Tsh. Trilioni 13 kwenye Bajeti ya Tanzania kwa mwaka 2023/24 ni Mikopo na Misaada

Tsh. Trilioni 13 kwenye Bajeti ya Tanzania kwa mwaka 2023/24 ni Mikopo na Misaada

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1678776290524.jpeg

Serikali inatarajia kuongeza 7% sawa na Tsh. Trilioni 2.9 ya Makusanyo kwenye Matumizi ya Fedha za Bajeti ya mwaka 2023/24 ili kufikia Tsh. Trilioni 44.38 kutoka Tsh. Trilioni 41.48 ya mwaka 2022/23.

Tsh. Trilioni 26.72 zitakusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupitia Kodi na kiasi kingine kitatoka kwenye vyanzo vingine visivyo vya Kikodi ikiwemo Misaada, Mikopo Nafuu na Mikopo ya Kibiashara.

Vipi Mdau, Una maoni gani kuhusu Bajeti na Je, inagusa maisha yako?

================

Serikali inatarajia kukusanya na kutumia Sh44.38 trilioni kwa mwaka 2023/2024 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.0 ya bajeti ya mwaka 2022/2023.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba ameyasema hayo leo Jumatatu Machi 13, 2023 wakati akiwasilisha kwa wabunge mapendekezo ya mpango wa Maendeleo wa Taifa na Ukomo wa Bajeti kwa mwaka 2023/2024.

Bunge mwaka jana lilipitisha Sh41.48 trilioni kwa ajili ya bajeti ya mwaka 2022/2023 kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka huo wa fedha.

Amesema katika mwaka wa 2023/2024 mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Sh31.38 trilioni sawa na asilimia 70.7 ya bajeti yote.

“Kati ya mapato hayo, mapato yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yanakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 13.0 hadi Sh26.72 trilioni kutoka makadirio ya Sh23.65 trilioni mwaka 2022/23,”amesema.

Amesema misaada na mikopo nafuu kutoka kwa washirika wa maendeleo inatarajiwa kufikia Sh5.46 trilioni sawa na asilimia 12.3 ya bajeti yote.

Aidha, Dk Mwigulu amesema Serikali inatarajia kukopa Sh5.44 trilioni kutoka soko la ndani ambapo Sh3.54 trilioni ni kwa ajili ya kulipia hatifungani na dhamana za Serikali zinazoiva.

Amesema pia Sh1.89 trilioni kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo na kwamba Serikali inatarajia kukopa Sh2.1 trilioni kutoka soko la nje kwa masharti ya kibiashara ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu.

MWANANCHI
 
Mikopo Kwa ujumla ni til.13.

Kuna mikopo ya ndani,
Mikopo ya Nje ya kibiashara,
Mikopo na Misaada (concessional loans)
 
Tunakopa 13
Tunalipa 12
Deni linaongezeka kwa 1
Zinazolipwa ni sawa na zinazokopwa..

Component kubwa ni deni la ndani so Haina shida ,pia Kwa deni la Nje component kubwa ni deni la concessional zaidi ya 70% so nako hakuna shida..

Ishu ni deni la kibiashara la Nje ndio Huwa mtihani ,ulazima wa Kukopa kwenye banks za biashara ni Kwa sababu unaweza kuzipata fasta so ukatobu shida ya haraka.
 
Back
Top Bottom