Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Siku zote nakumbuka jambo moja la utundu sana nililofanya nikiwa mdogo ambalo sintakaa nilisahau. Ni kwamba kulikuwa na nyaya za umeme nje ya nyumba ambazo zilikuwa zimekatwa na ziko wazi, Na siku zote tulijua kwamba hizo nyaya zilikuwa na umeme, na nikawa wa kwanza kuwaambia watoto wenzangu wasiziguse.
Lakini sijui nilipata wazo gani pale ambapo nilitoa bamia yangu na kuamua kuzikojolea! Naambiwa kelele niliyopiga ilikuwa ya kutisha kama ya mnyama ambaye hajawahi kugunduliwa. Bila kutambua nilijikuta nimelala chini mbali na sehemu nilipokuwa nimesimama, ambapo bila kujitambua nilimalizia mkojo wangu kwenye kaptula!
Lakini sijui nilipata wazo gani pale ambapo nilitoa bamia yangu na kuamua kuzikojolea! Naambiwa kelele niliyopiga ilikuwa ya kutisha kama ya mnyama ambaye hajawahi kugunduliwa. Bila kutambua nilijikuta nimelala chini mbali na sehemu nilipokuwa nimesimama, ambapo bila kujitambua nilimalizia mkojo wangu kwenye kaptula!