TTCL imezindua Minara sita ya Mawasiliano katika Wilaya ya Mlele mkoani Katavi

TTCL imezindua Minara sita ya Mawasiliano katika Wilaya ya Mlele mkoani Katavi

James Hadley Chase

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
1,984
Reaction score
3,695
TTCL imezindua Minara sita ya Mawasiliano katika Wilaya ya Mlele mkoani Katavi ili kuimarisha huduma ya upatikanaji wa Mawasiliano kwa Wananchi.

Uzinduzi huo umefanywa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (Mb) ambaye pamoja na mambo mengine amesema Serikali imedhamiria kuimarisha huduma za Mawasiliano na TEHAMA katika maeneo ya mipakani na maeneo yasiyo na mvuto wa kubishana ili kuchochea fursa mbalimbali za kiuchumi na kuimarisha sekta ya elimu na afya kwa Wananchi.

Minara hiyo iliyojengwa kwa ufadhili wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) itawanufaisha wakazi wa Kaulolo, Kamalampaka, Kafuru, Songambele na Ibelamafipa.

Akizungumza katika Uzinduzi huo Mbunge wa Jimbo la Mlele Mhe. Francis Kamwelwe eishukuru Serikali kupitia UCSAF kwakuliwezesha Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kujenga mnara katika kata ya Inyonga Jimbo la Mlele.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Mhandisi Peter Ulanga amesema ujenzi wa mradi huu umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 11.47 hadi kukamilika, mbapo kati ya hizo TTCL imetoa kiasi cha shilingi bilioni 6.35 na UCSAF imetoa kiasi cha shilingi bilioni 5.15.

#RudiNyumbaniKumenoga

May be an image of 3 people and people standing







May be an image of 7 people, people standing and outdoors





May be an image of 5 people and people standing



May be an image of 10 people, people standing and outdoors
 
Hiyo minara watatumia Airtel kujiimarisha na hakuna kitu mtafanya, watafunga antena zao hapo kama minara yao vile
Minara yote unaweza kodisha kuweka vifaa vyako.
Airtel, Tigo, Voda, Halotel hawamiliki minara, wao wamekodi kwa HTT

TTCL naye akijenga atakodisha ili apate faida
 
TTCL ilitakiwa iwe ndio baba wa mawasiliano yote hata njia zote za chini na juu ilikuwa wao ndio wanatoa

Hiyo Halo njia zake za chini kama wangekuwa na akili ilikua leo wanawakodishia

Wajifunze kwa BT wazungu wako mbali kila njia ni zao na landlines zote zao wanakodisha tu
Ila hongera zao
 
Minara yote unaweza kodisha kuweka vifaa vyako.
Airtel, Tigo, Voda, Halotel hawamiliki minara, wao wamekodi kwa HTT

TTCL naye akijenga atakodisha ili apate faida
Shida ni kwamba watawapa bure bila kulipwa chochote, ila kuna 10% itatembezwa hapo
 
ttcl inakuwaje mnakosa laini,nimefika ofisini na kwa mawakala mara kwa mara wanasema laini akuna,naona namba yangu iliyopotea itafungiwa kwa kuchelewa kui-renew.
 
Watu wa TBC, TTCL, POSTA sijui mkoje? Hii nayo Ni breaking news? 2023?
 
Back
Top Bottom