TRL mbona hambadiliki bado mnafanya biashara kizamani wakati Mkurugenzi ni wa kisasa?Hizi ratiba zenu za abiria kunapokuwa na mabadiliko labda ya ajali na ratiba ikavurugika hamtangazii wananchi.Inalazimika wananchi kwenda kutafuta taarifa kwenye mastesheni.Hebu jaribuni kuwa wa kisasa,mpeni hata station master uwezo wa kutangaza kwenye vyombo vya habari au hata kwenye magari ya matangazo.Tunadanganywa na wenye mabasi hakuna treni mara mnaiona hiyo inakuja kimya kimya.Na hapa Kigoma stesheni tuwekeeni hata ka Tv tunapongojea usafiri tupate hata taarifa za habari.