Tuache utani, usione mwenzako ana six packs ukadhani kaziokota barabarani

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Wakuu habari ya muda huu,

Kusema kweli nieape tu pongezi wote wenye six packs au flat belly kwa jitihada zao.Usione mtu ana six packs ukamchukulia poa ukadhani zinaokotwa ti barabarani au zinapatikana kwa urahisi.

Nimeanza mazoezi hii wiki ya pili mazoezi ya kipunguza tumbo baada ya kuona linaanza dalili za ukitambi ukitambi, aisee asikwambie mtu hapa natamani hata kuacha mazoezi, misuli yote ya tumbo inauma vibaya sana.

Kwa kweli heshima kwenu wenye six packs, kupata six packs au tumbo flat hasa kama una kitambi sio kazi lele mama, unahitaji kujitoa dhabihu(sacrifice).

Wakuu nitakieni heri nisike ishia njiani na haya mazoezi + kutokula.
 
Hongera Sana mkubwa. Ilinichukua miezi sita ku fikia Hatua hii.

Ningependa ku sisitiza uwe na diet plan. Sababu Kama unafanya mazoezi na kuendelea na nyama choma bia uta strangle tu na labda usitoe Hata hicho kitambi.

Kingine ule vyakula vyenye protein Sana. Mi nilikuwa kilo 70 sasa kilo 57.

Nadhani mwanamke au mwanaume anapendeza bila kitambi . Na kitambi ni ugonjwa.
 
Hongerah usiache kwani kurudia kazi. Kwa kweli hongerah zao!
 
mkuu diet ndo kitu cha muhimu kabisa katika kujenga six pack,usipozingatia diet utajikuta mwisho wa siku kidume umevimba makalio au hipsi kama unajijua unashindia big g na maji bora ukaachana na hiyo kitu ya kutaka six pack mwisho wa siku unakosa hizo six pack unapata seven pack yaan umbo kama la nyoka halina mbele wala nyuma...
 
Aisee kwa jinsi nilivyo kimbau mbau natamani kuwa na kitambi balaa, labda dharau hapa mjini kwa sababu ya haka ka mwili zitapungua.

Kitambi kinaleta heshima sana mjini hapa
Kitambi ni ugonjwa mkuu, mwanaume ukiwa na kitambi unakua shapeless, mbaya zaidi uwe mfupi unakua kama kichuguu.
 
Mbona unanikatisha tamaa asee mi nataka nilianzishe wasije wakanisaidia kiburudisho changu maana hapa nilipo nina 1pack ya balaa
Mkuu kwa kweli sio jambo la kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa, lazima ugangamale brother.
 
Ngoja na mie nianze kutafuta seven packs...
 
Shukrani mkuu, niongezee maujanja kiongozi.

Kwa kua nia yangu ni kupunguza tumbo nimenza kwanza na kubadili mfumo wangu wa ulaji.
Nakula mara moja kwa siku zaidi ya kunywa maji mengi sana na juice(blended).

Ni hayo tu nafanya kwa sasa, kwa kweli inahitaji moyo. Kama kuna sehem naatakiwa kurekebisha zaidi hasa kwenye mlo pia niambie.
 
Ok, hebu niambie nini cha kufanya.

Sinywi pombe na huwa sinywi.
Kwenye nyama choma hapo nilikua nakula karbu kila siku ila sasa nakula wkend tu mara moja,kitimoto nakula mara moja moja sana.

Ratiba nyingine ya kula nakula mara moja kwa siku toka mara tatu, yaani chai nimeiskip,chakula cha usiku nimeskip nakunywa tu kikombe kimoja cha maji ya moto au juice basi.

Wapi nakosea na wapi natakiwa kurekebisha. Nia yangu hasa sio kupata six pack, ni kua na tumbo flat tu liwe na six pack au lisiwe nayo.

Actually sina kitambi ila naona tumbo linaanza kudevelop tabia za ukitambi ukitambi.
 
Aisee kwa jinsi nilivyo kimbau mbau natamani kuwa na kitambi balaa, labda dharau hapa mjini kwa sababu ya haka ka mwili zitapungua.

Kitambi kinaleta heshima sana mjini hapa
 
Siku hizi kuna shortcut
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…