Trump na Xi Jinping tayari kimeshaumana huko. Kweli kila mbabe ana mbabe wake

China hawana lolote ni mikwara tu, soko lao kubwa ni Marekani.

Lakini kwenye migogoro kama hiyo ndio waafrika tungekuwa na akili ndo tungepata fursa ili kuuza bidhaa zetu lakini kwa bahati mbaya sana kama watu sampuli hii tulionao wa ccm ndio watawala hawana habari kabisa na hichi ninachokiongelea wao shida yao ni kuwa madarakani. That's all.
 
Kwa akili yako hujashikiliwa utauza nn China na USA au unaota ile ya kitanzania sisi tumatajiri hahaaa
 
View attachment 3231775
Trump anafikiri anaweza kumwendesha kila mtu atakavyo. Amekutana na kisiki cha China, hakitaki masihara hata kidogo. Ukimwaga mboga wenzako wanamwaga ubwabwa.
Jamii Forum imegeuka dampo na jalala la vihabari vya kuokoteleza. Kuna thread unakuta ni vihabari kutoka mtandao wa X tu lakini moderator wanachekelea tu.

Poor JF
 
Kwa akili yako hujashikiliwa utauza nn China na USA au unaota ile ya kitanzania sisi tumatajiri hahaaa
Kama Marekani anaweza kuagiza ndizi kutoka visiwa vya Caribbean, Uyoga kutoka Mexico na nguo kutoka mataifa mengi ya Amerika ya kati na kusini, sisi kama tungekuwa na serikali yenye kujitambua tungeshindwa nini kuuza hivyo vitu Marekani kupitia Agoa.
 
AGOA Trump anaensa kuifutilia mbali, sasa utauza vipi marekani?
 
CCM jurisdiction yake ni ndani ya mipaka ya Tanzania tu, haihusiki na bara lote la Afrika, hayo mataifa mengine ya Kiafrika si yachangamkie hizo fursa?
Kama hakuna basi hakuna sababu ya kuilamu CCM, Hilo ni tatizo mtambuka kwa bara lote, hivyo sio sahihi kuiweka CCM kama vile ndio SI Unit ya kushindwa.
 
... tatizo la dunia hii ni kila mzalishaji kulenga soko la Marekani, ... sasa huyo Marekani si atalinga sana? HII DUNIA INAENDA KUBADILIKA, TUTAKE TUSITAKE, NA MAREKANI KESHALIONA HILO!
 
akil zako ndogo sana , kwan ccp walisubir wenzake wa Asia ili kuiteka soko la dunia ? kuwa ccmu ni jibu tosha kwamb wew ni mjinga
 
Tuwauzie nini tena kwenye hiyo migogoro? Korosho, magobole?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…