Tuache shortcut; tuwekeze kweli kama tunataka mafanikio ya Taifa Stars

Tuache shortcut; tuwekeze kweli kama tunataka mafanikio ya Taifa Stars

chibuOG

Senior Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
169
Reaction score
337
Asalaam Aleikum Wanajukwaa,Natumai wote mko poa na mnaendelea na harakati za maisha ya kila siku.
Niende moja kwa moja kwenye pointi ya MSINGI ambayo ni Timu ya Taifa ya Tanzania yaani TAIFA STARS.Kama kichwa cha habari hapo kinavyojieleza kuwa tunatakiwa tufanye uwekezaji wa kweli kama tunataka mafanikio ya kweli kwenye soka letu,Kwa maana hizi lipua lipua na bahati nasibu haziwezi kutufikisha nchi ya Ahadi ya maziwa na Asali.

Cha kwanza, Ligi za vijana za under 17 na under 20 zisiwe mabonanza bali ziwe ligi haswa kama ilivyo ligi kuu.Yaani kama inawezekana ratiba ya ligi kuu ya NBC ndo iwe ratiba ya under 17 NA UNDER 20 vilevile ili kuwaandaa hao vijana kwaajili ya ushindani wa kweli.Huwezi kumuandaa kijana ambae anatarajiwa kucheza ligi kuu na timu ya Taifa kwa bonanza la wiki mbili au mwezi mmoja halafu awe tayari kucheza Ligi kuu.

Cha Pili,Mafanikio ya Vilabu vya SIMBA,YANGA na AZAM yasilipumbaze Taifa tukaona kuwa tumepiga hatua kubwa kisoka.Kuna gape kubwa mno la ubora na uwekezaji kati ya vilabu hivyo vitatu na vilabu vingine vya ligi kuu Tanzania.Kwahiyo tuweke mazingira sahihi na yenye usawa ili uwekezaji ufike mpaka huko kwenye timu za kati na timu za madaraja ya chini kabisa.

Cha Tatu, Tutoe siasa kabisa kwenye mpira wetu kwa maana unatumika kwa manufaa ya wanasiasa na wala sio kwaajili ya maendeleo ya mchezo wenyewe.Tuweke mifuo thabiti ya uendeshaji soka bila kuvipendelea hivi vilabu vya kurithi vya Kariakoo ambavyo kimsingi ni Mtaji mkubwa wa wanasiasa na vinatumika sana.

Cha Nne, TFF ambae kimsingi ndio mzazi na mlezi wa soka la nchi hii waweke msisitizo kwenye kanuni na taratibu walizoziweka kuhusu soka la vijana maana kwasasa kinachofanyika ni kama kiini macho na kujitekenya wenyewe.Under 20 na under 17 ni geresha tu na vilabu vimeanzisha kukidhi matakwa ya kikanuni tu wala hamna msisitizo wa hilo jambo kabisa kwa vilabu na hata TFF wenyewe.

Ongeza zingine mdau tuweze kujadili kulisaidia soka la nchi yetu.Ahsanteni kwa kunisoma na Nisameheni kwa makala ndefu.

NB:HIVI ULISHAWAHI KUJIULIZA KAMA MO DEWJI, GSM NA BAKHRESA WAKIAMUA KUACHANA NA SOKA LA NCHI HII TUTARUDI HATUA NGAPI NYUMA? TUWEKE MIFUMO SAHIHI ITAKAYOVUTIA UWEKEZAJI WA KWELI TUSITEGEMEE PESA ZA WATU MFUKONI BALI VILABU VIJIENDESHE VYENYEWE.
 
Umeongea Point sana,Yanga ni bora mara 100 kuliko Taifa stars,kwa nini Taifa Stars nayo isiwe bora?
Mkuu ubora na uwezo wa vilabu vyetu vinabebwa na wachezaji wa kigeni sio wazawa. Angalia Yanga iliyo bora inatoa wachezaji wangapi wa first eleven wa ndani? Ni Mudathir, Job, Mzize, na Baca pekee hao ndio wachezaji wazawa wanaoweza kupata nafasi ndani ya kikosi cha Yanga.
 
