i-Business Consult
Member
- Jun 28, 2017
- 72
- 124
Habari wadau wa jukwaa letu pendwa la Biashara, Uchumi na Ujasiriamali
Leo tuangalie na kuambiana(kuelezana)namna gani kila mmoja wetu aliefanikiwa au hajafanikiwa bado katika kufanya biashara au kutoa huduma anayotoa hadi sasa. Elezea japo kwa kifupi kwani huenda ikawa chachu na ukawasisimua “inspire” wengine kufanya biashara au kutoa huduma utoayo lakini kwa njia mbadala na bora zaidi
Kuna wengine waliingia katika biashara/ujasiriamali kwa sababu mbalimbali kama vile kwa sababu ya kukosa kazi au jambo kufanya kumshughulisha kupata kipato halali, wengine ni kutokana na kukosa ajira baada ya kusota mtaani kwa muda mrefu sana hivyo kuona njia mbadala ni kujiajiri kwa kuanza kufanya biashara au ujasiriamali na kuna wengine ni kutokana na asili ya familia au koo au makabila waliyotoka mfano kama Wachaga, Wakinga na Wayao (inavyoaminika wana asili ya biashara, makabila tajwa mniwie radhi ni mfano tu) na kadhalika
Kwa mleta mada nikiwa mchangiaji wa kwanza kwa ufupi tu sikuingia moja kwa moja katika biashara/ujasiriamali bali nilianza kwa kuajiriwa hadi kufikia kiwango cha SME Loan Officer Specialist katika taasisi ya fedha.
Baadae niliachana na kazi hii baada ya kugundua nina uwezo wa kusimamia mambo yangu baada ya kuanzisha ‘firm’ ambayo iliniasidia kuujua kwa undani zaidi biashara/ ujasiriamai kwa vitendo kwani nkupitia maandiko mbali mbali nikaanzisha miradi kama wa kuku wa kienyeji idadi elfu 4 na baadae biashara za mazao kuuza na kununua, biashara za usafirishaji (transit cargo)
Niliyojifunza na kuyaona ni kuwa biashara na ujasiriamali unahitaji kuwa na jitihada, nidhamu na juhudi za dhati kwa kila ufanyalo pasina kuhofu nini kitatokea (risks). Vile vile suala la aibu imekuwa mojawapo kati ya sababu za vijana wengi kutofanikiwa, kijana anaona aibu ataonekana mmachinga kutangaza bidhaa yake. Hii ni kwa kifupi sana lakini safari ni ndefu!!
Je nawe tuambie/tuelezee kwa nini wafanya biashara unayofanya leo?
karibuni
Leo tuangalie na kuambiana(kuelezana)namna gani kila mmoja wetu aliefanikiwa au hajafanikiwa bado katika kufanya biashara au kutoa huduma anayotoa hadi sasa. Elezea japo kwa kifupi kwani huenda ikawa chachu na ukawasisimua “inspire” wengine kufanya biashara au kutoa huduma utoayo lakini kwa njia mbadala na bora zaidi
Kuna wengine waliingia katika biashara/ujasiriamali kwa sababu mbalimbali kama vile kwa sababu ya kukosa kazi au jambo kufanya kumshughulisha kupata kipato halali, wengine ni kutokana na kukosa ajira baada ya kusota mtaani kwa muda mrefu sana hivyo kuona njia mbadala ni kujiajiri kwa kuanza kufanya biashara au ujasiriamali na kuna wengine ni kutokana na asili ya familia au koo au makabila waliyotoka mfano kama Wachaga, Wakinga na Wayao (inavyoaminika wana asili ya biashara, makabila tajwa mniwie radhi ni mfano tu) na kadhalika
Kwa mleta mada nikiwa mchangiaji wa kwanza kwa ufupi tu sikuingia moja kwa moja katika biashara/ujasiriamali bali nilianza kwa kuajiriwa hadi kufikia kiwango cha SME Loan Officer Specialist katika taasisi ya fedha.
Baadae niliachana na kazi hii baada ya kugundua nina uwezo wa kusimamia mambo yangu baada ya kuanzisha ‘firm’ ambayo iliniasidia kuujua kwa undani zaidi biashara/ ujasiriamai kwa vitendo kwani nkupitia maandiko mbali mbali nikaanzisha miradi kama wa kuku wa kienyeji idadi elfu 4 na baadae biashara za mazao kuuza na kununua, biashara za usafirishaji (transit cargo)
Niliyojifunza na kuyaona ni kuwa biashara na ujasiriamali unahitaji kuwa na jitihada, nidhamu na juhudi za dhati kwa kila ufanyalo pasina kuhofu nini kitatokea (risks). Vile vile suala la aibu imekuwa mojawapo kati ya sababu za vijana wengi kutofanikiwa, kijana anaona aibu ataonekana mmachinga kutangaza bidhaa yake. Hii ni kwa kifupi sana lakini safari ni ndefu!!
Je nawe tuambie/tuelezee kwa nini wafanya biashara unayofanya leo?
karibuni