Trector aina ya lovol

Trector aina ya lovol

Nyangabo2022

Senior Member
Joined
Nov 13, 2022
Posts
126
Reaction score
195
Wanajukwaa nawasalimu nyote, napenda kufahamu Kwa yeyote mwenye uzoefu na hizi trector aina ya LOVOL kw kuangalia utendaji KAZI wake, utumiaj was mafuta, kuvumilia mazingra magumu, kupambana na ardhi ngumu nk. Nahtaji kujua maana nmeona wanauza Kwa bei rafiki
 
Foton tractor
 

Attachments

  • Screenshot_20230316_153824.jpg
    Screenshot_20230316_153824.jpg
    102.7 KB · Views: 28
  • Screenshot_20230316_154034.jpg
    Screenshot_20230316_154034.jpg
    74.9 KB · Views: 32
  • Screenshot_20230316_154047.jpg
    Screenshot_20230316_154047.jpg
    98 KB · Views: 27
  • Screenshot_20230316_154103.jpg
    Screenshot_20230316_154103.jpg
    112.8 KB · Views: 22
  • Screenshot_20230316_154133.jpg
    Screenshot_20230316_154133.jpg
    80.5 KB · Views: 23
Ukikuta kitu Bei rahisi ujue Kuna issue za spea, kuharibika Mara Kwa Mara hasa baada ya miaka miwili ya kazi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Pia inawezekana ni ishu ya kupromote soko KWA bidhaa mpya sokoni.
Fuso ziliuzwa kwa bei ya chini Sana, hata mabus na lori za kichina pia wakati zinaingia
 

Attachments

  • Screenshot_20230316_154143.jpg
    Screenshot_20230316_154143.jpg
    87.9 KB · Views: 22
Pia inawezekana ni ishu ya kupromote soko KWA bidhaa mpya sokoni.
Fuso ziliuzwa kwa bei ya chini Sana, hata mabus na lori za kichina pia wakati zinaingia
Umeongea kitu kizur mjumbe huenda baadae tunaeza kujuta ohoooo tungenunua wakat huo muda ushapta! Nakumbuka Kuna wilaya niliwahi kuuziwa shamba kw laki tatu nkaringa Leo huwez pata hata kw milion na nusu na ni miaka sita tu imepta
 
Kwenye kilimo kuna ishu wanasema, 'taarifa sahihi'. Ndani ya huu msemo kuna suala la muda ambalo ndani yake tena litaamua ni muda gani sahihi wa kulima, kupanda, kuvuna hadi kupeleka bidhaa sokoni. Ukikosea hapa, una asilimia kubwa ya kupata maumivu. Trekta nyingi za kichina kwa nchini kwetu, shida ni kupata spare. Unaambiwa dunia ni kijiji utaagiza na itakufikia.

Sawa hatukatai utaagiza na itakufikia. Je itachukua muda gani kukufikia? Muda wote wakati unasubiri hiyo spare, msimu wa kulima utaendelea kukusubiri?

Je Utafaninisha na yule ambae trekta ikiharibika, akipiga simu Mwanza mjini, Morogoro, Arusha, Dodoma au Dar na akasema spare anayohitaji akataja na namba ya spare kesho jioni anaipokea na kuifunga na kazi kuendelea?

Kuna ishu ya reliability, nina uzoefu na trekta aina tatu tofauti za kichina ambazo kwa umbo, mngurumo wake na sifa zilizokua zinapewa, utasema mashine ndo hizi. Ila hakuna hata moja ambayo ililima kwa misimu miwili.

Kingine, operators wengi wa matrekta hapa Tz ni wako rough sana. Nenda huko Kibaigwa, Kiberege, Bwawani na maeneo mengine mengi ukaone jinsi swarajs, masseys, new holland na zingine nyingi zinavyoteswa. Naamini trekta ya kichina ikimaliza msimu wa kulima itakua imechakaa kupita maelezo.