Umeongea Point sana,Yanga ni bora mara 100 kuliko Taifa stars,kwa nini Taifa Stars nayo isiwe bora?
Eeeh club na national team dynamics zake ni todauti sana. Yanga anaweza nununua mchezaji yoyote duniani suala ni ndalama tuu national team u cant
 
Mkuu ubora na uwezo wa vilabu vyetu vinabebwa na wachezaji wa kigeni sio wazawa. Angalia Yanga iliyo bora inatoa wachezaji wangapi wa first eleven wa ndani? Ni Mudathir, Job, Mzize, na Baca pekee hao ndio wachezaji wazawa wanaoweza kupata nafasi ndani ya kikosi cha Yanga.
Sii ujinga wetu wenyewe kuruhusu wageni wengi ingiwekwa limit ya foreigners watano tuu
 
Sii ujinga wetu wenyewe kuruhusu wageni wengi ingiwekwa limit ya foreigners watano tuu
Ishu sio ujinga wetu ishu je wazawa wenye viwango wapo? Kama wapo ni rahisi tu kushindania namba dhidi ya hao wageni. Angalia Mudathir anavyokiwasha, angalia Baca, angalia Job je wachezaji wengi wa kitanzania kwenye vilabu vyao wangekuwa na ubora na kiwango kwa mfano huo je tusingekuwa na timu nzuri ya taifa? Mfano mwingine mwangalie Tshabalala pamoja na umri umeenda lakini bado pale Simba ni mtu haswa hata akija mgeni ajipange kwa kila kitu kwanzia fitness hadi kiwango. Tshabalala ana utimamu mzuri wa kimwili. Hio ni baadhi tu ya mifano, tusizingizie wageni bali hatuna wachezaji wa maana kwenye ligi yetu. Wageni ndio wanaojitahidi kutupa mwamko na changamoto za kufanya vizuri.
 
Umeongea Point sana,Yanga ni bora mara 100 kuliko Taifa stars,kwa nini Taifa Stars nayo isiwe bora
 
Ishu sio ujinga wetu ishu je wazawa wenye viwango wapo? Kama wapo ni rahisi tu kushindania namba dhidi ya hao wageni. Angalia Mudathir anavyokiwasha, angalia Baca, angalia Job je wachezaji wengi wa kitanzania kwenye vilabu vyao wangekuwa na ubora na kiwango kwa mfano huo je tusingekuwa na timu nzuri ya taifa? Mfano mwingine mwangalie Tshabalala pamoja na umri umeenda lakini bado pale Simba ni mtu haswa hata akija mgeni ajipange kwa kila kitu kwanzia fitness hadi kiwango. Tshabalala ana utimamu mzuri wa kimwili. Hio ni baadhi tu ya mifano, tusizingizie wageni bali hatuna wachezaji wa maana kwenye ligi yetu. Wageni ndio wanaojitahidi kutupa mwamko na changamoto za kufanya vizuri.
Bwana wewee huku chini mmewekeza mpaka mpate hao vijana wazuri kwa wingi wakutosha? Hao ethiopia ligi yao in aforeige rs wangapi mbona jana wanaubonda kweli kweli....asikudanganye mtu bwana ukiwekeza huku chini utafanikiwa tuu tena wee ndio utakuwa unauza wachezaji. Sie hatutaki kufanya hivyo na sio kwamba quality players hawapo...wapo ila tunataka mambo ya upigani katika selections za hao u17 na u20.
Ili mtoto achaguliwe basi mzazi wake atoe japo kitu ndio majanga yenyewe hayo.
 
Asalaam Aleikum Wanajukwaa,Natumai wote mko poa na mnaendelea na harakati za maisha ya kila siku.
Niende moja kwa moja kwenye pointi ya MSINGI ambayo ni Timu ya Taifa ya Tanzania yaani TAIFA STARS.Kama kichwa cha habari hapo kinavyojieleza kuwa tunatakiwa tufanye uwekezaji wa kweli kama tunataka mafanikio ya kweli kwenye soka letu,Kwa maana hizi lipua lipua na bahati nasibu haziwezi kutufikisha nchi ya Ahadi ya maziwa na Asali.

Cha kwanza, Ligi za vijana za under 17 na under 20 zisiwe mabonanza bali ziwe ligi haswa kama ilivyo ligi kuu.Yaani kama inawezekana ratiba ya ligi kuu ya NBC ndo iwe ratiba ya under 17 NA UNDER 20 vilevile ili kuwaandaa hao vijana kwaajili ya ushindani wa kweli.Huwezi kumuandaa kijana ambae anatarajiwa kucheza ligi kuu na timu ya Taifa kwa bonanza la wiki mbili au mwezi mmoja halafu awe tayari kucheza Ligi kuu.

Cha Pili,Mafanikio ya Vilabu vya SIMBA,YANGA na AZAM yasilipumbaze Taifa tukaona kuwa tumepiga hatua kubwa kisoka.Kuna gape kubwa mno la ubora na uwekezaji kati ya vilabu hivyo vitatu na vilabu vingine vya ligi kuu Tanzania.Kwahiyo tuweke mazingira sahihi na yenye usawa ili uwekezaji ufike mpaka huko kwenye timu za kati na timu za madaraja ya chini kabisa.

