Labani og
JF-Expert Member
- Sep 15, 2020
- 19,637
- 29,473
Mwenyekiti wa bodi ya Simba Salim Abdallah Try Again amesema Cesar Lobi Manzoki alisaini mkataba wa awali Simba (Pre contract) lakini baada ya kusaini mkataba na klabu ya hiyo, Manzoki alipata ofa nzuri zaidi ambayo analipwa mara sita zaidi ya wao walivyotaka kumlipa hivyo mchezaji aliomba aende China, na wao kama binadamu waliona ni bora wamruhusu kwasababu wachezaji wanategemea mpira kuendesha maisha yao hivyo basi sio vema kumzuia mchezaji kwenda sehemu ambayo atapata maslai zaidi.
“Manzoki alishasajili mkataba wa awali (pre-contract Simba) lakini yule ni binadamu, ni mchezaji ana career yake. Akatuomba, nimepata ofa China, nalipwa mshahara mara sita ambao mtanipa nyinyi. Mshahara wake kule ni Euro 60,000. (TSH150M kwa mwezi) Kama ubinadamu unafanyaje na yule ni mchezaji? Wewe hauna uwezo wa kumlipa Euro 60,000, unamruhusu!” alisema Salim Abdallah 'Try Again'
“Manzoki alishasajili mkataba wa awali (pre-contract Simba) lakini yule ni binadamu, ni mchezaji ana career yake. Akatuomba, nimepata ofa China, nalipwa mshahara mara sita ambao mtanipa nyinyi. Mshahara wake kule ni Euro 60,000. (TSH150M kwa mwezi) Kama ubinadamu unafanyaje na yule ni mchezaji? Wewe hauna uwezo wa kumlipa Euro 60,000, unamruhusu!” alisema Salim Abdallah 'Try Again'