Tsivangarai akataa mapendekezo ya SADC.

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
..hivi kwanini hawampi Tsivangarai hiyo wizara na Zimbabwe ikasonga mbele?

..au kwanini Tsivangarai anakataa hata mapendekezo ya ku-share hiyo wizara ili wazimbabwe wasipate matatizo zaidi?

..baada ya kuwagomea viongozi wote wa SADC ni nani atakuwa na muda wa kusikiliza matatizo ya Zimbabwe??

 
Jokaa kuu

SADC ni kichekesho!

Hivi kweli hata ungekuwa ni wewe ungekubali?

Wewe angalia hiyo distribution ya wizara hapo juu. Do you think kuna lolote hapo? Mimi nimefuatilia kikao cha SADC nimegundua hata SADC wanamuogopa Mugabe kabisa! Its just pathetic.

All in all I advise Morgan to pull out. Mugabe anafikiri yeye ndo mwenye haki ya kuiongoza Zimbabwe as a private company!

Hivi waafrika tulirogwa? Morgan alipata kura kama Mugabe..lakini huyu mzee yeye anaona ndo mwenye haki ya kila kitu.

I say Morgan shoul resist this..inhuman and sadistic move by Mugabe and his henchmen.....
 
Masanja,

..wewe ungependekeza wagawane vipi hizo wizara?

..kwa jinsi nilivyoangalia MDC-T wamepewa wizara ambazo kwa kweli zitawapa nafasi ya kushughulikia matatizo ya wananchi wa Zimbabwe.

..hata wizara nyeti kama Finance wamepewa.

..halafu MDC-T wameonekana kuridhika na mgawanyo huo, na kilichobakia kilikuwa hiyo wizara ya mambo ya ndani.
 
SADC needs to grow a pair and do whats right, tell Mugabe whats whats, you cant treat dictators with kid gloves.
 
I still think it was a mistake for Morgan not to take part in the election, he could have taken part or called for the election to be postponed until an adequate level of oversight was administered.

My comfort level with Morgan stepped down significantly after that, revolutionaries do not fear bloodshed, the few who do, do not give up that easily.

Mugabe won the big jackpot and now we have this unnecessary stallmate.

If only Morgan was not such a coward.
 
Last edited:
inaonyesha jinsi gani nguvu ya dola ilivyo
muhimu kwa bw. morgan. anataka mambo ya
ya ndani ili nae awe na "kajeshi" kake. na wala sio
suala la kuwafikia wananchi na kuwaletea maendeleo.

wananchi wamefungwa goli na wanasiasa.
 
Tsivangarai yuko right kwenye hili. Hizo wizara alizopewa ni za kutafutiwa lawama. Hazina haina hela na uchumi umekufa. Chochote atakachofanya ili kujaribu kuufufua atawaudhi wananchi. Na wakati wote Robert ameshika rungu akimkoromea. Morgan alikosea kukubali kushirikiana na huyu dikteta. Yeye angejikalia pembeni amwache afurukute. Sasa amempa loophole ya kutokea.

Hao SADC nao wanazidi kujiaibisha. Heri wangenyamaza tu.
 
Kwenye institutions nyingine ni useless. Credibility ya SADC inaendelea kuporomoka kwa kufanya mambo ambayo hayana maana. Sijui wananufaika vipi kwa kumlinda Mugabe, sijui SADC inapata heshima gani kwa kumlinda Mugabe. Au ndio inaaza kuwa kama OAU, klabu ya madikteta?
 
George Soros kupitia taasisi zake za The Open Society Initiative for Southern Africa na The Open Society Institute ndiye anayeleta fujo kwenye nchi zinazoendelea kwa kumwaga fedha bila kuingiliwa. Matokeo yake akina Morgan Tsvangirai, Odinga and the alikes (Zanzibar wakiiga)hawakubali kushindwa. Kuna haja gani ya kufanya chaguzi za kidemokrasia kama vyama havikubali kushindwa then wanadai serikali ya mseto.. si watunge sheria ya kupokezana tu tujue moja?

Mbona hawapeleki idea zao za "mshindwa" kupewa umakamu wa rais, uwaziri mkuu au kugawana wizara kwenye nchi zilizoendelea?

