tuandike mazuri ya ballali kwa tanzania


Ndugu yangu, acha hizo, ukiulizwa ushahidi unao utatuletea, au ndio unafata mkumbo tu, watu watakachozungumza na wewe, mwisho wa siku watu watasema na wewe fisadi je utakubali tukunyonge?????/

Acha kuhukumu watu ndugu, hujafa hujaumbika, Mimi nina imani jamaa wamemtoa KAFARA yeye alikuwa nafata ORDER kutoka kwa mabosi zake, hawezi kuambiwa na bosi wake fanya hiki yeye akakataa atakuwa amekiuka taratibu za kazi yake, hata wewe bosi wako akikupa maelekezo utoe pesa ulipe sehemu utakataa???????

Wamemuacha jamaa aje ajitetee na awaseme wote ambao wamehusika na hili ingekuwa vizuri zaidi.

Nawakilisha.
 
Domo Kaya


We domokaya, Acha unafiki. Unahitaji ushahidi gani zaidi ya ule ulokuwepo mbele ya umma na wa kimazingira? Unataka kusema CCM walivunja Benk kuu kuiba pesa kupeleka uchaguzi? walioiba pesa za EPA walimshikia Bunduki? alisign kwa ridhaa yake akijua inayoumia ni nchi na si yeye na makuwadi wake.
Na ninasema wazi hao CCM hawajafanya kosa kumpika supu. sawa kabisa!! Mkubwa na msomi mzima unakubali kutumika? amefanya shirika la kimataifa kwa miaka kibao anakuja kuuza utu wake kwa wanasiasa wajinga?

Angefanya moja tu na angeheshimika na angekuwa hai mapaka leo hii nalo ni: ANGEJIUZULU !!! CCM walipotaka kumtumia kuiibia nchi angeacha kazi. kama angeresgn angekuwa mtu anayelaaniwa hivi leo kiasi kwamba anazikwa huko na wazungu na mbwa wachache?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…