Cha Tatu, Tutoe siasa kabisa kwenye mpira wetu kwa maana unatumika kwa manufaa ya wanasiasa na wala sio kwaajili ya maendeleo ya mchezo wenyewe.Tuweke mifuo thabiti ya uendeshaji soka bila kuvipendelea hivi vilabu vya kurithi vya Kariakoo ambavyo kimsingi ni Mtaji mkubwa wa wanasiasa na vinatumika sana.

Cha Nne, TFF ambae kimsingi ndio mzazi na mlezi wa soka la nchi hii waweke msisitizo kwenye kanuni na taratibu walizoziweka kuhusu soka la vijana maana kwasasa kinachofanyika ni kama kiini macho na kujitekenya wenyewe.Under 20 na under 17 ni geresha tu na vilabu vimeanzisha kukidhi matakwa ya kikanuni tu wala hamna msisitizo wa hilo jambo kabisa kwa vilabu na hata TFF wenyewe.

Ongeza zingine mdau tuweze kujadili kulisaidia soka la nchi yetu.Ahsanteni kwa kunisoma na Nisameheni kwa makala ndefu.

NB:HIVI ULISHAWAHI KUJIULIZA KAMA MO DEWJI, GSM NA BAKHRESA WAKIAMUA KUACHANA NA SOKA LA NCHI HII TUTARUDI HATUA NGAPI NYUMA? TUWEKE MIFUMO SAHIHI ITAKAYOVUTIA UWEKEZAJI WA KWELI TUSITEGEMEE PESA ZA WATU MFUKONI BALI VILABU VIJIENDESHE VYENYEWE.
Bwana yesu asifiwe
 
Bwana wewee huku chini mmewekeza mpaka mpate hao vijana wazuri kwa wingi wakutosha? Hao ethiopia ligi yao in aforeige rs wangapi mbona jana wanaubonda kweli kweli....asikudanganye mtu bwana ukiwekeza huku chini utafanikiwa tuu tena wee ndio utakuwa unauza wachezaji. Sie hatutaki kufanya hivyo na sio kwamba quality players hawapo...wapo ila tunataka mambo ya upigani katika selections za hao u17 na u20.
Ili mtoto achaguliwe basi mzazi wake atoe japo kitu ndio majanga yenyewe hayo.
Hapo kwenye uwekezaji ngazi ya vijana ndio lilipo tatizo lakini sio swala la kusema wageni kuwa wengi ndio iwe tatizo.
 
Hapo kwenye uwekezaji ngazi ya vijana ndio lilipo tatizo lakini sio swala la kusema wageni kuwa wengi ndio iwe tatizo.
Kuwa na wageni wengi ni tatizo mwanawane tusishupaze vichwa.
 
Tatizo lake ni lipi? Zamani ligi yetu ilikuwa na wageni wachache je tulipiga hatua kwa kiasi gani?
Sasa mgei hatua vipi wakati wananchi wenyewe wapuuzi. Waziri anasema mochezo itolewe mashuleni na sie tunakubali sii ujinga huo.
Ukiweka limitation on foreign quota maana yake ni kwamba watu watalazimika kuthink on how to develope players na vitu kama hivyo. Lakini unaniambia kwamba naweza jaza from namba moja mpaka 11 wachezaji wakigeni sii najaza tuu. Kiufupi wingi wa wachezaji wa kigeni udumaza fikra za watu wanao husika kwenye hiyo sector.
Leo hii wee sema tuu kwamba ositions mbili za gk na striker huwezi kuleta foreign player. The ripple effect ni kwamba tayari watu inabidi waanze kuwa namna gani tutadevelope gk wazuri na strikers wazuri. Tutaanza kufikiri na ndio wenzetu walipata kuendelea.
 
Huo mpira wenyewe tunaosema umekuwa unategemea vilabu vitatu tuu ambavyo navyo havina cha kujivunia zaidi tu ya kutegemea HYPE ya wasemaji wao kitu ambacho sio kibaya kibiashara lakini kiufundi na kimaendeleo ya mpira haswa inakuwa ni sawa na kupaka rangi upepo maana Mahyperman kweli wanafanya kazi ya kuhype lakini je tunafanya uwekezaji sahihi katika kulea kukuza na kuendeleza vipaji vya watoto na vijana wa kitanzania? Mfano Mzize katoka Under 20 ya YANGA je huko alikokuwa mchezaji mzuri alikuwa peke yake tuuu? Hao wengine wameenda wapi? Vipaji vyao ndo vimekufa au nani ataviendeleza?
 
Wachezaji wetu wajifunze kufanya mazoezi binafsi mechi ya jana frisal, balua na mzize fitness yao ilikuwa chini mno
 
Back
Top Bottom