Inabidi watuachie bara letu.
La muhimu turekebishe sheria za uchaguzi ili tufanye uchaguzi wa huru na wa haki, na tuache kubusu "behinds" za imperialists!! Haya mambo ya kuingilia mambo ya ndani ya serikali zetu ndio yanayosababisha ku-develop madikteta!
Vox populi, Vox Dei!
Sauti ya uma, Sauti ya Mungu!
Kama chama kimeshindwa uchaguzi, kisubiri next time. Mbona hawafanyi upuuzi huu Washington, Paris, London et cetera??
 
SADC for yet another time has shown its true colors. A cabal for African leaders in this area to guard their interest and meal and invite only the few they chose to and not otherwise. But a day of reckoning is not far. May be Tsivangarai can show the way!
 
SADC ni kikundi kingine kilichojaa cowards!Hivi wataendelea kumuogopa Mugabe mpaka lini?Kwani huyo Mugabe anawatishia nini?
Hawawezi kufanya maamuzi sahihi ambayo yatawakomboa Wazimbabwe?Kwa nini mtu mmoja anakosesha watu zaidi ya Milioni Kumi Amani na utulivu and still he is being entertained?
Kwenye kikao cha SADC wanadai Mugabe was so abusive,violent and aggressive.Sasa wataendelea na huo upuuzi mpaka lini?
Tumwogope Mungu na hiyo SADC wawatendee haki watu wa Zimbabwe!
 
hivi ni kwanini tunamchukia Mugabe?, hapa mimi naona watu wengi hawapendi rais kukaa madarakani muda mrefu wakati hilo si kosa kabisa. muhimu wananchi wanamtaka. Nakuhusu uchumi kuharibika sio Mugabe wa kulaumiwa, walioumiza uchumi wa zimbambwe ni Mazungu ya ulaya baada ya kufukuzwa kwa wapwa zao.
Ukitaka kujua siasa ya dunia ilivyombaya kumbuka wakati mzee kabila alipompindua Mobutu alipongezwa na dunia yote wakisahau shutuma na laana walizotoa kwa wanajeshi waliopindua Ivory Cost wikimoja iliyopita. yaani akiwa aliyepinduliwa ni Mzee wa sikunyingi na kuitwa dikteta basi ni sawa, lakini akiwa ni "kijana"(japo pia ni mzee) na mwenzetu rafiki basi hilo ni kosa kubwa sana.
 

Wananchi ndio waliomchagua Mugabe?I thought Tsangirai ndiye aliyeshinda uchaguzi then Mugabe rigged the elections?
Ni kwa nini aliwafukuza hao Wazungu kama siyo upuuzi wake?
Hawa watu walikuwa wanachangia kukua kwa uchumi wa Zimbabwe then yeye from nowhere expels them!What dou expect wazungu wenzao ambao ndio wameshikilia uchumi wa dunia watareact?
Nchi yake hivi sasa ina shida ya chakula vibaya sana and he is dong nothing to adress that issue!
 
Malengo ya Tsvangarai wakati mwingine ni magumu kuyaelewa. Yeye amepewa wizara ya katiba na sheria na ana viti vingi bungeni, sasa anashindwa nini kukubali wizara hizo na kutumia wizara hiyo na wabunge wake kushape katiba katika mfumo anaomini utawafaa wazimbabwe. Yaani kwake yeye silaha na askari wa wizara ya mambo ya ndani zina nguvu sana kuliko bunge, katiba and by the way na wizara ya uchumi iko kwenye column yake. Huyu jamaa is a moving natural disaster!!!
 

hajapewa wizara ya fedha kwani?
 
hajapewa wizara ya fedha kwani?
Kapewa wizara ya uchumi na biashara. Wizara ya fedha nadhani imebaki kwa Mkongwe. Huyu Tsvangarai nadhani anaenjoy kupata attention ya dunia, kwa sababu ukiangalia challenges alizokutana nazo hii ya kunyimwa wizara ya mambo ya ndani haitegemewi kumfanya aendelee kubakia "mitaani", kama lengo lake ni kuwatumikia wazimbabwe then amepewa fursa hiyo na sasa anaikataa "in your face"!
 


apewe na hiyo wizara ya fedha, bila hivyo kelele hazitakwisha.
 
...Mugabe must go,30 yrs in power bado anataka nini? na SADCC nayo ni aibu nyingine tuu ndio maana viongozi wenye akili hawashughuliki nayo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…