Pale Nanenane Morogoro. Wale jamaa wa Suma jkt. Walileta trekta za kichina zilikaa kama miezi nje pale, wakahamishia mle ndani zika kaa karibia mwaka na hazikuuzika. Ziliondolewa kimya kimya. Nawez kukupa namba ya muhusika palepale Morogoro umuulize ni kwanini hazikuuzika atakueleza mambo mengi tu.

Mwisho wa siku wewe mteja ndo mwenye maamuzi ya mwisho ya kuchukua kinachokufaa kwa kuzingatia ukubwa wa kazi yako, mazingira yako na aina ya kazi yako.
 
Nmekupata mkuu, je wew unashauri trector ipi inafaa sababu Kuna mtu mwingne anakwambia hata lovol znabei ndogo kw sasa kisa ni brand mpya wakishapata wateja ztapaa, km tech. Za kichina zmeweza kulisha China enyewe iweje huku zshindwe kaz? Mwngne akasema kampun ngap za mabas y kichina yabakimbiza hapa bongo mfn new force, je huon km nazd kuchanganykiwa Zaid na ulchokisema ww
 
Kuna jamaa alinunua Lovol yupo kiberege hapo. Alikua analima mashamba ya mpunga. Trekta ilikuja mwezi wa 11 ikiwa mpya kabisa ika mpaka msimu unaisha wa kulima mwezi wa pili ile trekta haikumaliza msimu ilikua ina matatizo kibao.

Tutafute statistics za Lovol. Ngapi zimeuzwa kwa wakulima, na ngapi bado zinafanya kazi. Changamoto gani wanaziface hao wakulima? Tuongee na hao wauzaji wa Lovol watuunganishe na wateja wao wa maeneo tofauti tofauti watupe uhalisi wa hizo trekta. Hawa watu wa mauzo hawezi kukuambia ukweli kama machines zao zina changamoto, ila watumiaji watasema. Lovol ngapi wewe binafsi umeziona zinafanya kazi hapa Tz? Kila siku watu wananunua matrekta. Mfano ni CASE, Sonalika na mengineyo ambayo yote bei zake zipo juu kuliko hiyo Lovol, kwanini hao wanaonunua wasikimbilie hii ya bei rahisi?

Isije kua kama yale Ursus. Trekta ziliingia nchini zikauzwa kwa bei nzuri sana na mkopo nafuu sana. Ziko wapi sasa hivi? Na zenyewe zilisifiwa mno na wakulima wengi wakazichukua tena kwa mkopo. Sasa hivi zaidi ya asilimia 70 wanalia kuhusu hizo trekta, na hapo spare zilikua zinapatikana hapa hapa nchini, je kama na spare zingekua za kuagiza huko Poland ingekuaje? Tuliaminishwa ni trekta imara hazina changamoto. Changamoto zilivyo anza kujitokeza. Kibao tukageuziwa wakulima hatujui namna ya kuzitumia. Report juu ya hizo trekta ilitolewa ikaonekana trekta zenyewe ndo hazifai huku kwetu. Ila hakuna mkulima alielipwa fidia, zaidi ya wale walioshindwa kulipa mkopo kunyang'anywa trekta zao.
 
Mtoa madam kama anapromote Hiyo lovol,, sijui labda Nimefatilia Reply zake na kuzielewa tofauti
 
Hapana ndg nmeleta hapa tupeane ufahamu maana sijawah kuiona ikiwa shamban kilchonivutia ni uzur wa Bei tu
 
Wanajukwaa nawasalimu nyote, napenda kufahamu Kwa yeyote mwenye uzoefu na hizi trector aina ya LOVOL kw kuangalia utendaji KAZI wake, utumiaj was mafuta, kuvumilia mazingra magumu, kupambana na ardhi ngumu nk. Nahtaji kujua maana nmeona wanauza Kwa bei rafiki
Lile gruop la wadau mbona jana wameongelea sana hili na ulikuwemo mule
 
Back
Top Bottom