Tuacheni uharibifu huu wa lugha yetu maridhawa Kiswahili

Tuacheni uharibifu huu wa lugha yetu maridhawa Kiswahili

MwanaHaki

R I P
Joined
Oct 17, 2006
Posts
2,401
Reaction score
707
Waungwana,

Hebu jamani tuache uharibifu wa lugha yetu maridhawa, Kiswahili. Ninayo mifano mingi ya uharibifu, lakini ngoja niwape hii michache.

1. Tangazo la Zain linasema "Ongea kwa Sh 1 masaa 24". Kwenye muda, hakuna uwingi, kwa hiyo, tangazo hilo lilipaswa kutamka "Ongea kwa Shs 1 kwa saa 24".

2. Watangazani wengi wa redio na luninga, na sasa hata vijana wengi, wanasema "nyimbo hii" wakiwa wanatamka juu ya "wimbo" mmoja. Tamko sahihi ni "wimbo huu". Ni Kiswahili potofu kutamka "nyimbo hii", kwani kwa usahihi, kinachopaswa kutamkwa ni "wimbo huu" au "nyimbo hizi".

3. Wanasiasa wengi huwa wanatamka "mashuleni" au "mahospitalini". Maneno "shule" na "hospitali" ni baadhi ya maneno ambayo hayana uwingi. Kwa hiyo, wanachopaswa kutamka ni "shuleni" au "hospitalini". Wengine wanadiriki kwenda mbali zaidi, na kutamka "maofisini", wakati walipaswa kutamka "ofisini", au "makazini" wakati walipaswa kutamka "kazini".

4. Kwenye hafla nyingi sana, watu hutamka "Kwa niaba yangu mimi mwenyewe..." Hii si sahihi hata kidogo. Huwezi kusema kitu kwa niaba yako mwenyewe... unasema kwa niaba ya mtu au watu wengine. Huwezi kujiwakilisha wakati wewe upo kwenye hafla hiyo. Neno "niaba" linatumika kwa kuwawakilisha watu ambao wapo au hawapo mahala unapokuwa unaongea; unaweza kuzungumza kwa niaba ya watu ambao kwa mujibu wa ratiba, hawawezi kuongea au itakuwa ni usumbufu, na pia, watu ambao kwa wakati huo hawapo mahala hapo.

5. Hili la mwisho ni baya zaidi, kwani linatumiwa na waandishi wengi wa habari. Mfano: "Binti huyo aliyetaka kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." Hivi hii inaingia akilini kweli? Kina mtu anayetaka kubakwa? Wangeandika: "Binti huyo aliyenusurika kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." ingeeleweka kwa usahihi wake. Lakini kwa kuwa siku hizi kwenye vyombo vya habari HAKUNA WAHARIRI, wanapitisha makosa ya AIBU kama hayo!

TUSIPOTOSHE kwa makusudi lugha yetu maridhawa, Kiswahili!

./Mwana wa Haki (Mwanafunzi wa Andanenga...)
 
Waungwana,

Hebu jamani tuache uharibifu wa lugha yetu maridhawa, Kiswahili. Ninayo mifano mingi ya uharibifu, lakini ngoja niwape hii michache.

1. Tangazo la Zain linasema "Ongea kwa Sh 1 masaa 24". Kwenye muda, hakuna uwingi, kwa hiyo, tangazo hilo lilipaswa kutamka "Ongea kwa Shs 1 kwa saa 24".

2. Watangazani wengi wa redio na luninga, na sasa hata vijana wengi, wanasema "nyimbo hii" wakiwa wanatamka juu ya "wimbo" mmoja. Tamko sahihi ni "wimbo huu". Ni Kiswahili potofu kutamka "nyimbo hii", kwani kwa usahihi, kinachopaswa kutamkwa ni "wimbo huu" au "nyimbo hizi".

3. Wanasiasa wengi huwa wanatamka "mashuleni" au "mahospitalini". Maneno "shule" na "hospitali" ni baadhi ya maneno ambayo hayana uwingi. Kwa hiyo, wanachopaswa kutamka ni "shuleni" au "hospitalini". Wengine wanadiriki kwenda mbali zaidi, na kutamka "maofisini", wakati walipaswa kutamka "ofisini", au "makazini" wakati walipaswa kutamka "kazini".

4. Kwenye hafla nyingi sana, watu hutamka "Kwa niaba yangu mimi mwenyewe..." Hii si sahihi hata kidogo. Huwezi kusema kitu kwa niaba yako mwenyewe... unasema kwa niaba ya mtu au watu wengine. Huwezi kujiwakilisha wakati wewe upo kwenye hafla hiyo. Neno "niaba" linatumika kwa kuwawakilisha watu ambao wapo au hawapo mahala unapokuwa unaongea; unaweza kuzungumza kwa niaba ya watu ambao kwa mujibu wa ratiba, hawawezi kuongea au itakuwa ni usumbufu, na pia, watu ambao kwa wakati huo hawapo mahala hapo.

5. Hili la mwisho ni baya zaidi, kwani linatumiwa na waandishi wengi wa habari. Mfano: "Binti huyo aliyetaka kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." Hivi hii inaingia akilini kweli? Kina mtu anayetaka kubakwa? Wangeandika: "Binti huyo aliyenusurika kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." ingeeleweka kwa usahihi wake. Lakini kwa kuwa siku hizi kwenye vyombo vya habari HAKUNA WAHARIRI, wanapitisha makosa ya AIBU kama hayo!

