiwa kukwama tena baada ya Umeme kukatika Stesheni ya Kilosa
~ Shirika la Reli Tanzania (TRC) laomba radhi kutokana na kuchelewa kwa safari kulikosababishwa na changamoto zilizo nje ya uwezo wao
~ Treni ya SGR Dodoma kwenda Dar imekwama kituoni Mkata SGR station toka saa 1 jioni
Naomba kuuliza labda hazina betri ya backup maana ni hatari namna hii na itafanya wananchi tuogope mradi mzuri kama huu. Naamini treni hii imekuwa ni kivutio na imerahisisha sana safari kwa sisi wananchi sasa kama vitu nya namna hii vikiwa vinatokea marakwa mara inaweza sababisha kuhofia kutumia.
 
Majira ya Asubuhi ya leo Desemba 4, 2024, iliripotiwa kuwa Treni ya Abiria ya Kisasa (SGR) iliyokuwa ikitokea Dar kuelekea Dodoma imekwama katika Stesheni ya Kilosa Mkoani Morogoro kwa kilichoelezwa kuwa ni hitilafu ya Umeme na hivyo kusababisha safari hiyo kushindwa kuendelea.

JamiiForums imezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano TRC, Fredy Mwanjala ambaye anafafanua kilichotokea:

“Treni zetu zilisimama katika maeneo matatu tofati kutokana na hitilafu ya umeme katika gridi ya Taifa, hivyo mikoa inayopata umeme kutoka katika gridi ya Taifa yote haikupata umeme ikiwemo Dar es Salaam na Morogoro.

“TANESCO wameshatoa taarifa yao kuhusu changamoto hiyo, kutokana na kuwa Treni yetu ni ya umeme na tunalishwa umeme na TANESCO ndio maana ikatokea changamoto hiyo.

“Hivyo sio shida ya Treni, kichwa wala reli, shida ni kukatika kwa umeme katika Gridi ya Taifa, tayari umeme umerejea na ilipofika Saa tano na nusu Asubuhi hii safari zimeanza zote rasmi.”

Pia soma
~
Treni ya SGR kutoka Dar kwenda Dodoma yadaiwa kukwama tena baada ya Umeme kukatika Stesheni ya Kilosa
~ Shirika la Reli Tanzania (TRC) laomba radhi kutokana na kuchelewa kwa safari kulikosababishwa na changamoto zilizo nje ya uwezo wao
~ Treni ya SGR Dodoma kwenda Dar imekwama kituoni Mkata SGR station toka saa 1 jioni
Huo mradi hizi nyani haziwezi kuendesha ni kupoteza fedha za ummah bure, kwani Tanesco haijui hizo vichwa havina backups za umeme au Engine mbadala ya diesel
 
Sijakuona kwenye mazishi ya Ndugulile kaka
Kaka, Mie na marehemu hatukuwa na ujamaa wowote, hivyo iliniwia ugumu kuacha shughuli zangu na kwenda msibani.
Jana nilipita pale mnadani, natokea kwenye kubangaiza, nikakuta ndio wanatoka, nami nikawasha double hazard, nikaufata ule msafara, mpaka mjimwema kwenye mataa, wao wakaongoza njia ya gezaulole, mie nikakunja ya kibada.

APUMZIKE KWA AMANI
 
Uchunguzi ufanyike kusiwe na hujuma ya kuua huu mradi. Wanaadamu ni wabinafsi mno. Siyo wote wanaoufurahia huu maradi. Kitu kingine wakati wa visibility study walijua hakika umeme wetu una shida. Wangetakiwa wawe na option B kama kuwa na backup generators.
 
Uchunguzi ufanyike kusiwe na hujuma ya kuua huu mradi. Wanaadamu ni wabinafsi mno. Siyo wote wanaoufurahia huu maradi. Kitu kingine wakati wa visibility study walijua hakika umeme wetu una shida. Wangetakiwa wawe na option B kama kuwa na backup generators.
tungeanza na uwajibikaji kwa vitu vya uzembe tungekua tunasonga, maana kama hapo anayetakiwa kufanya uchunguzi huwenda akawa anatakiwa kuwajibika katika incident fulani inakua ngumu
 
Hili lilitolewa tahadhali kabla hata mradi wa ujenzi wa reli yenyewe haujaanza.
 
Back
Top Bottom