Treni ya kwanza ya Umeme nchini Tanzania

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240


Kwa mara ya kwanza toka tanganyika na Zanzibar kuungana na kupatikana Tanzania Jana safari ya Kwanza ya treni ya umeme ya kisasa yenye kazi ya kusafirisha abiria ambayo inaitwa Electric multiple Unit kwa jina maarufu ni Treni ya mchongoko.



Ilianza safari toka Dar Es salaam, Morogoro mpaka Dodoma. Safari yake ya kwanza imeanza muda wa saa mbili asubuhi na kufika dodoma majira ya saa Tano na kupokelewa na mkuu wa mkoa dodoma mhe Rosemary senyamule.



Treni hiyo yenye Uwezo wa kusafirisha abiria jumla ya 589 lakini waliofanikiwa kusafiri Leo ni 320 ni mashuhuda wa Kwanza kupanda treni ya mwendokasi.



Chanzo: Trc (shirika la reli Tanzania)
 
Train ya kwanza ya umeme
Mkuu, zile zilizokuwa zinapiga route za dar to dodoma kwa sgr siku zote zilikuwa zinatumia makaa ya mawe?

Tangu April 2024 train za umeme zilikuwa zinafanya kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…