TUSIPOTOSHE kwa makusudi lugha yetu maridhawa, Kiswahili!

./Mwana wa Haki (Mwanafunzi wa Andanenga...)

Ananlysis yako ni nzuri sana kwa mwalimu anayefundisha kiswahili darasani, au mytu anapokuwa annandika kwenye karatasi, na si kwa mswahili aliyezaliwa anaongea kiswahili. After all, wewe unadhani wanaotamka hivyo hawajui kuwa kifasaha maneno yake ni yapi? Lugha ya kuongea ina manjonjo yakena in fact imnatofautiana kidogo na lugha ya kuandika. Ya kuongea always inakuwa si haina ulzima sana wa kuwa fasaha mno, japo inabidi iwe intelligible!
 
Waungwana,

Hebu jamani tuache uharibifu wa lugha yetu maridhawa, Kiswahili. Ninayo mifano mingi ya uharibifu, lakini ngoja niwape hii michache.

1. Tangazo la Zain linasema "Ongea kwa Sh 1 masaa 24". Kwenye muda, hakuna uwingi, kwa hiyo, tangazo hilo lilipaswa kutamka "Ongea kwa Shs 1 kwa saa 24".

2. Watangazani wengi wa redio na luninga, na sasa hata vijana wengi, wanasema "nyimbo hii" wakiwa wanatamka juu ya "wimbo" mmoja. Tamko sahihi ni "wimbo huu". Ni Kiswahili potofu kutamka "nyimbo hii", kwani kwa usahihi, kinachopaswa kutamkwa ni "wimbo huu" au "nyimbo hizi".

3. Wanasiasa wengi huwa wanatamka "mashuleni" au "mahospitalini". Maneno "shule" na "hospitali" ni baadhi ya maneno ambayo hayana uwingi. Kwa hiyo, wanachopaswa kutamka ni "shuleni" au "hospitalini". Wengine wanadiriki kwenda mbali zaidi, na kutamka "maofisini", wakati walipaswa kutamka "ofisini", au "makazini" wakati walipaswa kutamka "kazini".

4. Kwenye hafla nyingi sana, watu hutamka "Kwa niaba yangu mimi mwenyewe..." Hii si sahihi hata kidogo. Huwezi kusema kitu kwa niaba yako mwenyewe... unasema kwa niaba ya mtu au watu wengine. Huwezi kujiwakilisha wakati wewe upo kwenye hafla hiyo. Neno "niaba" linatumika kwa kuwawakilisha watu ambao wapo au hawapo mahala unapokuwa unaongea; unaweza kuzungumza kwa niaba ya watu ambao kwa mujibu wa ratiba, hawawezi kuongea au itakuwa ni usumbufu, na pia, watu ambao kwa wakati huo hawapo mahala hapo.

5. Hili la mwisho ni baya zaidi, kwani linatumiwa na waandishi wengi wa habari. Mfano: "Binti huyo aliyetaka kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." Hivi hii inaingia akilini kweli? Kina mtu anayetaka kubakwa? Wangeandika: "Binti huyo aliyenusurika kubakwa aliokolewa na msamaria mwema..." ingeeleweka kwa usahihi wake. Lakini kwa kuwa siku hizi kwenye vyombo vya habari HAKUNA WAHARIRI, wanapitisha makosa ya AIBU kama hayo!

TUSIPOTOSHE kwa makusudi lugha yetu maridhawa, Kiswahili!

./Mwana wa Haki (Mwanafunzi wa Andanenga...)
asante kwa kutukumbusha ila hapo nilipobold nisaidie plz
 
Waungwana,


2. Watangazani wengi wa redio na luninga, na sasa hata vijana wengi, wanasema "nyimbo hii" wakiwa wanatamka juu ya "wimbo" mmoja. Tamko sahihi ni "wimbo huu". Ni Kiswahili potofu kutamka "nyimbo hii", kwani kwa usahihi, kinachopaswa kutamkwa ni "wimbo huu" au "nyimbo hizi".



TUSIPOTOSHE kwa makusudi lugha yetu maridhawa, Kiswahili!

./Mwana wa Haki (Mwanafunzi wa Andanenga...)
wakati nasoma kazi yako nilikuwa nikifikiria hili. kumbe umeliona. huwa nakereka sana pia. pia kitendo cha kuchanganya kingereza na kiswahili kukikopitiliza, huwa naumwa kichwa. unakuta mtu anasema kwa mfano, "hii nyimbo nilivyoirelease redioni ikahit sana hadi mafans wakaapreciate kazi yangu. unajua kuwa artist it takes time na kudedicte muda wako kwa what you are doing..." SHIT!

mwingine utakuta anasema, "kiukweli this time tunahitaji changes za kweli hasa ukichukulia hii trend ya ufisadi na vitu kama hivyo. kiongozi anatakiwa awe dedicated kwa wananchi. tunapokwenda kwenye hii general election lazima tufikiri in advance ni kiongozi gani atatuletea development ya kweli..." wapumbavu kama hawa ukiwaambia ongeeni kiingereza basi inakuwa tena tabu. kiswahili kibovu, kiingereza kibovu. sasa we kama si popo ni nani?
 
Back
Top Bottom