TRL, TAZARA, Uchina na Uendeshaji Treni

Iga

Senior Member
Joined
Dec 17, 2007
Posts
112
Reaction score
6
SIJUI kama wakuu na Wanasiasa wa Tanzania wakiwemo Kikwete, Lipumba, Slaa na wengineo wana habari kwamba China imekwishatengeneza Treni iendayo kasi kama zile za Japani na Ufaransa.

Na hivi ninavyoandika haya tayari Wachina wamewapiga chini Wajapani na kuikamata tenda ya kujenga treni iendayo mbio huko Saudi Arabia ili kurahisisha usafiri wa mahujaji nchini humo.

Kwa mtaji huu nitashangaa kama viongozi wetu kwa upofu na ubinafsi wao wataitoa tena TRL na TAZARA kwa watu wengine na sio WACHINA.
 
Inshu ni kwamba viongozi wetu hawaingii madarakani kuifanyia kazi nchi ila wanafanyia kazi nchi zingine! kama kiongozi anaenda nje kila siku anakutana na hizi vitu, kwa nini hata siku moja akasema ngoja nasi tujaribu hata kuboresha mradi mmoja baada ya mwingine seriously siyo kuachia katibu ambaye naye ni chapombe kweli hata plan hana! Nchi yetu ina vichwa kibao zinafanya kazi nje ya nchi, viongozi wetu hawataki changamoto za kuwalipa mishahara mizuri ili wafanyie kazi nchi yetu! Tuna kila sababu ya kuitwa masikini na tuna kila sababu ya kuitwa matajiri kwani wachina hao hao wanapora mali zetu wanatengeneza vitu vikali ambavyo huwezi kuamini raw material yanatoka Tz.

Kwa ufupi, kufanya mabadiriko Tz ni kujitoa mhanga kama sasa watz wanavyoonekana kutaka kufanya! Human resource ipo ya kutosha lakini management ndo mbovu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…