Tetesi: Trend Reading: Mabadiliko Madogo ya Baraza la Mawaziri Yananukia!. Head-hunting Imeishaanza!.

Waziri wa Nishati needs to go. Tanesco inafilisika, inahitaji sio chini ya $200m haraka to sustain business. Hakuna taasisi itakayotoa mkopo bila guarantee kwamba mkopo utalipwa, na hili litahitaji tariffs kupanda. Muhongo amelivuruga shirika katika hili na anapaswa kuwajibika.

Waziri wa fedha ameshindwa kusimamia uchumi wa nchi, hasa bajeti. Bajeti yake ya karibia TZs trilioni 30 haikuwa realistic. Haitekelezeki. Pia vyanzo vya mapato ya serikali vimeshindwa to deliver. Anahitajika mtu Mpya.

Waziri wa mambo ya nje - tumekwama, tumejivuruga na jumuiya ya kimataifa.

Waziri wa Elimu - tumebomoa kuliko kujenga in the past one year. She needs to step aside.

Waziri TAMISEMI - masuala yote ya kimaendeleo ngazi za chini kuanzia elimu, afya, kilimo, Maji nk yanasimamiwa na wizara hii. Hakuna kinachofanyika. He needs to go.

Waziri wa nchi Muungano na Mazingira - tangia Uhuru mgogoro wa muungano haujawahi kufikia hali mbaya kama leo; pia mabadiliko ya tabia nchi yameathiri sana usalama wa chakula na wizara haikuja na intervention yoyote ya maana. He needs to step aside.

Waziri wa Chakula needs to go too. Ameshindwa kusimamia vyema the issue of national food security. He needs to go.

Waziri wa Katiba na Sheria. Taifa limepoteza fedha na muda kujikita katika mchakato wa katiba ambao matokeo yake yametupwa jalalani na yeye ametetea hilo. Akae pembeni.

Waziri wa utumishi - self explanatory. Hakuna kipindi watumishi wa umma wamedhalilishwa kinyume cha Sheria na katiba kama kipindi hiki. Hatoshi, she needs to go.

Waziri wa Habari - self explanatory.

And so forth and so forth.
Karibia kila wizara inahitaji mabadiliko.

Waziri Mkuu ameshindwa kusimamia serikali ipasavyo katika masuala yote haya na mengine mengi ikiwa ni pamoja na kushindwa kumshauri Rais ipasavyo. Yeye pia ajitafakari katika nafasi yake. Kama atabaki, basi mawaziri wote mizigo huko juu washughulikiwe.
 
Yeah kweli kabisa. Hata malaika Gabriel akiwa chini ya mheshimiwa wetu, nothing will happen
 
Tunataka mabadiliko ya Rais badala ya mabadiliko ya Mawaziri. Hili likiwezekana itakuwa bomba sana tuondokane na huyu janga kubwa la Taifa anayeendesha gari kama haina sukani.

 
Kwa vyovyote vile uteuzi huu ni ishara kwamba Profesa Maghembe ajiandae ajiandae....
Tetesi za ndani sana zinasema Dr.Mwakyembe anakwenda Maliasili na Utalii, Professa Kabudi anakwenda kuchukua Sheria na Katiba.

From very very reliable source.
[emoji19] [emoji19]
 
mkuu ungerahisisha tuuu.....BARAZA LA MAWAZIRI LIVUNJWE...!!!!......kwa kiasi cha mapungufu uliyoyabainisha...
 
Sawa Mayalla, lakini kwenye siasa hizo brains za Kabudi huenda zisitumika ipasavyo. Ni kweli siyo lazima awe waziri akamteua kwenda kusaidia bungeni lakini akimpa uwaziri tu kwangu kamtumia vibaya.
 
Hatimae umeunganisha I'd zako na umeamua kubaki na I'd verified user.. Na kuchukua post zako zileee zimekuja huku baada ya kugundua katika fake I'd ulileta post mzuri sana
Nilitaka kumuuliza ,mbona aliyeziletaga hizo tag zake za nyuma ni Pasco na siyo Paskali?teh teh!huyu mwandishi wa kujitegemea mara nyingine anajisahau
 
Jana baada ya teuzi mbili za wabunge wa bunge la JMT, ni wazi uteuzi wa Prof. Palamagamba Kabudi inaashiria baraza jipya la mawaziri kubadilishwa kuanzia sasa. Prof. Kabudi ni gwiji wa sheria na Mwalimu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kwa uteuzi wake, tayari kuna tetesi kuwa baadhi ya mawaziri watapigwa chini ama kubadilishwa katika wizara zingine. Hii ni kutokana na utendaji wao duni, na kushindwa kwenda na kasi ya Rais Dr. John Pombe Magufuli. Ambaye kasi yake ya kiutendaji imevunja rekodi mpaka sasa...

Wanaotarajiwa kupumnzishwa katika mabadiliko haya ni.......

1. Prof. Mpango
2. Eng. Lwenge
3. January Makamba
4. George Simbachawene
5. Ummy Mwalimu
6. Mwijage
7. Dr. Mwakyembe
8. Prof. Maghembe

Manaibu....
1. Kingwangala
2. Ramo Makani
3. Stela Manyanya

Sura mpya zinategemewa kuingia!...
 
Mmmm
Wameteuliwa Wawili Jana..Wewe umeandika list ndeefu...ina Maana wengine watachaguliwa Miongoni mwa Wabunge waliopo?Ili Kukidhi Hiyo "list yako?
Nawaza Tuuu...
 
Ummy Mwalimu Watakuwa wanamwonea!

Yule waziri wa mali asili Faru John hayupo? Big big no jamaa kweli mtambo, kma kweli hayupo nitaamini zile tetezi kuwa alifukia ngombe mzima asahaulike kutumbuliwa
 
Kwanini Prof. Kabudi na siyo wewe au mimi? Ngoja nipeleke suti zangu kwa dobi
 
Hamis Kigwangala yuko vizuri...sema ni muoga...ni kama anafanya ili kumrithisha mkulu...ila kujua anajua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…